Soko la Kariakoo limebaki asilima chache kukamilika, zaidi ya billioni 30 zatumika

JUMA JUMA

JF-Expert Member
Jan 5, 2013
783
959
SOKO LA KARIAKOO IMEBAKI ASILIMA CHACHE KUKAMILIKA ZAIDI YA BILLIONI 30 ZATUMIKA

Ukarabati wa soko la Kariakoo umegharimu zaidi ya Bilioni 30 na zimebaki asilima chache kukamilika Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ataenda kukagua baada ya kukamilika pia ametoa fedha kwaajili ya ujenzi wa masoko likiwemo soko la Machinga Jangwani na Gongo la Mboto.

Hayo ameyasema Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mh Edward Mpogolo na kusema kuwa wao kama Halmashauri ya Jiji la Dar Es Salaam wanaenda kujenga soko la Mchikichini ambalo lina wafanyabishara zaidi ya 3000 na Soko la Ilala ambalo lina wafanyabishara zaidi ya 2000.

"Kuna baadhi ya maeneo kulikuwa na changamoto ya maji lakini Mh Rais ametupatia kiasi cha fedha zaidi ya Bilioni 36.7 , ukienda Bangulo kuna tenki kubwa la maji linajengwa litakuwa linauwezo wa kuwasambazia maji watu zaidi ya 4000 maana yake maeneo ya Tabata Segerea,Bonyokwa,Kinyerezi,Majohe Kitunda Kivule hao wote wanaenda kusaidiwa na maji hayo"amesema Dc Mpogolo

#DiraYaSamia


- Ujenzi wa soko la Kariakoo wafikia 32% likikamilika Wamachinga watarejeshwa na litafanya kazi kwa saa 24
 
Jambo jema, inamaana haiwezekani kabisa kusema serikali imetenga pesa au imetoka fungu bila kumtaja Rais? Naamini mambo mazuri yakifanywa na serikali, wananchi ni waelewa kujua kwamba Rais anachapa kazi.

Hizo picha za kuonyesha mwenendo wa ujenzi wa soko ziko wapi?
 
Back
Top Bottom