Ninahisi nguvu ya sasa ya CHADEMA ni kwa hisani ya CCM, tunahitaji Upinzani halisi

Nehemia Kilave

JF-Expert Member
Jan 9, 2022
1,005
2,198
Tanzania ina Jumla ya vyama vya Siasa 19, ACT Wazalendo kikiwa ni chama mwisho kusajiliwa May 2014.

CUF na NCCR MAGEUZI ya kina Mbatia walijaribu kuwa wapinzani halisi lakini wakadhohofishwa.

CCM ni chama kikubwa na kina mbinu Nyingi sana ninahisi kinaipa nguvu ya kifedha CHADEMA kwa faida yake kisiasa.

Kinatengenezwa kuwa Chama chenye wafuasisi wengi kisicho na madhara hasa kwenye nafasi ya Mgombea wa Urais.

Wanachama wa CHADEMA hapa mtaona umuhimu wa chama kuchangisha pale ruzuku na vyanzo vingine visipotosha.

Kama Upinzani una malengo ya kuchukua dola uangaliwe Upinzani Mpya either vyama vingine viungane au Chama kipya.

Mwisho kabisa 2025 wazalendo na wana harakati hawajalala na kuna kila dalili mpinzani mwenye nguvu anatikisa na kuchukua dola hivyo "HAKIKISHA UNAJIANDIKISHA KATIKA DAFTARI LA WAPIGA KURA" .
 
Back
Top Bottom