Labani og
JF-Expert Member
- Sep 15, 2020
- 17,511
- 26,823
YANGA ITATISHA SANA MSIMU UJAO KAMA ITAMSAJILI CHAMA - ROBERTINHO
Kocha wa zamani wa Simba, Robero Oliveira 'Robertinho' licha ya kushituka kusikia uwezekano wa Chama kwenda Yanga amesema endapo hilo litatimia linaweza kuleta shida kubwa kwa timu pinzani kwani kikosi Cha Mabingwa hao kitaongeza ugumu katika safu yao ya ushambuliaji.
"Muda unavyosogea Chama anazidi kwenda mwisho lakini haina maana kuwa hataweza kuisaidia Yanga. Tatizo ninaloliona hapa ni kwamba mchezaji bora anakwenda kuungana na wengine bora hili litakuwa tatizo kwa timu pinzani", amesema Robertinho.
"Nadhani unakumbuka safu yao ya kiungo ilivyokuwa bora msimu uliomalizika, walikuws na watu wabunifu sana eneo hilo kama yule Pacome, Aziz KI na Maxi Nzengeli, anapokeenda na Chama itakuwa ngumu zaidi itategemea na hesabu za kocha wao", amesema Robertinho.
Kumekuwa na taarifa kuwa Chama amesaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia klabu ya Yanga na kinachosubiriwa ni kumtangaza tu.
Je: Makolo hauogopi .......yajayo yanatisha
Kocha wa zamani wa Simba, Robero Oliveira 'Robertinho' licha ya kushituka kusikia uwezekano wa Chama kwenda Yanga amesema endapo hilo litatimia linaweza kuleta shida kubwa kwa timu pinzani kwani kikosi Cha Mabingwa hao kitaongeza ugumu katika safu yao ya ushambuliaji.
"Muda unavyosogea Chama anazidi kwenda mwisho lakini haina maana kuwa hataweza kuisaidia Yanga. Tatizo ninaloliona hapa ni kwamba mchezaji bora anakwenda kuungana na wengine bora hili litakuwa tatizo kwa timu pinzani", amesema Robertinho.
"Nadhani unakumbuka safu yao ya kiungo ilivyokuwa bora msimu uliomalizika, walikuws na watu wabunifu sana eneo hilo kama yule Pacome, Aziz KI na Maxi Nzengeli, anapokeenda na Chama itakuwa ngumu zaidi itategemea na hesabu za kocha wao", amesema Robertinho.
Kumekuwa na taarifa kuwa Chama amesaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia klabu ya Yanga na kinachosubiriwa ni kumtangaza tu.
Je: Makolo hauogopi .......yajayo yanatisha