Spika Tulia, ukweli wa aliyosema Mpina haubatilishwi kwa kumkasirikia kwamba amekiuka kanuni za Bunge na kudai hakuheshimu!

Synthesizer

Platinum Member
Feb 15, 2010
11,780
20,298
Wala haihitaji akili kubwa sana kuona kwamba Spika wa Bunge Tulia na jopo zima la uongozi wa serikali wametambua kwamba Mpina amewaumbua kwa kuweka wazi uongo wanaoufanya kuwahadaa Watanzania. Na sasa wanataka kubadilisha uzito wa tuhuma za uongo wa Waziri Bashe na kuelekeza fikra kwa ukiukwaji wa utaratibu wa Mpina.

Tuseme ukweli, mbele ya macho ya Watanzania, nani mwenye kosa kubwa na baya zaidi kati ya Bashe na Mpina? Na kama Tulia anaona Mpina haheshimu u-Spika wako wa Bunge la Tanzania dunia, anaona Bashe anauheshimu zaidi ya Mpina kwa kusema uongo huku akimwangalia bila hata kupepesa macho?

Kosa la Mpina, kama ni kosa, ni kuanika uongo wa Bashe hadharani. Kosa la Bashe ni kuwadanganya Watanzania katika jambo ambalo lina kila dalili za ufisadi na uvunjaji sheria. Sasa kwa nini Tulia kama Spika anaweka nguvu nyingi dhidi ya Mpina kuliko mtuhumiwa wa uongo Bashe? Kosa la Mpina ni kosa dhidi yako kama Spika wa Bunge, na kosa na Bashe ni kosa dhidi ya Watanzania wote. Sasa nani mhalifu zaidi kati ya hawa wawili? Nani anapaswa kwenda kamati ya Bunge ya maadili kwa haraka iwezekanavyo?

Pendekezo langu kama Mtanzania alieyedanganywa ama mtoto na waziri Bashe, ni kwamba hili la Mpina kukiuka taratibu za Bunge tuliweke pembeni kwanza. Tumalize lile lililotangulia na lililo jambo kuu hapa - uongo wa Bashe kwa Bunge na kwa Watanzania. Tukimaliza kushughulika na Bashe, basi ndio tuje turudi kwa Mpina - kama kweli alichofanya ni kosa kubwa kiasi ambacho Spika Tulia anataka kutuambia. Bunge ni la wananchi, sio la Spika na Raisi, kwa hiyo sisi kama wananchi tuna haki ya kupata ufafanuzi wa Mpina dhidi ya uongo wa Bashe kwa Bunge letu.

Sisi kama Watanzania, tuko tayari kuvumilia na kusamehe Tulia anachoona ni kosa la Mpina kuliko kosa la Bashe.

Halafu jambo jingine kwa Tulia - heshima hailazimishwi, inakuja yenyewe tu kutokana na matendo na personality yako. Unaweza kuwa Spika wa Bunge la Tanzania na dunia au hata ulimwengu, sasa kuheshimiwa na watu si jambo la kulazimisha. Hii philosophy ya "unanijua mimi ni nani" ni ya kitoto sana, na inatumiwa na watu ambao hawajaelimika hata kama ni maprofessor, watu wasiojiamini au watu waliotoka katika maisha duni na kufikia kuwa maarufu.
 
Wala haihitaji akili kubwa sana kuona kwamba Spika wa Bunge Tulia na jopo zima la uongozi wa serikali wametambua kwamba Mpina amewaumbua kwa kuweka wazi uongo wanaoufanya kuwahadaa Watanzania. Na sasa wanataka kubadilisha uzito wa tuhuma za uongo wa Waziri Bashe na kuelekeza fikra kwa ukiukwaji wa utaratibu wa Mpina.

Tuseme ukweli, mbele ya macho ya Watanzania, nani mwenye kosa kubwa na baya zaidi kati ya Bashe na Mpina?

Kosa la Mpina, kama ni kosa, ni kuanika uongo wa Bashe hadharani. Kosa la Bashe ni kuwadanganya Watanzania katika jambo ambalo lina kila dalili za ufisadi na uvunjaji sheria. Sasa kwa nini Tulia kama Spika anaweka nguvu nyingu dhidi ya Mpina kuliko mtuhumiwa wa uongo Bashe?

Pendekezo langu kama Mtanzania alieyedanganywa ama mtoto na waziri Bashe, ni kwamba hili la Mpina kukiuka taratibu za Bunge tuliweke pembeni kwanza. Tumalize lile lililotangulia na lililo jambo kuu hapa - uongo wa Bashe kwa Bunge na kwa Watanzania. Tukimaliza kushughulika na Bashe, basi ndio tuje turudi kwa Mpina - kama kweli alichofanya ni kosa kubwa kiasi ambacho Spika Tulia anataka kutuambia.

