DOKEZO NIDA Kinondoni wanahatarisha Faragha ya Wateja wao

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Jiuzi nilienda ofisi ya NIDA Kinondoni huko Kawe. Kisa mtandao wao kukata nilipoenda mara ya kwanza nilipaswa kuacha makaratasi yangu ofisini kwao. Niliporudi kupigwa picha na kuchukuliwa alama za vidole yaani kuingizwa kwenye mfumo, maafisa wote wa chumba cha picha walikuwa bize na shughuli zao. Wakaniambia nipitie fomu zote zilizokaa mezani kwa kutafuta ya kwangu mwenyewe.

Kwa hiyo niliweza kuangalia na kupitia taarifa binafsi za watu kama mia kabla ya kupata fomu yangu. Hapo sikuwa na nia mbaya na sikuangalia sana fomu za watu wengine ila nilishangaa sana. Kumbe hivi ndivyo taarifa zetu zinavyolindwa na NIDA. Mtu anaweza kuingia chumbani kwao akijifanya kama aliacha fomu yake kule jana na ana access rahisi ya taarifa za watu, majina, namba za simu, makazi, nk.

Aidha kirasmi hairuhusiwi kutumia simu ndani ya chumba hicho lakini kanuni hiyo haitelezeki. Wengi waliosubiri kupata huduma kule walitumia simu zao bila kusitishwa. Hii inahatarisha taarifa zetu zaidi.

Hatua zichukuliwe kuhakikisha faragha yetu na ulinzi wa taarifa yetu binafsi. Maafisa hawa waelimishwe kuhusu hatari za vitendo hivi na umuhimu wa kufuatilia itifaki ya kulinda taarifa binafsi.
 
Yaan hapo n mbuzi umempigia kitaa yy ataendelea kula majan tu ,Wala c kusikiliza gitaa lako Linapigajee mkuu.

NIDA kiufupi Kila kitu Chao n sifuri wanakera mpk wanakera tena
 
Vitamvulishwa ndiyo vimetupwa huko kwenye ofisi za watendaji kata/mitaa.

Ila nasisi watz sijui kwa nini hatufuatilii vitambulisho. Unakuta kwa mtendaji kuna vitambulisho vimejaa unajiuliza hawa watu wameshkufa ama wapo hai?

Nida ijitahidi kuwahimiza wananchi waende kuchukua vitambulisho vyao.
 
Kuna watu walisajiliwa 2017, vitambulisho vimetolewa leo ili hali mtu ameshahamia mbali sana, wengine nje ya nchi, wengine wamefsriki.
Katika hali kama hiyo lazima vitambulisho vibaki kwa WEO's
Vitamvulishwa ndiyo vimetupwa huko kwenye ofisi za watendaji kata/mitaa.

Ila nasisi watz sijui kwa nini hatufuatilii vitambulisho. Unakuta kwa mtendaji kuna vitambulisho vimejaa unajiuliza hawa watu wameshkufa ama wapo hai?

Nida ijitahidi kuwahimiza wananchi waende kuchukua vitambulisho vyao.
 
Kwa kawaida utaratibu wa NIDA, mwombaji anapokamioisha hatua za kuthibitisha makazi, Serikali ya Mtaa na Uraia, Uhamiaji hatakiwi kubaki na fomu wala kujitafutia fomu kwa ajili ya kukamilisha hatua yoyote ile ya Usajili.
Kutoruhusu kupiga picha ni moja ya hatua/njia ya kudumisha faragha ya taarifaza watu. Mleta thread naona pamoja na kusoma kakiuka hilo pia.
 
huku kwetu nsiku za nyuma kdg ndg mwandishi, kulikuwa kuna utaratibu wa kubandika mapingamizi inaitwa objection, huwa zinabandikwa kila mtu aone, kama kuna shida kwa mhusika mtu yeyote anatoa taarifa au kama kuna taarifa imekosewa basi unapewa muda kupitia karatasi hizo ndani ya siku kadhaa, kabla hazijafanyiwa kazi, kingine punguza ujuaji au umbea
 
Back
Top Bottom