Prof. Janabi: Kula mlo mmoja hurefusha maisha

The Watchman

JF-Expert Member
Nov 7, 2023
693
1,165
“Wale watu wanaokula mara nyingi, wanaokula mara kwa mara wanakuwa hawana muda wa kuunguza mafuta. Wanaofunga muda mrefu wanakuwa na muda mrefu pia wa kuunguza mafuta ya Mwili. Kuna magonjwa mengi yanayosababishwa na ulaji wetu wa mara kwa mara. Ukitaka kinga ya mwili iwe juu na kurefusha maisha, si kurefusha tu maisha bali maisha yenye quality (Ubora), kula mlo mmoja. Ni ngumu kuvumilia lakini mwili siku zote una tabia ya kuzoea. Si lazima ule mlo mmoja kila siku, unaweza kubadili ukala mara mbili au tatu kwa wiki, siku zingine ukala mara mbili”

Nukuu ya Pro. Mohamed Janabi, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili na Mshauri wa Rais kuhusu Masuala ya Afya akizungumza kupitia Afya Podcast ya Muhimbili TV, Septemba 4, 2023
 
Kila kitu kwa kiasi wandugu. Kuleni kwa kiasi. Nilijaaliwa kumuona Janabi kwa karibu sana, ukweli ni kwamba yuko weak, sikuona nuru kwenye ngozi yake... SIMSIMANGI ila anahitaji kuongeza mlo kidogo. Siku hiyo alishindia kikombe cha kahawa nyeusi bila sukari. nilikuwa namwangalia sana... nilimhurumia. Hatuishi milele hapa... tule tufurahi kwa KIASI
 
Kila kitu kwa kiasi wandugu. Kuleni kwa kiasi. Nilijaaliwa kumuona Janabi kwa karibu sana, ukweli ni kwamba yuko weak, sikuona nuru kwenye ngozi yake... SIMSIMANGI ila anahitaji kuongeza mlo kidogo. Siku hiyo alishindia kikombe cha kahawa nyeusi bila sukari. nilikuwa namwangalia sana... nilimhurumia. Hatuishi milele hapa... tule tufurahi kwa KIASI
:D :D :D haha kwamba aongeze mlo, ukamhurumua hahaha kunenepa sio afya
 
“Wale watu wanaokula mara nyingi, wanaokula mara kwa mara wanakuwa hawana muda wa kuunguza mafuta. Wanaofunga muda mrefu wanakuwa na muda mrefu pia wa kuunguza mafuta ya Mwili. Kuna magonjwa mengi yanayosababishwa na ulaji wetu wa mara kwa mara. Ukitaka kinga ya mwili iwe juu na kurefusha maisha, si kurefusha tu maisha bali maisha yenye quality (Ubora), kula mlo mmoja. Ni ngumu kuvumilia lakini mwili siku zote una tabia ya kuzoea. Si lazima ule mlo mmoja kila siku, unaweza kubadili ukala mara mbili au tatu kwa wiki, siku zingine ukala mara mbili”

Nukuu ya Pro. Mohamed Janabi, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili na Mshauri wa Rais kuhusu Masuala ya Afya akizungumza kupitia Afya Podcast ya Muhimbili TV, Septemba 4, 2023
Siku hizi tangu ametumwa kwenda ukurugenzi wa WHO aakula hadi keki kwenye birtdays anazoalikwa, hadi Pepsi baridi anakunywa ili aonekane ni mtu wa watu
 
Kwanini mada za prof. Janabi huwa mnazileta kimzaha?
pengine kama hamuelewi anazungumzia nini ulizeni?

Kwa kifupi "njaa" ni mazoea Tu, shibe inaua mwili kuliko hata "ukimwi" ndio maana wafungwa wa kibongo wanakula mlo mmoja na wananenepa!

Alichosema Janabi kinaitwa "INTERMITTED FASTING" nenda Google utaelewa.

Najuta kuchelewa kujua Jambo hili....nimekuwa napambana na uzito uliokithiri ila kwa Kula 18:6 najiuliza kitambi kimepotelea wapi? 18:6 maana yake nafunga masala 18 na kuwa na muda WA Kula CHOCHOTE ndani ya masaa 8 kwa siku moja 24hrs.

Hii mbinu ni ya kale Sana madaktari kabla ya kuvurugwa na pharm companies walikuwa wakitumia njia hii kutibu wagonjwa wa sukari, shinikizo la damu, kansa NK.

Wengi tunakula Tu kwasababu ya mazoea ya Kula ila mwili hauhitaji hiyo Milo yako mitatu na pepsi ili kupunguza kuvimbiwa, ....

Soma, soma,soma vuka upeo wa kufikiri a tuliowekewa na CCM! Sorry , SYSTEM!
 
Back
Top Bottom