Rwanda wameweza kuzuia makanisa kuenea kama uyoga

ngara23

JF-Expert Member
Aug 31, 2019
9,850
22,520
Naipongeza Serikali ya Rwanda kuona mbali na kuweka utaratibu mzuri wa makanisa, Misikiti na taasisi za dini

Rwanda imefungia zaidi ya makanisa 600,

Kabla walipiga marufuku matumizi ya azana Kwa Misikiti kuwa unaleta usumbufu Kwa wasio kuwa wa Imani hiyo na kuweka ustaarabu wa kuitana Kwa alarm

Sio alfajiri unapiga ukunga na watu wamepumzika

Taratibu za kufungua kanisa Rwanda

1. Elimu
Lazima mwanzilishi wa Kanisa na wachungaji waandamizi wawe na degree ya teolojia.

Sio kuamka na darasa la 7 yako eti Mungu amekuita uwe nabii na ufungue kanisa
Mwishowe unaanza mahubiri ya Zumaridi, kuuza mafuta na chumvi ya upako au kuamuru waumini kufunga hadi kufa

2. Miundo wa uongozi
Kanisa linatakiwa liwe na mfumo wa uongozi yani liwe taasisi sio mali ya mtu binafsi.
Kwa Hapa nawapongeza wenzetu waislam, hakuna Misikiti unaomilikiwa na shehe Fulani

3 Uungwaji mkono
Mchungaji anayeanzisha kanisa atatakiwa apate idadi ya watu wasiopungua 1000 katika wilaya yake. Sio kanisa Lina la mavazi na maturubai Lina waumini 6 tu huku kwetu

4 Pesa ya kiingilio
Kiingilio au pesa ya kutuma maombi ni takbani million 5 hadi 6, ambayo haitarudishwa kama vigezo vingine havitatimizwa

5 Kuratibu mapato
Serikali itataka kujua mapata ya kanisa na kuyalipia Kodi
Haiwezekani makanisa yakamue Raia masikini wa nchi hiyo huku mchungaji akinunua chopa na magari ya kifahari huku waumini wakitelea yebo

6 Eneo la kujenga kanisa
Serikali ya Rwanda itajiridhisha kuwa kanisa halipo karibu na makazi ya watu, sio kanisa lipo katikati ya makazi ya watu, mikesha kila siku na watu hawalali

Rais Kagame ameonyesha hekima kuu ya utapeli unaojipenyeza katika Imani,
Mwaka Jana maelfu ya watu walikufa huko Kenya msitini Kwa kufuata mafundisho ya uongo

Hapa kwetu makanisa hayalipi Kodi japo wanaingiza mapato makubwa, mizigo bandarini hailpi

Natumai serikali yetu itajipa muda kuinga mfano wa Rwanda
 
Hii nchi ina uhuru wa kuabudu ili mradi huvunji sheria...
Acha kila mtu atafute ugali kwa jinsi anavyoona maana hakuna mchungaji au sheikh aliyekuja kuomba ugali nyumbani kwako.
 
Nampongeza Serikali ya Rwanda kuona mbali na kuweka utaratibu mzuri wa makanisa, Misikiti na taasisi za dini

Rwanda imefungia zaidi ya makanisa 600,

Kabla walipiga marufuku matumizi ya azana Kwa Misikiti kuwa unaleta usumbufu Kwa wasio kuwa wa Imani hiyo na kuweka ustaarabu wa kuitana Kwa alarm

Sio alfajiri unapiga ukunga na watu wamepumzika

Taratibu za kufungua kanisa Rwanda

1. Elimu
Lazima mwanzilishi wa Kanisa na wachungaji waandamizi wawe na degree ya teolojia.

Sio kuamka na darasa la 7 yako eti Mungu amekuita uwe nabii na ufungue kanisa
Mwishowe unaanza mahubiri ya Zumaridi, kuuza mafuta na chumvi ya upako au kuamuru waumini kufunga hadi kufa

2. Miundo wa uongozi
Kanisa linatakiwa liwe na mfumo wa uongozi yani liwe taasisi sio mali ya mtu binafsi.
Kwa Hapa nawapongeza wenzetu waislam, hakuna Misikiti unaomilikiwa na shehe Fulani

3 Kodi
Kanisa lililosajiriwa linatakiwa lilipe Kodi ya dollar 1000 sawa na million karibu 3 Tshs
Na mapato ya kanisa ikiwemo sadaka yatakaguliwa na Serikali na kulipia Kodi

4 Eneo la kujenga kanisa
Serikali ya Rwanda itajiridhisha kuwa kanisa halipo karibu na makazi ya watu, sio kanisa lipo katikati ya makazi ya watu, mikesha kila siku na watu hawalali

Rais Kagame ameonyesha hekima kuu ya utapeli unaojipenyeza katika Imani,
Mwaka Jana maelfu ya watu walikufa huko Kenya msitini Kwa kufuata mafundisho ya uongo

Hapa kwetu makanisa hayalipi Kodi japo wanaingiza mapato makubwa, mizigo bandarini hailpi

Natumai serikali yetu itajipa muda kuinga mfano wa Rwanda
Namba 3: 1000 ni idai ya waumini wanaokukubali kama unaweza kuwaongoza wilaya nzima. Unaweza kidhi vigezo, hao watu usipowapata, ndo imeisha hivo.

