Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 299,512
- 751,975
Ni mwezi wa royal tour (jina haliakisi Utanzania)
Bado tuna safari ndefu kujinasua kwenye makucha ya mabeberu, lakini hili si hoja yangu kwa leo.
Wabongo tuna tatizo sugu na lazima tuliseme hapa wazi na hili ni tatizo mpaka kwenye mamlaka zetu Rasilimali watu hatuipi kipeumbele hata siku moja mbinu za kibiashara na huduma bora nalo ni tatizo kubwa sana.
Tunaamini katika majengo na vitu vya kuonekana kwa macho.
Tunaamini katika kununua madege mengi kisha tunaishia hapo mengine yataji sort yenyewe
Tunaamini katika takwimu za kujenga madarasa mengi bila kusema chochote kwa walimu na vifaa vya kufundishia
Tunaamini katika takwimu za kujenga vituo vya afya vingi lakini bila watalam wa kuvisimamia na vifaa tiba..
Hili tatizo naona nalo linajitokeza kwenye royal tour. Wachambuzi kila kona wanaongea siasa na vitu vya kufikirika. Wanaongea kuhusu watalii milioni 2.5 warakaokuja kwa sababu tu wameona filamu ya Royal Tour.
Sijaona hata mmoja akizungumzia sasa maandalizi muhimu ya kuwapokea kuwahudumia tangu wanapoingia mpaka wanapoondoka ili yasitokee mashetani yakaharibu nia njema.
Hawazungumzii hotel nzuri na za bei stahimilivu
Hawazungumzii changamoto na uswahili wa airport zetu
Hawazungumzii ubabaishaji kwenye huduma mbali mbali kuanzia usafiri wa ndani wawapo nchini, usafiri wa ndege zetu, huduma za vyakula, vinywaji na malazi
Hawazungumzii tatizo la rushwa kwenye mamlaka zetu na hata watu wa kawaida
Hawazungumzii customer care ya viwango vya wageni nknk
Kinachoendelea mitandaoni ni majisifu, kusifiasifia tu na siasa nyingi as if hiyo filamu itafanya yote hayo in automation mode. Maandalizi yasipokuwa mazuri watalii watakaokuja mwaka huu baada ya kuona filamu ya royal tour Wa naweza kuwa wa mwisho.
Tusiwaige hawa wafanyabiashara wetu wanajenga bar nzuri, ama hotel nzuri ama sehemu ya vyakula nzuri kabisa. Lakini anakuja kuajiri cheap labour isiyofahamu chochote kuhusu customer care. Yaani badala ya kumuona mteja ni mfalme yeye ndio anataka kuonwa ni malkia
Kuna vita ya kibiashara hapo hasa na majirani zetu. Je, tumejipangaje kwa hilo? Lazima kuna wachafuzi watataka kuharibu.. Je tuna maandalizi yoyote? Tuache siasa tufanye kazi
La mwisho ni hili la tetesi zisizothibitishwa kwamba mfadhili wa royal tour hawekwi wazi. Ni kwanini inakuwa hivyo? Maana kila kiongozi anaongea lake. Tusianze kuharibu mapema. Hii ikiingia kwenye hisia za kashfa. Tutaharibu mengi. Tutaharibu mapema
Viva tour du royale!
Bado tuna safari ndefu kujinasua kwenye makucha ya mabeberu, lakini hili si hoja yangu kwa leo.
Wabongo tuna tatizo sugu na lazima tuliseme hapa wazi na hili ni tatizo mpaka kwenye mamlaka zetu Rasilimali watu hatuipi kipeumbele hata siku moja mbinu za kibiashara na huduma bora nalo ni tatizo kubwa sana.
Tunaamini katika majengo na vitu vya kuonekana kwa macho.
Tunaamini katika kununua madege mengi kisha tunaishia hapo mengine yataji sort yenyewe
Tunaamini katika takwimu za kujenga madarasa mengi bila kusema chochote kwa walimu na vifaa vya kufundishia
Tunaamini katika takwimu za kujenga vituo vya afya vingi lakini bila watalam wa kuvisimamia na vifaa tiba..
Hili tatizo naona nalo linajitokeza kwenye royal tour. Wachambuzi kila kona wanaongea siasa na vitu vya kufikirika. Wanaongea kuhusu watalii milioni 2.5 warakaokuja kwa sababu tu wameona filamu ya Royal Tour.
Sijaona hata mmoja akizungumzia sasa maandalizi muhimu ya kuwapokea kuwahudumia tangu wanapoingia mpaka wanapoondoka ili yasitokee mashetani yakaharibu nia njema.
Hawazungumzii hotel nzuri na za bei stahimilivu
Hawazungumzii changamoto na uswahili wa airport zetu
Hawazungumzii ubabaishaji kwenye huduma mbali mbali kuanzia usafiri wa ndani wawapo nchini, usafiri wa ndege zetu, huduma za vyakula, vinywaji na malazi
Hawazungumzii tatizo la rushwa kwenye mamlaka zetu na hata watu wa kawaida
Hawazungumzii customer care ya viwango vya wageni nknk
Kinachoendelea mitandaoni ni majisifu, kusifiasifia tu na siasa nyingi as if hiyo filamu itafanya yote hayo in automation mode. Maandalizi yasipokuwa mazuri watalii watakaokuja mwaka huu baada ya kuona filamu ya royal tour Wa naweza kuwa wa mwisho.
Tusiwaige hawa wafanyabiashara wetu wanajenga bar nzuri, ama hotel nzuri ama sehemu ya vyakula nzuri kabisa. Lakini anakuja kuajiri cheap labour isiyofahamu chochote kuhusu customer care. Yaani badala ya kumuona mteja ni mfalme yeye ndio anataka kuonwa ni malkia
Kuna vita ya kibiashara hapo hasa na majirani zetu. Je, tumejipangaje kwa hilo? Lazima kuna wachafuzi watataka kuharibu.. Je tuna maandalizi yoyote? Tuache siasa tufanye kazi
La mwisho ni hili la tetesi zisizothibitishwa kwamba mfadhili wa royal tour hawekwi wazi. Ni kwanini inakuwa hivyo? Maana kila kiongozi anaongea lake. Tusianze kuharibu mapema. Hii ikiingia kwenye hisia za kashfa. Tutaharibu mengi. Tutaharibu mapema
Viva tour du royale!