Tanzania hatuna shule inayovaa sare ya aina hii. Acheni kuichafua na kuipaka matope Serikali yetu iliyojenga madarasa bora mpaka vijijini huko

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Jul 28, 2022
28,684
20,581
Ndugu zangu Watanzania,

Kumekuwa na utamaduni na tabia ya baadhi ya watanzania wachache wenye wivu na chuki binafsi za kuchukua picha mitandaoni kutoka Nchi za nje ya Tanzania na kuziweka mtandaoni na kusema ni Tanzania.

Picha hizo zimekuwa ni zile zenye kuchafua Taswira nzuri ya maendeleo na mafanikio tuliyoyapata na kufikia kama Taifa. Imekuwa ni kawaida kuona mtu anachukua picha ya wanafunzi au kipande cha barabara kibovu na kisicho pitika kutoka nchi fulani barani Afrika Na kusema ni Tanzania.

Lengo likiwa ni kuichafua na kuipaka Matope serikali yetu na kuonyesha kuwa haifanyi kazi. Jambo ambalo siyo la kweli hata kidogo. Kwa kuwa Watanzania wote wanafahamu namna serikali ilivyofanya kazi kubwa ya kusogeza huduma za kijamii karibu kabisa ya Mwananchi zenye ubora wa kiwango cha juu.


Screenshot_20250211-124415_1.jpg


Kuna picha hiyo hapo juu watu wameiweka mtandaoni ikionyesha wanafunzi waliovalia sare nyekundu kwa upande wa sketi na suruali pamoja na shati jeupe na kusema kuwa ni Tanzania wakiwa wamekaa kwenye matofali na darasa bovu la miti na lililokandikwa kwa udongo huku likiwa linapitisha Maji Matupu chini . Jambo hilo ni la uongo kwa sababu hakuna sare ya aina hiyo inayotumika na kuvaliwa na wanafunzi katika shule za serikali kwa upande wa shule za Msingi.

Rai yangu ni kuwaasa na kuwataka watanzania kuacha tabia hiyo mbaya na isiyokubalika ya kuichafua na kuipaka Matope serikali yetu kwa chuki binafsi. Tuache kueneza upotoshaji na habari za uongo kwa malengo Binafsi. Tuendelee kuiunga Mkono serikali yetu na kushiriki katika shughuli za maendeleo pamoja na kulinda Miundombinu na miradi ambayo imekuwa ikijengwa kila kona ya Nchi yetu pasipo kumchangisha hata mia Mwananchi.

Embu Tazama hapa kama Sample Namna serikali yetu ilivyojenga shule kwa ubora na kuvutia Utafikiri ulaya pasipo kuomba michango kutoka kwa watanzania.

Screenshot_20250211-125939_1.jpg
Screenshot_20250211-125416_1.jpg


Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
 
Safi kabisa, hayo ni matokeo ya kodi zetu sisi wenyewe watanzania, Rais au mbunge hana hela mfukoni, ni fedha zetu kodi yetu Hiyo 🤔🤔
Kwani Nchi ambazo wanafunzi wao wanakaa chini na kukosa madarasa na huduma zingine.Je wao hawakusanyi kodi? Tujifunze kupongeza pale serikali inapofanya vizuri.
 
Kwani Nchi ambazo wanafunzi wao wanakaa chini na kukosa madarasa na huduma zingine.Je wao hawakusanyi kodi? Tujifunze kupongeza pale serikali inapofanya vizuri.
Kukosoa na kupongeza vyote viende sambamba

Shida ni wewe, kazi yako wewe ni kupongeza tu na hukosowi

Kwa nini unawakasirikia wanaokosoa?

Wewe sitiki kwenye eneo lako la kupongeza, waache wanaookosoa nao waendelee
 
Kwani Nchi ambazo wanafunzi wao wanakaa chini na kukosa madarasa na huduma zingine.Je wao hawakusanyi kodi? Tujifunze kupongeza pale serikali inapofanya vizuri.
Hakuna kupongeza,Maana ni wajibu wao na wametuchelewesha sana. Miaka 60 ya uhuru na nchi Ina rasilimali Kibao,bado mnatuletea picha za kawaida sana ambazo wenzetu nchi zenye viongozi wanaojitambua,mambo haya waliyamaliza miaka20 iliyopita.
 
