Nipeni ushauri kuhusu printer

Digital Ticha

Member
Jun 16, 2023
58
94
Natafuta printer kwa ajili ya ofisi yangu ni ofisi ndogo inajitafuta lakini uwa tuna kazi za kuprint na kutoa copy kwa wastani wa karatasi 2000 za black and white na 100 za coloured kwa mwezi.

Kuna mtu kanipa pendekezo la printer ya: HP LaserJet Pro MFPM 426 FDW anaiuza kwa laki 7 ila changamoto yake haitoi kazi za coloured.

Naomba mwenye pendekezo la printer ya HP dizain kama hii HP ila inatoa pia copy za rangi anisaidie details.

Au kama itabidi niwe na printer mbili yani nitafute ndogo maalum kwa kazi za rangi tu nitapata printer ipi ndogo lakini nzuri na affordable yani nipate details zake mimi nipo blind kidogo kuhusu printers ila nilipewa somo kidogo kuhusu wino kuna zinazotumia wino expensive na za cheap hiyo HP nilipenda kwa kuwa inafanya karibu kila kitu yani printing, photocopy na scanning na wino wake niliambiwa unanunua kwa elfu 30 changamoto ni haitoi coloured.

Au kama kuna printer nzuri inayofanya kazi multi-purpose kama HP LaserJet Pro MFPM 426 FDW na ni bora zaidi na affordable naombeni ushauri wenu niufanyie kazi

Karibuni!
 
Kuna aina mbili kuu za printer,
Inkjet zinazotumia "wino" na Laser zinazotumia toner hiyo yako ni ya Laser.

Wino ni gharama sana kufananisha na toner kwa gharama ya kurasa moja hasa kama utajaribu kutumia original. Ningesema inkjet haifai ofisini unless una mahitaji maalumu. Ni nafuu sana printer yeneyewe ila wanakukamata kwenye wino.

Inkjet ndo inatoa photo quality prints kama unahitaji picha za color ambazo zinafanana na picha za kweli itabidi utumie inkjet.

Laser za color zipo ila itabidi uwe unanunua toner 4, unaweza kuprint picha ambazo sio mbaya ila haitakuwa photo quality graphics za kiosifi charts/graphs zinatoka vizuri zaidi.

Watengenezaji wa printer wanaweka ujinga ujinga mwingi siku hizi kwa mfano kulazimisha ununue original ink/toner na kuzuia kuprint kama rangi moja ikiisha so inaisha yellow printer inakataa kuprint b/w mpaka uweke yellow mpya, zengine zinalazimisha online subscription so inabidi uchunguze kidogo.

Printer karibia zote za ofisi zina hiyo copy/scan siku hizi. Tafuta ya Brother quality nzuri na hawana ujinga mwingi ila angalia pia upatikanaji wa wino/toner kwa hapo ulipo hasa za 3rd party original ni pigo.
 
hapo kwenye copy 2000 nakushauri nunua photocopy machine tu ili upate faida nzuri, toner za hp ni ndogo alafu gharama kama unataka kutoa copy ni harara ukilinganisha na kuwa na photocopy machine ambayo ina toner kubwa na gharama nafuu black & white, unaweza kununua canon photocopy machine mpya kabisa kwa kuanzia ambayo haizidi 2M lkn itaokoa pesa nyingi na baadae kazi zikiomgezeka unatafuta heavy duty photoxopy machine. Pia unaweza nunua used ila tafuta fundi photocopy mzuri akague kabla hujanunua na nunua mitumba ya kutoka nje ina afadhali kidogo.

Hapo kwenye color sasa unanunua epson zipo nzuri zinakuwa na tank nne za wino zinatoa copy vizuri pia utatumi kwa colour printing.

KUmbuka hata photocopy pia unaweza tumia kama printer.
 
Natafuta printer kwa ajili ya ofisi yangu ni ofisi ndogo inajitafuta lakini uwa tuna kazi za kuprint na kutoa copy kwa wastani wa karatasi 2000 za black and white na 100 za coloured kwa mwezi.

Kuna mtu kanipa pendekezo la printer ya: HP LaserJet Pro MFPM 426 FDW anaiuza kwa laki 7 ila changamoto yake haitoi kazi za coloured.

Naomba mwenye pendekezo la printer ya HP dizain kama hii HP ila inatoa pia copy za rangi anisaidie details.

Au kama itabidi niwe na printer mbili yani nitafute ndogo maalum kwa kazi za rangi tu nitapata printer ipi ndogo lakini nzuri na affordable yani nipate details zake mimi nipo blind kidogo kuhusu printers ila nilipewa somo kidogo kuhusu wino kuna zinazotumia wino expensive na za cheap hiyo HP nilipenda kwa kuwa inafanya karibu kila kitu yani printing, photocopy na scanning na wino wake niliambiwa unanunua kwa elfu 30 changamoto ni haitoi coloured.

