Ninakabiliwa na changamoto nyingi sana, sijui nifanye nini ili kuboresha hali yangu

mhogoz

JF-Expert Member
Oct 16, 2021
729
1,184
Nimepitia mengi katika maisha. Pamoja na juhudi kubwa za kusoma na kuwa na akili nyingi, bado naishi maisha magumu na yenye kudharaulika.

Nina familia na watoto, lakini nahisi kama mke wangu haniheshimu tena baada ya yeye kujipatia mafanikio. Nahisi muda wowote anaweza kufanya uamuzi mgumu dhidi yangu kwa sababu kauli zake ni ngumu kuelewa. Nahisi kama nilishapoteza mwelekeo siku nyingi zilizopita.

Nimepata hasara nyingi kwenye mambo mengi niliyowekeza. Ingawa nimeajiriwa, nahisi hakuna kitu ninachoweza kufanya ili kuboresha hali yangu. Zaidi ya hayo, madeni niliyonayo yanazidi kunisumbua. Siwezi kufanya jambo lolote la kumuumiza mtu mwingine, lakini mara nyingi nashutumiwa kwa vitu ambavyo sijafanya au sikuhusika navyo.

Kwa kweli, ninakabiliwa na changamoto nyingi sana, na sijui nifanye nini ili kuboresha hali yangu.
 
Nimekutafuta sana kwenye maisha,pamoja na kusoma sana na kuwa na akili nyingi naishi maisha magumu mno Tena ya kudharaulika.nina familia na watoto but nikama wife ananidharau baada ya kujipatia.nina hisi muda wowote anaweza kubipiga tukio kwa maana kauli zake siziekewi elewi.nahisi ya kuwa nilishapoteza dira siku nyingi.kimsingi nimepata hasara kwenye mambo mengi ambayo nimejaribu kuwekeza,nimeajiriwa but nahisi hakuna chochote naweza kufanya plus madeni niliyo nayo .siwezi kufanya jambo lolote la kumuumiza mtu mwingine.huwa nalaumiwa sana kwa vitu ambavyo sijafanya au siku husika nalo ,kimsingi ninachangamoto nyingi mno,sijui nifanyeje jamani.Nilitaka kusoma but nimeshindwa kulipa ada
 
Hata nyakati ngumu hazidumu milele. Mshukuru muumba wako pumzi ipo. Kaza kaza kaza man
 
Pesa...PESA...PESA..PESaaaaa.. only money 💰💰💰💰
 
Tatizo mnadharau wasomi waliosema mahitaji ya binadamu ni
1.chakula
2.mavazi
3. Na makazi yani uwe na sehemu ya kuishi ambapo ndio makazi

Sasa nyie vijana mnajichanganya mara biashara mara gari sijui nini

Ebu tafuta mwajiriwa kama wewe ambaye alianza na mahitaji hayo matatu muhimu kama mke anamzingua


Sikieni nyie Gez-Z fanya yote hakisha una makazi haijalishi ya thamani ipi ila akikisha una pakulala na kuamka na kwenda kwenye mishe haya mengine matokeo,

Ujinga wa binadamu wanamini kila mtu anaweza fanya biasha akafanikiwa nakusahau biashana mafanikio ni kama akili shuleni si kila mtu anazo
 
Back
Top Bottom