Ni tamaa au? Ndani ya mwaka baada ya kifo cha mzazi wanafamilia wanakuja julishwa na mwenyekiti kuna mwanafamilia kakopea milioni 30 nyumba ya urithi

wastani kwa idadi

JF-Expert Member
Jun 28, 2024
249
682
To cut the story short watoto tupo sita rika ni 30 hadi 40, wengi tayari tunaishi mikoa mingine sababu tumeajiriwa serikalini

Mzee alifariki 2015, Bi Mkubwa 2023

Pale mjini kuna nyumba mbili, ya kwanza ni ya kitambo tuliyoikuta na kuishi nao wazazi, nyingine tuliijenga watoto miaka ya 2013 lakini mama aliendelea kubaki ile nyumba ya kwanza, baada ya hapo hio nyumba ilikuwa kama abandoned, ni mara chache sana tunaenda watoto.

Ila sasa cha kushangaza hio nyumba kuna mwanafamilia kwa mbinu anazojua yeye akaenda kukopea milioni 30 hivi, Na ajabu ni kwamba yeye tayari ana kazi mshahara almost milioni 4 kasoro na kajenga nyumba nzuri tu huko aliko.

Tunapewa taafifa na Mwenyekiti kwamba kuna Mwanafamilia kakopa pesa hizo kwa kuiweka dhamana nyumba

Taarifa ni kwamaba nyumba inakaribia kuwa mali ya taasisi hio ya kutoa mikopo, Ni kama vile lengo lilikuwa ni kuiuza nyumba bila nia ya kuresha mkopo.

Tulichoamua wanafamilia wengine
Tunaweza kumbana kwenye vyombo vya sheria lakini hatutaki kufika huko, hatutaki hadhara ijue haya matatizo ya kifamilia, hatutaki vyombo vya habari kuanza kututangaza, n.k.

A. Mwanafamilia mwenzetu aliekopa tumempa deadline ya kurudisha hizo fedha zote na riba sambamba na nyaraka za uthibitisho zisizo na shaka maana ni ndani ya uwezo wake na baada ya hapo kuna utaratibu maalum wa kuwajibika kwa alichofanya ikiwemo kwenda kuwaomba wazazi msamaha kaburini na kutuomba sisi msamaha,

B. Akikataa itabidi wanafamilia wengine tujichange tuikomboe nyumba lakini nasikitika kusema huyo mwengine hatakuwa sehemu ya familia tena, he will be an outsider atajijuaga mwenyewe na maisha yake, tutamzikaga tu.
 
Mpunga mrefu...30m....mshahara 4m. Hio nyumba ikoje hadi uchukue 30m uiweke dhamana? Mtu mshahara 4m ashindwe kukopa 30m mpaka ahatarishe nyumba?
 
hizo tamaa 4m na bado unakopa kwa dhamana ya nyumba ya familia
anasa za wazi wazi
 
Mpunga mrefu...30m....mshahara 4m. Hio nyumba ikoje hadi uchukue 30m uiweke dhamana? Mtu mshahara 4m ashindwe kukopa 30m mpaka ahatarishe nyumba?
nyumba ingeuzwa kwa ushirikiano na uwazi ingefika hata 50 japo ilijengwa zamani sana

itakuwa aliona kuiuza moja kwa moja hatweza kufikia malengo yake yaliyomfanya atumie njia ya kuuzia taasisi ya mikopo
 
Mpunga mrefu...30m....mshahara 4m. Hio nyumba ikoje hadi uchukue 30m uiweke dhamana? Mtu mshahara 4m ashindwe kukopa 30m mpaka ahatarishe nyumba?
Kafanya kusudi anajua hawawezi mfanya kitu maana si ndugu zake
Kuna ndugu zetu wana roho mbaya sana na wabinafsi
 
nyumba ingeuzwa kwa ushirikiano na uwazi ingefika hata 50 japo ilijengwa zamani sana

itakuwa aliona kuiuza moja kwa moja hatweza kufikia malengo yake yaliyomfanya atumie njia ya kuuzia taasisi ya mikopo
Wekeni zuio mahakamani hapo
Apambane na hali yake huyo ndugu yenu
 
Mpunga mrefu...30m....mshahara 4m. Hio nyumba ikoje hadi uchukue 30m uiweke dhamana? Mtu mshahara 4m ashindwe kukopa 30m mpaka ahatarishe nyumba?
Huyo amewaletea uhuni tu kukopea nyumba. Kama analengo la kuiuza kabisa, Ila Mshahara wa mil 4 anaweza kopa zaidi ya mil 50
 
Wekeni zuio mahakamani hapo
Apambane na hali yake huyo ndugu yenu
tunaweza lakini ni jambo linaloharibu legacy ya familia katika jicho la hadhara

Tulichoamua wanafamilia wengine

A. Mwanafamilia mwenzetu aliekopa tumempa deadline ya kurudisha hizo fedha zote na riba sambamba na nyaraka za uthibitisho zisizo na shaka maana ni ndani ya uwezo wake na baada ya hapo kuna utaratibu maalum wa kuwajibika kwa alichofanya na kuomba msamaha,

B. akikataa itabidi wanafamilia wengine tujichange tuikomboe nyumba lakini nasikitika kusema huyo mwengine hatakuwa sehemu ya familia tena, he will be an outsider atajijuaga mwenyewe na maisha yake, tutamzikaga tu.
 
tunaweza lakini ni jambo linaloharibu legacy ya familia katika jicho la hadhara

Tulichoamua wanafamilia wengine

A. Mwanafamilia mwenzetu aliekopa tumempa deadline ya kurudisha hizo fedha zote na riba sambamba na nyaraka za uthibitisho zisizo na shaka maana ni ndani ya uwezo wake na baada ya hapo kuna utaratibu maalum wa kuwajibika kwa alichofanya na kuomba msamaha,

B. akikataa itabidi wanafamilia wengine tujichange tuikomboe nyumba lakini nasikitika kusema huyo mwengine hatakuwa sehemu ya familia tena, he will be an outsider atajijuaga mwenyewe na maisha yake, tutamzikaga tu.


Hampaswi hata kujichanga. Nyumba ya familia. Haiwezi uzwa na bank kizembe zembe
 
Hampaswi hata kujichanga. Nyumba ya familia. Haiwezi uzwa na bank kizembe zembe
Cha msingi tumemtaka arudishe hizo pesa zote na riba yote kwa mpigo iwe fundisho kwake, na bado hapo kuna utaratibu wa kuwajibika kwa alichotaka kufanya itamgharimu zaidi sio kwa fedha tu bali hata muda na juhudi ya kurudisha hadhi yake kwenye family, yote hii ni kumtia adabu na kumfunza mali za familia sio za kuchezea
 
Back
Top Bottom