LGE2024 Polisi: Kuna chama cha Siasa kinapanga kufanya Vurugu katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Mtoa Taarifa

JF-Expert Member
Sep 21, 2024
213
667
Screenshot_2024-11-08-20-59-47-605_com.instagram.android-edit.jpg

TAARIFA KWA UMMA

Baada ya uteuzi wa Wagombea wa nafasi za Uongozi katika nafasi mbalimbali za Serikali za Mitaa, kuna Chama cha Siasa kimepanga na kinahamasisha wafuasi wao kwa njia mbalimbali ikiwepo kukutana, kupigiana simu, kutumiana ujumbe na kwa kutumia makundi sogozi, kudhuru watu na kuharibu Ofisi za Serikali.

Jeshi la Polisi linaendelea kuwafuatilia kwa karibu ili wakamatwe na hatua nyingine za kisheria zifuate.

Kupata matukio mengine ya kiusalama wakati wa uchaguzi bofya: LIVE - Uzi Maalum wa Matukio ya Kiusalama kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Jeshi la Polisi linatoa wito kwa Viongozi wa Vyama vya Siasa na Wafuasi wao kama wanaona kuna kasoro katika mchakato wa uteuzi wa wagombea wao, wafuate sheria na kanuni zinavyoelekeza na si kupanga na kuhamasishana kufanya uhalifu.

Aidha, linatoa onyo kali kwa yeyote anayepanga na kuhamasisha uhalifu wa aina hiyo kuacha mara moja.

Vinginevyo hatupo tayari kumvumilia mtu, kikundi cha watu au chama chochote cha Siasa kinachopanga uhalifu wowote ili kutaka kuvuruga amani ya nchi, kwani hatuta muonea muhali tutamchukulia hatua kali kwa mujibu wa sheria za nchi.

Tuna wahakikishia wananchi kuwa, Jeshi la Polisi limejiimarisha vizuri kuhakikisha kuwa wanafanya shughuli zao za kujiletea maendeleo na kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika mazingira yenye amani, utulivu na usalama hivyo wasiwe na hofu ya aina yeyote.

Imetolewa na:
David A. Misime - DCP Msemaji wa Jeshi la Polisi Dodoma, Tanzania.
 
Chadema hao ,Wana option mbili tu kushiriki au kutoshiriki,waache upuuzi ,wasiposhiriki wao act,chauma,ADC nk vitashiriki
 
Ndugu zangu Watanzania,

Hiii ndio taarifa ya jeshi la Polisi Nchini.ikitoa onyo kali kwelikweli kwa chama cha siasa ambacho baada ya wagombea wake kukatwa katika hatua za uteuzi kinapanga kuwahamasisha wafuasi na wanachama wake kufanya vurugu, kuharibu ofisi za serikali na uharibifu mwingine mbalimbali.

Ambapo jeshi hilo la Polisi Nchini Limetaka chama ambacho hakijaridhishwa na mchakato wa uteuzi kifuate sheria,kanuni,taratibu na miongozi mbalimbali kama inavyoelekezwa na sheria za uchaguzi wa serikali za mitaa.

Jeshi hilo ambalo linatajwa kuwa jeshi bora katika ukanda huu wa Afrika mashariki na kusini mwa jangwa la Sahara.limesema kuwa halitasita kuchukua hatua kali sana kwa yeyote yule atakaye kiuka taratibu na sheria kwa kufanya vurugu
Screenshot_20241108-211203_1.jpg


Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
 
Yule DC aliekiri kuwa wanafanya uharamia maporini aliishia tu kufukuzwa ukuu wa wilaya ila Polisi sijui hata kama waliwahi kumuita na kumuhoji.

Better were colonial days.
 
Back
Top Bottom