Au kama kuna printer nzuri inayofanya kazi multi-purpose kama HP LaserJet Pro MFPM 426 FDW na ni bora zaidi na affordable naombeni ushauri wenu niufanyie kazi

Karibuni!
Hp printer coloured achana nazo.kabisa, hapa nina printer hp colured inatumia toner 4, bei tu ya huo wino ni tsh 400,000-500,000, halafu unawahi kuisha mmoja hasa yellow, halaf huwezi kununua mmoja mmoja au ku refil kama epson, kanunu epson mkuu kwa coulor printing
 
hapo kwenye copy 2000 nakushauri nunua photocopy machine tu ili upate faida nzuri, toner za hp ni ndogo alafu gharama kama unataka kutoa copy ni harara ukilinganisha na kuwa na photocopy machine ambayo ina toner kubwa na gharama nafuu black & white, unaweza kununua canon photocopy machine mpya kabisa kwa kuanzia ambayo haizidi 2M lkn itaokoa pesa nyingi na baadae kazi zikiomgezeka unatafuta heavy duty photoxopy machine. Pia unaweza nunua used ila tafuta fundi photocopy mzuri akague kabla hujanunua na nunua mitumba ya kutoka nje ina afadhali kidogo.

Hapo kwenye color sasa unanunua epson zipo nzuri zinakuwa na tank nne za wino zinatoa copy vizuri pia utatumi kwa colour printing.

KUmbuka hata photocopy pia unaweza tumia kama printer.
Ok nimekusoma, je kuna canon isiyozidi million 1 ambayo inaweza kufanya majukumu yangu vizuri na specifications zake ni zipi nikitaka kuitafuta?
 
Hp printer coloured achana nazo.kabisa, hapa nina printer hp colured inatumia toner 4, bei tu ya huo wino ni tsh 400,000-500,000, halafu unawahi kuisha mmoja hasa yellow, halaf huwezi kununua mmoja mmoja au ku refil kama epson, kanunu epson mkuu kwa coulor printing
Unashaurije, photocopier iwe brand gani na printer iwe brand gani na specifications zake ni zipi na bei?
 
Kuna aina mbili kuu za printer,
Inkjet zinazotumia "wino" na Laser zinazotumia toner hiyo yako ni ya Laser.

Wino ni gharama sana kufananisha na toner kwa gharama ya kurasa moja hasa kama utajaribu kutumia original. Ningesema inkjet haifai ofisini unless una mahitaji maalumu. Ni nafuu sana printer yeneyewe ila wanakukamata kwenye wino.

Inkjet ndo inatoa photo quality prints kama unahitaji picha za color ambazo zinafanana na picha za kweli itabidi utumie inkjet.

Laser za color zipo ila itabidi uwe unanunua toner 4, unaweza kuprint picha ambazo sio mbaya ila haitakuwa photo quality graphics za kiosifi charts/graphs zinatoka vizuri zaidi.

Watengenezaji wa printer wanaweka ujinga ujinga mwingi siku hizi kwa mfano kulazimisha ununue original ink/toner na kuzuia kuprint kama rangi moja ikiisha so inaisha yellow printer inakataa kuprint b/w mpaka uweke yellow mpya, zengine zinalazimisha online subscription so inabidi uchunguze kidogo.

Printer karibia zote za ofisi zina hiyo copy/scan siku hizi. Tafuta ya Brother quality nzuri na hawana ujinga mwingi ila angalia pia upatikanaji wa wino/toner kwa hapo ulipo hasa za 3rd party original ni pigo.
Naomba suggestions zako kwa printer ya kutoa coloured na photocopy machine za bei nzuri
 
Angalia mambo haya muhimu mkuu.

1. Gharama ya wino ya hiyo Printer.
2. Printing Speed ya Printer kama wewe ni mtu wa kutoa copy nyingi au lah.
3. Quality ya printing.

Epson za kurefill wino inakupa unafuu sana kwenye gharama ya wino na itakupa quality nzuri ya kuprint on paper. Epson utakwazika nae sehemu tu ya speed, copy 500 za black and white zinachukua around 1 hour, zikiwa colored hapo hata masaa 2 au 3. Hizi kibiashara huwa hazifai kabisa.

HP anakupa speed with good quality too isipokuwa kwenye wino atakutesa, narudia tena, kwenye wino anaweza akakupasua akili hata ukashawishika kuiweka tu ndani Printa bila kuitumia.

Ushauri, kabla hujanunua Printa ulizia gharama za wino kwanza za hiyo Printa.
 
Angalia mambo haya muhimu mkuu.

1. Gharama ya wino ya hiyo Printer.
2. Printing Speed ya Printer kama wewe ni mtu wa kutoa copy nyingi au lah.
3. Quality ya printing.

Epson za kurefill wino inakupa unafuu sana kwenye gharama ya wino na itakupa quality nzuri ya kuprint on paper. Epson utakwazika nae sehemu tu ya speed, copy 500 za black and white zinachukua around 1 hour, zikiwa colored hapo hata masaa 2 au 3. Hizi kibiashara huwa hazifai kabisa.

HP anakupa speed with good quality too isipokuwa kwenye wino atakutesa, narudia tena, kwenye wino anaweza akakupasua akili hata ukashawishika kuiweka tu ndani Printa bila kuitumia.

Ushauri, kabla hujanunua Printa ulizia gharama za wino kwanza za hiyo Printa.
Sawa mkuu nimekuelewa. Gharama za wino ambazo ni reasonable ni kiasi gani?
 
Sawa mkuu nimekuelewa. Gharama za wino ambazo ni reasonable ni kiasi gani?
Kwa mashine ipi sasa kati ya hizo? Kumbuka hata hizo Epson za kurefill wino wake OG ni elfu 25 mpaka 30 ila upo compatible elfu tano hadi elfu kumi lakini ni vyema zaidi ukachukua compatible wa elfu kumi kwenye maduka ya Posta, ni elfu 10 na sehemu zingine hadi elfu 7 sijui 8 kuliko viwino vya Kkoo.
 
Back
Top Bottom