Pasu kwa Pasu: Shilingi bilioni 318 za Pep Guardiola kugawanywa baada ya mke kudai talaka, Mke ataja sababu ni Pep kuwa busy sana

wastani kwa idadi

JF-Expert Member
Jun 28, 2024
503
1,421
1737573233321.png


Ukose Hela akukatae haupo bize, utafute ela akukatae uko bize

Kocha mkuu wa Manchester City ya Uingereza Pep Guardiola ameachana rasmi na mke wake Cristina Serra baada ya kudumu kwenye ndoa miaka 30. Katika talaka waliyopeana mahakamani mke huyo wa Guardiola atatwaa nusu ya utajiri wa Guardiola na jumba lake kubwa la kifahari lililopo jijini Manchester nchini Uingereza.

Vyanzo vimetathmini utajiri wa Pep kuwa dola za kimarekani milioni 126 sawa na shilingi bilioni 318

Sababu kuu ya mke huyo kuomba talaka ni yeye kudai Guardiola yupo bize na kazi.

Guardiola na mke wake katika miaka 30 ya ndoa wamefanikiwa kupata watoto watatu Marius, Maria na Valentina

Inadaiwa mgao huo umempa stress zinazochangia timu anayoifundisha Manchester City kufanya vibaya msimu huu.
 
Back
Top Bottom