Kuhusu pesa, kuna pesa ya kama kiingilio, ambayo ni karibu milioni 4 na nusu au 5 ya Kitanzania, ambayo hairudishwi.
 
Viongozi wakasome au unataka ya Shakohola Kwa mchungaji Mackenzie
Viongozi wakisoma haitasaidia. Ila wafuasi wao wakisoma ndio wataweza kutofautisha mbivu na mbichi, na watachukua hatua ambapo hao viongozi na utapeli wao watakufa kifo cha mende. Na tatizo litakuwa limetatuta.

Wakienda kusoma na kupigwa pini;mtaa utaongeza jobless.
 
Namba 3: 1000 ni idai ya waumini wanaokukubali kama unaweza kuwaongoza wilaya nzima. Unaweza kidhi vigezo, hao watu usipowapata, ndo imeisha hivo.

Kuhusu pesa, kuna pesa ya kama kiingilio, ambayo ni karibu milioni 4 na nusu au 5 ya Kitanzania, ambayo hairudishwi.
Asante Kwa masahihisho
 
a) a certificate issued by the District or the City of Kigali, confirming that the building designated for worship activities adheres to the legal construction requirements applicable to the specified location;


(b) a document confirming the exclusive use of building for worship activities;


(c) a document confirming the conduct of all religious rituals, ceremonies and practices exclusively within the building of the organization designated for worship activities;

(d) documents of the legal representative of the organization and his or her deputy required by laws. If such documents were issued abroad, they are channelled through the Rwandan Embassy located in the country of issuance and authenticated by the Ministry in charge of foreign affairs in Rwanda to ensure their validity;

(e) a proof of payment of a non-refundable service fee of FRW 2,000,000 as a requisite for the legal personality application, paid to the national treasury;

(f) notarized declaration of exclusive representation of the legal representative and his or her deputy certifying that they do not serve as representatives of any other organization registered in Rwanda;

(g) an equivalence certificate of a certificate or degree in theology obtained by the Legal Representative and his or her deputy from foreign higher learning institutions, issued by the competent authority;

(h) an evidence of religious studies completion demonstrating that the legal representative and his or her deputy, whose qualifications are unrelated to theology, have completed at least 1,200 hours of religious studies from an institution accredited by the competent authority.
 
a) a certificate issued by the District or the City of Kigali, confirming that the building designated for worship activities adheres to the legal construction requirements applicable to the specified location;


(b) a document confirming the exclusive use of building for worship activities;


(c) a document confirming the conduct of all religious rituals, ceremonies and practices exclusively within the building of the organization designated for worship activities;

(d) documents of the legal representative of the organization and his or her deputy required by laws. If such documents were issued abroad, they are channelled through the Rwandan Embassy located in the country of issuance and authenticated by the Ministry in charge of foreign affairs in Rwanda to ensure their validity;

(e) a proof of payment of a non-refundable service fee of FRW 2,000,000 as a requisite for the legal personality application, paid to the national treasury;

(f) notarized declaration of exclusive representation of the legal representative and his or her deputy certifying that they do not serve as representatives of any other organization registered in Rwanda;

(g) an equivalence certificate of a certificate or degree in theology obtained by the Legal Representative and his or her deputy from foreign higher learning institutions, issued by the competent authority;

(h) an evidence of religious studies completion demonstrating that the legal representative and his or her deputy, whose qualifications are unrelated to theology, have completed at least 1,200 hours of religious studies from an institution accredited by the competent authority.
Asante sana mkuu
 
Viongozi wakisoma haitasaidia. Ila wafuasi wao wakisoma ndio wataweza kutofautisha mbivu na mbichi, na watachukua hatua ambapo hao viongozi na utapeli wao watakufa kifo cha mende. Na tatizo litakuwa limetatuta.

Wakienda kusoma na kupigwa pini;mtaa utaongeza jobless.
Wachungaji wasome ili wasitoe mafundisho ya ulaghai
 
Hii nchi ina uhuru wa kuabudu ili mradi huvunji sheria...
Acha kila mtu atafute ugali kwa jinsi anavyoona maana hakuna mchungaji au sheikh aliyekuja kuomba ugali nyumbani kwako.
Eeh,maajabu shetani sio ufurahie hilo jambo! Unataka watu waendelee kuabudu tena? Bwana ibilisi imekuaje!
 
Eeh,maajabu shetani sio ufurahie hilo jambo! Unataka watu waendelee kuabudu tena? Bwana ibilisi imekuaje!
Mtu anayesali/swali kwa imani na kweli hawezi kutanga tanga kwenye kila nyumba ya ibada kutafuta miujiza.
Shida sio kuabudu ila ni imani ya kweli kwa kile unachokiabudu.
 
sina ushirika wa mambo ya rohoni na watu wasioamini uwepo wa MWENYE ENZI MUNGU so kaa kando na hayo si sehemu ya mjadala huu. tafuta wenzio mjadili utokuwepo wa MUNGU.
Labda huenda ukawa umepotea njia. Hapa kinajadiliwa nini! Alieleta mada, kuna Mungu umeona humo?
 
Back
Top Bottom