Tanzania haina mufti!Tanzania haina sheikh mkuu

Chifu mkuu

JF-Expert Member
Jan 6, 2025
220
181
TANZANIA HAINA MUFTI !
TANZANIA HANA SHEKH MKUU!

Kwa muda mrefu tumekuwa tukisikia kiongozi mkuu wa taasisi ya kidini iitwayo Baraza kuu la waislamu wa Tanzania bara akitajwa kama mufti na sheikh mkuu wa Tanzania na mtazamo huu ni makosa makubwa sana na uamebeba maudhui ya upotoshaji kwa kumvika mtu cheo ambacho kiuhalisia hakipo na hakiwezekani kuwepo kwa sababu zifuatazo;

..... Inaendelea.

3️⃣ Sababu ya tatu kwanini Tanzania haina Mufti wala sheikh mkuu ni kwakuwa vilevile serikali ya Tanzania haina dini maalumu inayofuatwa na serikali na imeruhusu watanzania wafuate dini wanazozitaka.
Swala la kuabudu na kuwa na dini lipo nje ya shughuli na majukumu ya kiserikali.
Watanzania wamegawanyika katika dini na madhehebu yenye taasisi tafautitafauti.
Waislamu wapo madhehebu tafauti tafauti na chini ya kila dhehebu kuna taasisi tafauti tafauti zilizosajiliwa serikalini.
Baadhi ya madhehebu ya dini ya kikristo/kikristu hapa Tanzania ni Roman Catholic, Lutheran, Anglican, Pentecostal, wasabato nk. Sasa wakristo wao wanapotajwa viongozi wao utasikia ASKOFU WA JIMBO KATOLIKI MKOA WA DAR ES SALAAM, DAYOSISI FULANI, PAROKIA AU USHARIKA FULANI!
Walutheri hivyohivyo utasikia ASKOFU WA KKKT ( Kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania ) Kanda au dayosisi ya mashariki nk.
Upande wa wasabato hivyo atatajwa kuwa ni mchungaji wa kanisa la kisababto, au la kipentekoste, la ufufuo na uzima nk.
Hatujasikia kuwepo ASKOFU MKUU WA TANZANIA bila kutaja wa kanisa gani, na eneo gani!
Wala hatujasikia KARDINALI MKUU WA TANZANIA bila kuongeza kwamba ni wa kanisa katoliki.Hata papa wa huko vitikani hutajwa kama KIONGOZI WA KANISA KATOLIKI DUNIANI , SIO KIONGOZI WA DUNIA AU KIONGOZI WA WAKRISTO WOTE DUNIANI.
Kiongozi wa KANISA KATOLIKI.
Kila kinasa linapomtaja kiongozi wake lazima wataje na jina la kanisa analoliongoza na Kanda,mkoa, parokia, dayosisi au kigango anachoongoza.
Ni BAKWATA PEKE YAKE INAYOMTAJA KIONGOZI WAKE MKUU KAMA MUFTI NA SHEIKH MKUU WA TANZANIA kama vile watanzania wa dini zote na madhehebu yote wako chini yake!
Ni bakwata peke yake inaowataja viongozi wake wa mikoa kama MASHEIKH WA MIKOA bila kutaja wa dini gani au madhehebu na taasisi gani kama vile raia wa dini zote waliomo kwenye mkoa huo wapo nyuma yake!!.

NITOE MFANO.
Ukisema jaji mkuu wa Tanzania tunaelewa kuwa unamzungumzia kiongozi anayewatumikia watanzania wote wa dini , madhehebu, makabila na vyama vyote vya kisiasa na kijamii katika sekta ya mahakama chini ya wizara ya katiba na sheria Tanzania nzima.
Ukisema mkuu wa mkoa wa Mwanza unamaanisha mtu anayemuwakilisha mh Rais katika mkoa wa Mwanza akiwa mtumishi wa watu wa dini, madhehebu, makabila na vyama vyote!.
Ukisema mwenyekiti wa CCM taifa, mkoa au wilaya tunajua unamzungumzia kiongozi wa chama maalumu cha siasa anayewaongoza wanachama wa chama hicho katika nafasi iliyotajwa na sio kiongozi wa watanzania wote.
Upande wa taasisi za kidini ni hivyo hivyo lazima itajwe taasisi hiyo na nafasi ya kila muhusika.
Nimetoa mifano ya taasisi za kikristo hapa Tanzania zinavyowatambulisha viongozi wake.
Ni BAKWATA PEKE YAKE ambayo viongozi wake utasikia MUFTI NA SHEIKH MKUU WA TANZANIA.
JE ni mtumishi wa watanzania wote kama ilivyo JAJI MKUU WA TANZANIA?!
Je Mufti wa Tanzania anafanya kazi chini ya wizara gani na kwa sheria gani?!
Ili kuweka mambo sawa kuna nukta zifuatazo .

