Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,516
- 3,806
Ripoti ya mwaka 2018 iliyotolewa na Benki ya Dunia inaonyesha kila Mwanamke duniani hadi mwaka 2016 anajifungua wastani wa chini ya watoto 2.5
Idadi hiyo ni kama nusu ya ilivyokuwa katikati ya miaka ya 1960 ambapo Mwanamke mmoja alikuwa anajifungua watoto watano
Kiwango cha uzazi kinawakilisha idadi ya watoto ambao watazaliwa na Mwanamke ikiwa ataishi hadi mwisho wa miaka yake ya kuweza kubeba mimba na kuzaa watoto kwa mujibu wa viwango vya uzazi wa mwaka maalum
Katika mataifa yaliyoendelea kiviwanda, ripoti hiyo imeonyesha Mwanamke anazaa watoto wachache kuliko inavyotakiwa duniani huku katika mataifa maskini matokeo ni kinyume
Aidha, katika mataifa 43 wanawake wanakozaa angalau watoto wanne, mataifa 38 ni ya Afrika na kubainishwa kuwa idadi hiyo kubwa ya uzazi inatokana na ukosefu wa elimu na kinga wakati wa ngono
Kwa nchi ya Tanzania ripoti hiyo inaonesha kuwa wastani wa mwanamke mmoja kuzaa katika miaka ya 1960 ilikuwa ni watoto 6.8 ila kwa mwaka 2016 ni watoto watano
Idadi hiyo ni kama nusu ya ilivyokuwa katikati ya miaka ya 1960 ambapo Mwanamke mmoja alikuwa anajifungua watoto watano
Kiwango cha uzazi kinawakilisha idadi ya watoto ambao watazaliwa na Mwanamke ikiwa ataishi hadi mwisho wa miaka yake ya kuweza kubeba mimba na kuzaa watoto kwa mujibu wa viwango vya uzazi wa mwaka maalum
Katika mataifa yaliyoendelea kiviwanda, ripoti hiyo imeonyesha Mwanamke anazaa watoto wachache kuliko inavyotakiwa duniani huku katika mataifa maskini matokeo ni kinyume
Aidha, katika mataifa 43 wanawake wanakozaa angalau watoto wanne, mataifa 38 ni ya Afrika na kubainishwa kuwa idadi hiyo kubwa ya uzazi inatokana na ukosefu wa elimu na kinga wakati wa ngono
Kwa nchi ya Tanzania ripoti hiyo inaonesha kuwa wastani wa mwanamke mmoja kuzaa katika miaka ya 1960 ilikuwa ni watoto 6.8 ila kwa mwaka 2016 ni watoto watano