Hakuna kupongeza,Maana ni wajibu wao na wametuchelewesha sana. Miaka 60 ya uhuru na nchi Ina rasilimali Kibao,bado mnatuletea picha za kawaida sana ambazo wenzetu nchi zenye viongozi wanaojitambua,mambo haya waliyamaliza miaka20 iliyopita.
Unaposema wajibu unamaanisha nini? Kwani Nchi ngapi zimeshindwa kutimiza wajibu wao? Kwanini usipongeze kwa kazi nzuri iliyofanywa na serikali yetu?
 
Kukosoa na kupongeza vyote viende sambamba

Shida ni wewe, kazi yako wewe ni kupongeza tu na hukosowi

Kwa nini unawakasirikia wanaokosoa?

Wewe sitiki kwenye eneo lako la kupongeza, waache wanaookosoa nao waendelee
Ukosoaji wa kufanya upotoshaji wa makusudi kwa kuweka taarifa za uongo na uzushi . zisizo na uhalisia inakuwa ni jambo baya na lisilokubalika kabisa
 
Ndugu zangu Watanzania,

Kumekuwa na utamaduni na tabia ya baadhi ya watanzania wachache wenye wivu na chuki binafsi za kuchukua picha mitandaoni kutoka Nchi za nje ya Tanzania na kuziweka mtandaoni na kusema ni Tanzania.

Picha hizo zimekuwa ni zile zenye kuchafua Taswira nzuri ya maendeleo na mafanikio tuliyoyapata na kufikia kama Taifa. Imekuwa ni kawaida kuona mtu anachukua picha ya wanafunzi au kipande cha barabara kibovu na kisicho pitika kutoka nchi fulani barani Afrika Na kusema ni Tanzania.

Lengo likiwa ni kuichafua na kuipaka Matope serikali yetu na kuonyesha kuwa haifanyi kazi. Jambo ambalo siyo la kweli hata kidogo. Kwa kuwa Watanzania wote wanafahamu namna serikali ilivyofanya kazi kubwa ya kusogeza huduma za kijamii karibu kabisa ya Mwananchi zenye ubora wa kiwango cha juu.

Kuna picha hii 👉View attachment 3233233watu wameiweka mtandaoni ikionyesha wanafunzi waliovalia sare nyekundu kwa upande wa sketi na suruali pamoja na shati jeupe na kusema kuwa ni Tanzania wakiwa wamekaa kwenye matofali na darasa bovu la miti na lililokandikwa kwa udongo huku likiwa linapitisha Maji Ma tupu chini . Jambo hilo ni la uongo kwa sababu hakuna sare ya aina hiyo inayotumika na kuvaliwa katika shule za serikali kwa upande wa shule za Msingi.

Rai yangu ni kuwaasa na kuwataka watanzania kuacha tabia hiyo mbaya na isiyokubalika ya kuichafua na kuipaka Matope serikali yetu kwa chuki binafsi. Tuache kueneza upotoshaji na habari za uongo kwa malengo Binafsi. Tuendelee kuiunga Mkono serikali yetu na kushiriki katika shughuli za maendeleo kwa kulinda Miundombinu ambayo imekuwa ikijengwa kila kona ya Nchi yetu pasipo kumchangisha hata mia Mwananchi.

Embu Tazama hapa kama Sample Namna serikali yetu ilivyojenga shule kwa ubora na kuvutia Utafikiri ulaya pasipo kuomba michango kutoka kwa watanzania.View attachment 3233120View attachment 3233121

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Wewe ni hasara kwa wazazi wako na Taifa.

Samia mwenyewe Hawezi ikataa hiyo picha we unakataa vipi?
 
Back
Top Bottom