Halafu jambo jingine Tulia - heshima hailazimishwi, inakuja yenyewe tu kutokana na matendo na personality yako. Unaweza kuwa Spika wa Bunge la Tanzania na dunia au hata ulimwengu, sasa kuheshimiwa na watu si jambo la kulazimisha. Hii philosophy ya unanijua mimi ni nani ni ya kitoto sana, inatumiwa na watu ambao hawajaelimika hata kama ni maprofessor, watu wasiojiamini.
Kwa jinsi huyu Spika alivyo mdhalimu, najua tu kwamba atamuadhibu Mbunge Luhaga Mpina aliyesema UKWELI na kumpongeza Waziri Hussein Bashe aliyesema UONGO
 
Whatever but Mpina baada ya kupigwa chini uwaziri amekuwa akitafuta huruma tu kwa wananchi Hana jipya ni njaa na hasira za kutokuwa waziri
 
Wala haihitaji akili kubwa sana kuona kwamba Spika wa Bunge Tulia na jopo zima la uongozi wa serikali wametambua kwamba Mpina amewaumbua kwa kuweka wazi uongo wanaoufanya kuwahadaa Watanzania. Na sasa wanataka kubadilisha uzito wa tuhuma za uongo wa Waziri Bashe na kuelekeza fikra kwa ukiukwaji wa utaratibu wa Mpina.

Tuseme ukweli, mbele ya macho ya Watanzania, nani mwenye kosa kubwa na baya zaidi kati ya Bashe na Mpina?

Kosa la Mpina, kama ni kosa, ni kuanika uongo wa Bashe hadharani. Kosa la Bashe ni kuwadanganya Watanzania katika jambo ambalo lina kila dalili za ufisadi na uvunjaji sheria. Sasa kwa nini Tulia kama Spika anaweka nguvu nyingu dhidi ya Mpina kuliko mtuhumiwa wa uongo Bashe? Kosa la Mpina ni kosa dhidi yako kama Spika wa Bunge, na kosa na Bashe ni kosa dhidi ya Watanzania wote. Sasa nani mhalifu zaidi kati ya hawa wawili? Nani anapaswa kwenda kamati ya Bunge ya maadili kwa haraka iwezekanavyo?

Pendekezo langu kama Mtanzania alieyedanganywa ama mtoto na waziri Bashe, ni kwamba hili la Mpina kukiuka taratibu za Bunge tuliweke pembeni kwanza. Tumalize lile lililotangulia na lililo jambo kuu hapa - uongo wa Bashe kwa Bunge na kwa Watanzania. Tukimaliza kushughulika na Bashe, basi ndio tuje turudi kwa Mpina - kama kweli alichofanya ni kosa kubwa kiasi ambacho Spika Tulia anataka kutuambia. Bunge ni la wananchi, sio la Spika na Raisi, kwa hiyo kama wananchi tuna haki ya kupata ufafanuzi wa Mpina dhidi ya uongo wa Bashe kwa Bunge letu.

Sisi kama Watanzania, tuko tayari kuvumilia na kusamehe unachoona ni kosa la Mpina kuliko kosa la Bashe.

Halafu jambo jingine Tulia - heshima hailazimishwi, inakuja yenyewe tu kutokana na matendo na personality yako. Unaweza kuwa Spika wa Bunge la Tanzania na dunia au hata ulimwengu, sasa kuheshimiwa na watu si jambo la kulazimisha. Hii philosophy ya "unanijua mimi ni nani" ni ya kitoto sana, na inatumiwa na watu ambao hawajaelimika hata kama ni maprofessor, watu wasiojiamini au watu waliotoka katika maisha duni na kufikia kuwa maarufu.
Yeye kwake anaona yale yote aliyosema tena kwa kuleta ushahidi hayana maana chenye maana ni kuheshimiwa yeye tu. Upigaji, mchezo wa sukari kupanda bei na mengine yanayowaumiza watanzania milioni 60 hayana maana kuliko heshima yake. Ni Miungu watu hawa.
 
Ili bunge ukiangalia unaweza ata ukataka kuama nchi aisee Pasua tupu
Imefikia mahali sasa hadi wananchi wanaanza kuona ni afadhali kufanya mabadiliko ya uongozi wa nchi kwa nguvu. Sasa hii ni hatari sana, tunakoenda sio kuzuri, kama hadi Bungeni watu wanahukumiwa kwa kuwa na nia nzuri na waovu wanatetewa katika ufisadi na uovu wao kwa kutumia vinpengele vidogo vidogo dhidi ya wanaofichua uovu wao na kuwafanya wanaofichua waonekane wao ndio wenye makosa makubwa zaidi
 
Tuseme ukweli, mbele ya macho ya Watanzania, nani mwenye kosa kubwa na baya zaidi kati ya Bashe na Mpina?

Kosa la Mpina, kama ni kosa, ni kuanika uongo wa Bashe hadharani. Kosa la Bashe ni kuwadanganya Watanzania katika jambo ambalo lina kila dalili za ufisadi na uvunjaji sheria. Sasa kwa nini Tulia kama Spika anaweka nguvu nyingu dhidi ya Mpina kuliko mtuhumiwa wa uongo Bashe? Kosa la Mpina ni kosa dhidi yako kama Spika wa Bunge, na kosa na Bashe ni kosa dhidi ya Watanzania wote. Sasa nani mhalifu zaidi kati ya hawa wawili? Nani anapaswa kwenda kamati ya Bunge ya maadili kwa haraka iwezekanavyo?