A. Kwakuwa taasisi hii haina wala haitakiwi kuwa na ofisi Zanzibar kwa kuwa Tayari waislamu wa zanzibar wanayo taasisi inayosimamia mambo yao ya kidini chini ya serikali ya mapinduzi ya Zanzibar jina la taasisi hii yatakiwa liwe BARAZA KUU LA WAISLAMU WA TANGANYIKA
( au Tanzania bara)

B. Yatakiwa kiongozi wao mkuu ajulikane kama MUFTI NA SHEIKH MKUU WA BAKWATA na siyo mufti na sheikh mkuu wa Tanzania.
 
Katika Uislamu, "Mufti Mkuu" ni mwanachuoni wa ngazi ya juu anayetoa maamuzi ya kisheria (fatwa) kulingana na mafundisho ya Kiislamu. Kazi yake ni kuelekeza Waislamu katika masuala ya dini kwa mujibu wa Qur'an, Hadithi, Ijma' (makubaliano ya wanazuoni), na Qiyas (kulinganisha na hukumu zilizopo).

Katika ngazi ya kimataifa, hakuna Mufti Mkuu mmoja kwa Waislamu wote, kwani kila nchi au eneo lina Mufti wake Mkuu. Kwa mfano:

Saudi Arabia – Mufti Mkuu wa Saudi Arabia ndiye kiongozi wa Baraza la Wanazuoni Wakuu wa nchi hiyo.

Misri – Mufti Mkuu wa Misri huongoza taasisi kama Dar al-Ifta na kutoa fatwa za kitaifa.

Tanzania – Kuna Mufti Mkuu wa Tanzania ambaye ni kiongozi wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA).

Zanzibar – Mufti Mkuu wa Zanzibar huongoza masuala ya Kiislamu ndani ya Zanzibar.
 
Kuna sheik wa ccm na mufti wa ccm.
Kuna wasanii kupitia ccm.
Kuna waropokaji kupitia ccm.
Kuna idadi ya chawa kupitia ccm.
 
Katika Uislamu, "Mufti Mkuu" ni mwanachuoni wa ngazi ya juu anayetoa maamuzi ya kisheria (fatwa) kulingana na mafundisho ya Kiislamu. Kazi yake ni kuelekeza Waislamu katika masuala ya dini kwa mujibu wa Qur'an, Hadithi, Ijma' (makubaliano ya wanazuoni), na Qiyas (kulinganisha na hukumu zilizopo).

Katika ngazi ya kimataifa, hakuna Mufti Mkuu mmoja kwa Waislamu wote, kwani kila nchi au eneo lina Mufti wake Mkuu. Kwa mfano:

Saudi Arabia – Mufti Mkuu wa Saudi Arabia ndiye kiongozi wa Baraza la Wanazuoni Wakuu wa nchi hiyo.

Misri – Mufti Mkuu wa Misri huongoza taasisi kama Dar al-Ifta na kutoa fatwa za kitaifa.

Tanzania – Kuna Mufti Mkuu wa Tanzania ambaye ni kiongozi wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA).

Zanzibar – Mufti Mkuu wa Zanzibar huongoza masuala ya Kiislamu ndani ya Zanzibar.
Tanzania haina mufti mdogo wala mufti mkuu! Bakwata wana kiongozi wao mkuu ambaye cheo chake anaitwa mufti na sheikh mkuu.
Kwahiyo huyo ni mufti wa Bakwata na siyo mufti wa Tanzania.
Moja ya hoja ni kwamba Tanzania ni kubwa na pana zaidi kuliko bakwata.
Mipaka ya Tanzania inavizunguka hadi visiwa vya unguja na pemba.
Bakwata haina ofisi, kazi wala mwakilishi yeyote katika visiwa vya unguja na pemba! Tanzania bila Zanzibar haiitwi Tanzania bali ni Tanzania bara au Tanganyika.
Pia fuatilia sababu nilizozitaja namba 2 na namba 3 kwanini Tanzania haina Mufti.
 
Na Kuna madhehebu mengi ya waislamu,inabidi watofautishe

Kuna madhehebu kama Shia,Sunni,wahamadiya , n.k

Kuna vikundi kama Wahabi, Salafi, waismalia,n.k
 
TANZANIA HAINA MUFTI !
TANZANIA HANA SHEKH MKUU!

Kwa muda mrefu tumekuwa tukisikia kiongozi mkuu wa taasisi ya kidini iitwayo Baraza kuu la waislamu wa Tanzania bara akitajwa kama mufti na sheikh mkuu wa Tanzania na mtazamo huu ni makosa makubwa sana na uamebeba maudhui ya upotoshaji kwa kumvika mtu cheo ambacho kiuhalisia hakipo na hakiwezekani kuwepo kwa sababu zifuatazo;

..... Inaendelea.

3️⃣ Sababu ya tatu kwanini Tanzania haina Mufti wala sheikh mkuu ni kwakuwa vilevile serikali ya Tanzania haina dini maalumu inayofuatwa na serikali na imeruhusu watanzania wafuate dini wanazozitaka.
Swala la kuabudu na kuwa na dini lipo nje ya shughuli na majukumu ya kiserikali.
Watanzania wamegawanyika katika dini na madhehebu yenye taasisi tafautitafauti.
Waislamu wapo madhehebu tafauti tafauti na chini ya kila dhehebu kuna taasisi tafauti tafauti zilizosajiliwa serikalini.
Baadhi ya madhehebu ya dini ya kikristo/kikristu hapa Tanzania ni Roman Catholic, Lutheran, Anglican, Pentecostal, wasabato nk. Sasa wakristo wao wanapotajwa viongozi wao utasikia ASKOFU WA JIMBO KATOLIKI MKOA WA DAR ES SALAAM, DAYOSISI FULANI, PAROKIA AU USHARIKA FULANI!
Walutheri hivyohivyo utasikia ASKOFU WA KKKT ( Kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania ) Kanda au dayosisi ya mashariki nk.
Upande wa wasabato hivyo atatajwa kuwa ni mchungaji wa kanisa la kisababto, au la kipentekoste, la ufufuo na uzima nk.
Hatujasikia kuwepo ASKOFU MKUU WA TANZANIA bila kutaja wa kanisa gani, na eneo gani!
Wala hatujasikia KARDINALI MKUU WA TANZANIA bila kuongeza kwamba ni wa kanisa katoliki.Hata papa wa huko vitikani hutajwa kama KIONGOZI WA KANISA KATOLIKI DUNIANI , SIO KIONGOZI WA DUNIA AU KIONGOZI WA WAKRISTO WOTE DUNIANI.
Kiongozi wa KANISA KATOLIKI.
Kila kinasa linapomtaja kiongozi wake lazima wataje na jina la kanisa analoliongoza na Kanda,mkoa, parokia, dayosisi au kigango anachoongoza.
Ni BAKWATA PEKE YAKE INAYOMTAJA KIONGOZI WAKE MKUU KAMA MUFTI NA SHEIKH MKUU WA TANZANIA kama vile watanzania wa dini zote na madhehebu yote wako chini yake!
Ni bakwata peke yake inaowataja viongozi wake wa mikoa kama MASHEIKH WA MIKOA bila kutaja wa dini gani au madhehebu na taasisi gani kama vile raia wa dini zote waliomo kwenye mkoa huo wapo nyuma yake!!.

NITOE MFANO.
Ukisema jaji mkuu wa Tanzania tunaelewa kuwa unamzungumzia kiongozi anayewatumikia watanzania wote wa dini , madhehebu, makabila na vyama vyote vya kisiasa na kijamii katika sekta ya mahakama chini ya wizara ya katiba na sheria Tanzania nzima.
Ukisema mkuu wa mkoa wa Mwanza unamaanisha mtu anayemuwakilisha mh Rais katika mkoa wa Mwanza akiwa mtumishi wa watu wa dini, madhehebu, makabila na vyama vyote!.
Ukisema mwenyekiti wa CCM taifa, mkoa au wilaya tunajua unamzungumzia kiongozi wa chama maalumu cha siasa anayewaongoza wanachama wa chama hicho katika nafasi iliyotajwa na sio kiongozi wa watanzania wote.
Upande wa taasisi za kidini ni hivyo hivyo lazima itajwe taasisi hiyo na nafasi ya kila muhusika.
Nimetoa mifano ya taasisi za kikristo hapa Tanzania zinavyowatambulisha viongozi wake.
Ni BAKWATA PEKE YAKE ambayo viongozi wake utasikia MUFTI NA SHEIKH MKUU WA TANZANIA.
JE ni mtumishi wa watanzania wote kama ilivyo JAJI MKUU WA TANZANIA?!
Je Mufti wa Tanzania anafanya kazi chini ya wizara gani na kwa sheria gani?!
Ili kuweka mambo sawa kuna nukta zifuatazo .

A. Kwakuwa taasisi hii haina wala haitakiwi kuwa na ofisi Zanzibar kwa kuwa Tayari waislamu wa zanzibar wanayo taasisi inayosimamia mambo yao ya kidini chini ya serikali ya mapinduzi ya Zanzibar jina la taasisi hii yatakiwa liwe BARAZA KUU LA WAISLAMU WA TANGANYIKA
( au Tanzania bara)

B. Yatakiwa kiongozi wao mkuu ajulikane kama MUFTI NA SHEIKH MKUU WA BAKWATA na siyo mufti na sheikh mkuu wa Tanzania.
Hayo mambo yenu myamalize wenyewe... Hatutaki migogoro sisi...

Tunamchagua mama kwa kishindo 2925
 
Ishu ni kwamba nyie wenyewe waislam hamjitambui, huwa mnasema uislam ni mmoja. Kwa mtazamo wa uislam ni mmoja basi mufti aliyepo ndiyo kiongozi mkuu wa waislam wote Tanzania, na baraza ni moja tu BAKWATA
 
Huwa mnapotezea kuwa hamna madhehebu huku tunawaona wengine wakiitwa answar sunn, mabohora, ismailiyyah, aga khan na wana jumuiya zao kama jumuiya na taasisi za kiislam tanzania katibu ni sheikh ponda, kuna jumuiya ya mabohora, jumuiya ya ismailiya, jumuiya ya aga khan ongeza na ile shura ya maimam hawa sijui ni wa jumuiya gani kama si wa BAKWATA. Waislam hamueleweki wazi kama ulivyodadavua vema kwa wakristo wanatambuana vema kwa madhehebu yao
 
Ishu ni kwamba nyie wenyewe waislam hamjitambui, huwa mnasema uislam ni mmoja. Kwa mtazamo wa uislam ni mmoja basi mufti aliyepo ndiyo kiongozi mkuu wa waislam wote Tanzania, na baraza ni moja tu BAKWATA
Anayesema uislamu ni mmoja mm i MUONGO!
Mbona tunapishana siku za kufunga na kufungua mwezi wa Ramadhani?
Mbona wengine wanafanya sherehe za maulidi na wengine tunapinga sherehe hizo ?!
Mbona kuna wanaofanya matanga kumaliza misiba kwa kujumuka na kula vyakula vya pamoja na wengine tunapinga matanga ?!
Mbona kuna masheikh wanaohalalisha ushirikina wa kufuga majini, kupiga ramli na kuabudu makaburi na waislamu wengine tunapinga?!
Waislamu wenyewe kwa wenyewe tunapishana mambo mengi ya kiitikadi, kiibada na MIFUMO ila kama wewe sio muislamu unayeufatilia uislamu na waislamu huwezi kuelewa. Hata kwa wakristo sio wamoja.
Wakatoliki wana viongozi wao , walutheri wana viongozi wao, Wasabato wana viongozi wao na wapentecost , waothordox nao Wana viongozi wao!. Sasa hoja yangu ni kwamba huyo ambaye watu wanamuita shehe mkuu yatakiwa aitwe Mufti na shehe mkuu wa bakwata waliomchagua.
 
Hapa Tanzania waislam hawaeleweki ni wa shia au sunni, wale kina ponda itakuwa ni sunni na hawa BAKWATA itakuwa ni shia, bado wale mabohora, ismailiya, aga khani na wahabbi. Utambulisho wa viongozi wao kitaifa inakuwa utata kuwataja kirahisi kama viongozi wa madhehebu ya kikristo
 
Back
Top Bottom