nanjanga
JF-Expert Member
- Jan 3, 2014
- 330
- 111
Nimepima leo group la damu yangu, nina group 0+ Rh,
Nini faida ya hili group na hasara zake, na je naweza kumpa damu mtu wa group gani?
Nitashukuru nikisaidiwa mawazo, asante.
Nini faida ya hili group na hasara zake, na je naweza kumpa damu mtu wa group gani?
Nitashukuru nikisaidiwa mawazo, asante.
Kwa faida yetu sote nitaeleza kila group la damu:
Kwanza kuna Magroup 8 ya damu nayo ni: A+, O+, B+, AB+, A-, O-, B-, AB-
(1) GROUP A+
Anauwezo wa kutoa damu kwa mtu mwenye: A+ na AB+
Anauwezo wa kupokea damu kwa mtu mwenye: A+, A-, O+ na O-
(2) GROUP O+
Anauwezo wa kutoa damu kwa mtu mwenye: O+, A+, B+ na AB+
Anauwezo wa kupokea damu kwa mtu mwenye: O+ na O-
(3) GROUP B+
Anauwezo wa kutoa damu kwa mtu mwenye: B+ na AB+
Anauwezo wa kupokea damu kwa mtu mwenye: B+, B-, O+ na O-
(4) GROUP AB+
Anauwezo wa kutoa damu kwa mtu mwenye: AB+ TU
Anauwezo wa kupokea damu kwa mtu mwenye: KWA KUNDI LOLOTE
(5) GROUP A-
Anauwezo wa kutoa damu kwa mtu mwenye: A+, A-, AB+ na AB-
Anauwezo wa kupokea damu kwa mtu mwenye: A- na O-
(6) GROUP O-
Anauwezo wa kutoa damu kwa mtu mwenye: KWA KUNDI LOLOTE
Anauwezo wa kupokea damu kwa mtu mwenye: O- TU
(7) GROUP B-
Anauwezo wa kutoa damu kwa mtu mwenye: B+, B-, AB+ na AB-
Anauwezo wa kupokea damu kwa mtu mwenye: B- na O-
(8) GROUP AB-
Anauwezo wa kutoa damu kwa mtu mwenye: AB+ na AB-
Anauwezo wa kupokea damu kwa mtu mwenye: AB-, A-, B- na O-
Hii ni kwa mujibu ya mitandao ya afya.
Kwa ishu ya RH+ na RH- (RHESUS FACTOR) naona mdau Helcobacter Pylori kalielezea vizuri sana kwa lugha rahisi kueleweka.
NOTE: MITANDAO YA JAMII IKITUMIKA VIZURI NI MSAADA MKUBWA SANA KWA JAMII