Pendekezo langu kama Mtanzania alieyedanganywa ama mtoto na waziri Bashe, ni kwamba hili la Mpina kukiuka taratibu za Bunge tuliweke pembeni kwanza. Tumalize lile lililotangulia na lililo jambo kuu hapa - uongo wa Bashe kwa Bunge na kwa Watanzania. Tukimaliza kushughulika na Bashe, basi ndio tuje turudi kwa Mpina - kama kweli alichofanya ni kosa kubwa kiasi ambacho Spika Tulia anataka kutuambia. Bunge ni la wananchi, sio la Spika na Raisi, kwa hiyo kama wananchi tuna haki ya kupata ufafanuzi wa Mpina dhidi ya uongo wa Bashe kwa Bunge letu.

Sisi kama Watanzania, tuko tayari kuvumilia na kusamehe unachoona ni kosa la Mpina kuliko kosa la Bashe.
Sahihi kabisa, alichofanya Mpina hata kama kweli ni kosa halina uzito wowote wala athari kwa maslahi ya taifa na raia walio wengi.
 
'Hata saa mbovu wakati mwingine huwa inasema ukweli.'
Shida ya watanzania badala ya kujadili hoja wanamjadili mtu. Yote aliyosema kaambatanisha ushahidi mpaka wa tarehe. Lakini mtu kisa mpina hampendi basi hata huo ukweli hautaki. Haijalishi kayasema kisa kanyimwa uwaziri au ana bifu na bashe, lakini pointi ya msingi je, aliyosema ni ya kweli si ya kweli? Sisi tulipaswa kuwa na msemo wa vita vya panzi furaha kwa kunguru. Yani vita vya maslahi yao vimetufanya tujue ufisadi hivyo hatua zichukuliwe.
 
Sahihi kabisa, alichofanya Mpina hata kama kweli ni kosa halina uzito wowote wala athari kwa maslahi ya taifa na raia walio wengi.
Tatizo ni kwamba uongozi wote wa Tanzania sasa umefikia kuona Wananchi ote wa Tanzania ni mbumbumbu wazungu wa reli isipokuwa Tundu Lissu na Mwabukusi!
 
Shida ya watanzania badala ya kujadili hoja wanamjadili mtu. Yote aliyosema kaambatanisha ushahidi mpaka wa tarehe. Lakini mtu kisa mpina hampendi basi hata huo ukweli hautaki. Haijalishi kayasema kisa kanyimwa uwaziri au ana bifu na bashe, lakini pointi ya msingi je, aliyosema ni ya kweli si ya kweli? Sisi tulipaswa kuwa na msemo wa vita vya panzi furaha kwa kunguru. Yani vita vya maslahi yao vimetufanya tujue ufisadi hivyo hatua zichukuliwe.
Unakumbuka madudu aliyoyafanya akiwa waziri?
 
Whatever but Mpina baada ya kupigwa chini uwaziri amekuwa akitafuta huruma tu kwa wananchi Hana jipya ni njaa na hasira za kutokuwa waziri
Mpina alichaguliwa kuwa waziri ili kumnyamazisha. Badala ya kunyamaza alianza kuwachoma sindano za makalio huko huko ndani, ikabidi atemwe ili makalio yao yasidizi kutobolewa kwa sindano za Mpina!
 
Unakumbuka madudu aliyoyafanya akiwa waziri?
Kwani yanafuta ukweli atakaousema tena kwa ushahidi. Maana mpaka sasa ushahidi aliouleta hakuna aliyeupinga ila tu mko busy kujaribu kukumbusha alifanya hivi alifanya vile. Haijalishi alifanya madudu wizarani, lakini alichokiibua na ule ushahidi ni wa kweli si wa kweli?
 
Kwani yanafuta ukweli atakaousema tena kwa ushahidi. Maana mpaka sasa ushahidi aliouleta hakuna aliyeupinga ila tu mko busy kujaribu kukumbusha alifanya hivi alifanya vile. Haijalishi alifanya madudu wizarani, lakini alichokiibua na ule ushahidi ni wa kweli si wa kweli?
Well said Mkuu! Wanajaribu kupoteza lengo kwa saikoloji ya kitoto sana. Mtu ameua, unaenda na ushahidi kumshitaki Polisi, halafu Polisi wanaanza kusema kwa nini umewaonyesha watu wengine huu ushahidi, umeonyesha dharau kwa ofisi ya Polisi, vua viatu ingia rumande!

Sasa suala la muuaji halipo tena kwa sababu ni polisi mwenzao! Ni Mtanzania mjinga tu atakubali hili
 
Whatever but Mpina baada ya kupigwa chini uwaziri amekuwa akitafuta huruma tu kwa wananchi Hana jipya ni njaa na hasira za kutokuwa waziri
Ni kweli, ila Kuna shida gani kwa kitafuta huruma huku ukiongea ukweli?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom