"MsemajiUkweli, post: 19149542, member: 91662"]
Waeneza propaganda hawakutaka kutuambia kama Rais Kikwete ameziacha taasisi zifanye kazi zake kwa sababu kama wangesema hivyo basi hata hoja yao ya kusema Rais ni dhaifu ingekuwa haina nguvu.
Kauli hii tu inaonyesha unavyozungumzia propaganda badala ya uhalisia
Tanzania hakuna taasisi iliyo huru inayoweza kufanya kazi bila kuingiliwa na Serikali
Takukuru wanaripoti kwa Rais
Polisi wanaripoti kwa Rais
Majuzi tumeambiwa hata mihimili ya sheria na bunge ule wa serikali ''umezama'' zaidi
Hivyo hakukuwa na suala la Kikwete kuchia taasisi zifanye kazi
Richmond ilifichwa na PCCB kwa mara ya kwanza.
Hata ilipoabinika walipika taarifa hakuna aliyechukuliwa hatua.
Majadala ya kesi yalikuwa kwa DPP na DCI wakilumbana.
Hakuna aliyechukua hatua na kesi zikaisha hivyo hivyo
Kila siku tume ziliundwa ukiwa ni ushahidi kuwa hata serikali haikuamini vyombo vyake
Na hata ilipotumia vyombo hivyo, ilikuwa kuzuga tu na kuondoa watu barabarani
Hivi tume ya IGP, PCCB na Mwanasheria mkuu kuhusu EPA ilitoa taarifa gani?
Siku hizi haki ni kwa maelekezo kwa msemo wa maelekezo kutoka juu
Hivyo hoja kwamba kuna taasisi huru Tanzania haipo na hilo linaifanya mada nzima kuwa mfu, potofu na propaganda tu
Kuendelea kujadili ni kukubaliana na upotoshaji huu usio na maana kwa Taifa