Simba kumchukulia hatua za kinidhamu Kibu Denis kwa kutokuripoti kambini

Heparin

JF-Expert Member
Sep 24, 2021
200
857
1000093220.jpg

Klabu ya Simba inautaarifu Umma kuwa mchezaji wake, Kibu Denis Prosper hajaripoti kambini kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya wa mwaka 2024/2025.

Tunapenda kuutarifu umma kuwa Simba tulimuongezea Kibu mkataba wa miaka miwili zaidi utakaoisha, Juni 2026 na kumlipa stahiki zake zote za kimkataba.

Hata hivyo, mchezaji huyu amekuwa akitoa sababu kadha wa kadha zinazomfanya kushindwa kuripoti kambini.

Kutokana na utovu huu wa kinidhamu klabu itamchukulia hatua stahiki za kinidhamu na umma utapewa taarifa.

Imetolewa na:-
Idara ya Habari na Mawasiliano, Simba Sports Club.
Julai 23, 2024
 
View attachment 3050326
Klabu ya Simba inautaarifu Umma kuwa mchezaji wake, Kibu Denis Prosper hajaripoti kambini kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya wa mwaka 2024/2025.

Tunapenda kuutarifu umma kuwa Simba tulimuongezea Kibu mkataba wa miaka miwili zaidi utakaoisha, Juni 2026 na kumlipa stahiki zake zote za kimkataba.

Hata hivyo, mchezaji huyu amekuwa akitoa sababu kadha wa kadha zinazomfanya kushindwa kuripoti kambini.

Kutokana na utovu huu wa kinidhamu klabu itamchukulia hatua stahiki za kinidhamu na umma utapewa taarifa.

Imetolewa na:-
Idara ya Habari na Mawasiliano, Simba Sports Club.
Julai 23, 2024
Kibu ni msengerema,
Kile kigoli kimoja alichomfunga Diarra bado kinampa kiburi. Hata huo mkataba mmoja alioongeza hakustahili pia. Kifupi ni "overated player".
 
Maduka ya Yanga ndani ya Simba yanaanza kujionyesha,tulipigwa 5-1 kwa ajili ya haya maduka, Saido,Kibu,Inonga ,Chama na Manula. Upande wa pili utakuwa ulirubuni wachezaji wa Simba kucheza chini ya kiwango ili iwe rahisi wao kuchukua ubingwa, rejea jamaa alivyokuwa anawapa mbinu kwa whatsapp kina Tuisila walipokuwa Morocco ili waweza kuifunga Simba.
 
Kwa mujibu wa meneja wake Kibu kasaini na amesha ingiziwa mzigo wake wote.

Tukisemaga bongo kuna uhuni mwingi sana kwenye usajili wachezaji wana jiamulia tu,juzi Fei,jana Dube leo Kibu.

Zamu yenu safari hii,za andani anasema anaenda Norway.Nahisi anaweza kufanya kama alicho fanya Fei kwa Yanga,anawawekea mzigo wenu then yy mwenyewe anajitangazia yupo free. Kipindi kile 5imba mliona sawa kwenye issue ya Fei kwa sababu ni Yanga,ila kuna uwezekano Kibu akafanya ujinga alio ufanya Fei.

Na jioni hii ya leo kuna picha zimepostiwa Kibu akiwa Airport anaelekea, Norway (Millard Ayo amepost)


View: https://m.youtube.com/watch?v=2g66y4-CEsk
Ligi yetu ina usela mwingi sana.
 
Wasilete ujinga nao, hii taarifa haikupaswa kutolewa, ni kukaa kimya kisha kufanya maamuzi kama ni faini, wampige faini, sie watupe taarifa ya faini sio hizi porojo hapa ni kama mikwara kwa kibu.
Mkipewa taarifa rasmi shida msipopewa mkabaki na tetesi na minong'ono shida vile vile.

Watu kama nyinyi hamueleweki mnachotaka.

Simba wamefanya jambo zuri kuutarifu umma kwakuwa timu ni ya wanachama na mashabiki sio ya viongozi pekee.
 
Watetezi wa Kibu D karibuni kwa maoni.
Kumtetea mpuuzi kama huyo ni upuuzi
Mkipewa taarifa rasmi shida msipopewa mkabaki na tetesi na minong'ono shida vile vile.

Watu kama nyinyi hamueleweki mnachotaka.

Simba wamefanya jambo zuri kuutarifu umma kwakuwa timu ni ya wanachama na mashabiki sio ya viongozi pekee.
Wapi nilitaka taarifa ya kibu.

Kiukweli simba hapo wameboronga, taarifa hii ni kama mkwara tu kwa kibu, wangetoa taarifa ya maamuzi yao ingependeza
 
Back
Top Bottom