Neno Yesu na neno Kristo Inamaanisha Nini

John Magongwe

Member
Jan 4, 2024
68
117
Neno Yesu na neno Kristo Inamaanisha Nini

Neno Yesu

YESU ni jina la kiuanadamu la Bwana, alilopewa na Mariamu na malaika Gabrieli (Luka 1:31). “Yesu” maana yake ni “Mungu anaokoa”. Hili ndilo neno la Kigiriki linalofanana na neno la Kiebrania “Mashiak”au "Masihi."

Kuna vifungu vingi vya kinabii katika Agano la Kale ambavyo vinalenga kuja kwa Masihi ambaye atakomboa watu wake (Isaya 61:1; Danieli 9:26).

Hili lilikuwa jina la kawaida, na Yesu alizaliwa katika hali duni, mwanadamu, Mwana wa Adamu. Na ilikuwa kwa njia yake kwamba ulimwengu ungeokolewa! Dhambi ilikuwa imekuja ulimwenguni kupitia kutotii na kiburi cha mwanadamu wa kwanza, Adamu. Lakini ndani ya Mwanadamu Yesu, dhambi ilishindwa kupitia unyenyekevu na utii wake kwa Mungu. Kwa kutokubali kamwe kutenda dhambi alipojaribiwa, alishinda nguvu za mauti. Sasa tunaweza kuokolewa kutoka kwa dhambi kupitia kifo cha Yesu msalabani na kupata matunda ya Roho kwa kufuata maisha yake.

Israeli ya kale ilidhani Masihi wao angekuja na nguvu za kijeshi ili kuwaokoa kutoka utumwa wa miongo mingi na wafalme mbalimbali wa dunia hii (ikiwa ni pamoja na wafalme wa Kirumi). Lakini, Agano Jipya linaonyesha ukombozi bora zaidi anaoutoa Kristo Masihi, ni ukombozi kutoka kwa nguvu na adhabu ya dhambi (Luka 4:18; Warumi 6:23).

Wayahudi wa wakati wa Yesu walitarajia Masihi kukomboa Israeli kwa kupindua utawala wa Warumi na kuanzisha ufalme wa kidunia (Matendo ya Mitume 1:6). Baada ya kufufuka kwa Yesu, ndipo hatimaye wanafunzi wake walianza kuelewa ambacho unabii katika Agano la Kale ulimaanisha Masihi angefanya (Luka 24:25-27). Masihi "aliwekwa wakfu" kwanza kuwaokoa watu wake kiroho; kuwakomboa kutoka kwenye dhambi (Yohana 8:31-36). Alikamilisha wokovu huu kupitia kifo na kufufuka kwake (Yohana 3:16, Yohana 12:32).

Agano la Kale lilitabiri kuhusu Mkombozi ajaye, aliyechaguliwa na Mungu kukomboa Israeli (Isaya 42:1; 61:1-3). Mkombozi huyu alijulikana na Wayahudi kama Masihi. Yesu wa Nazareti alikuwa ndiye Masihi aliyetabiriwa (Luka 4:17-21; Yohana 4:25-26).

Neno Kristo
KRISTO ni jina la cheo chake, likiashiria kuwa Yesu alitumwa kutoka kwa Mungu kuwa Mfalme na Mkombozi
(Danieli 9:25; Isaya 32:1).

Kristo siyo jina la mwisho (la ukoo) la Yesu, la hasha. Kristo linatoka kwenye neno la Kigiriki Kristos, maana yake "mtiwa mafuta", au "aliyetiwa wakfu" au "mteule".

Katika Israeli ya kale, wakati mtu alipopewa nafsi ya mamlaka, mafuta yalimiminwa kichwani mwake, ikiwa ni ishara kuwa ametiwa wakfu kwa kazi ya Mungu, yaani ni mteule wa Mungu. Wafalme, makuhani, na manabii walitiwa wakfu namna hiyo. Kutiwa mafuta lilikuwa ni tendo la ishara kuonyesha chaguo la Mungu (1Samwel 10:1, 1Samwel 24:6).

Katika Agano la Kale, watu walitiwa wakfu kwa majukumu ya nabii, kuhani na mfalme. Mungu alimwambia Eliya amtie mafuta Elisha ili awe nabii wa Israeli (1Wafalme 19:16). Haruni aliwekwa wakfu kama kuhani mkuu wa kwanza wa Israeli (Walawi 8:12). Samwel aliweka wakfu Sauli na Daudi kuwa wafalme wa Israeli (1Samweli 10:1; 16:12-13). Wanaume hawa wote walikuwa na majukumu "yaliyotiwa wakfu".

Katika Agano Jipya tunaona thibitisho kwamba Yesu ndiye Mteule: "Lakini hizi zimeandikwa ili mpate kuamini ya kwamba Yesu ndiye Kristo, Mwana wa Mungu; na kwa kuamini muwe na uzima kwa jina lake" (Yohana 20:31). Tunasikia ushuhuda kwamba Yesu ni "Masihi, Mwana wa Mungu aliye hai" (Mathayo 16:16).

Biblia inasema kuwa Yesu alitiwa wakfu kwa mafuta katika matukio mawili tofauti, na wanawake wawili tofauti (Mathayo 26:6-7; Luka 7:37-38). Lakini wakfu muhimu ulikuja wa Roho Mtakatifu (Matendo 10:38). "Kristo" kuwa jina la Yesu inamaanisha Yeye Yesu mwokozi, ndiye Mtiwa Mafuta wa Mungu, yule mmoja aliyetimiza nabii za Agano la Kale, Mwokozi mteule ambaye alikuja kukomboa wenye dhambi (1Timotheo 1:15).

Hii ndiyo sababu Yesu pia alipewa jina la cheo “Kristo”, linalomaanisha “Mtiwa-Mafuta” au “Mteule” au “Masihi”, aliyetumwa na Mungu Baba Yake kwa kazi kubwa ya kuokoa mwanadamu kutoka kwenye dhambi na mauti.

Yesu ni jina linalomaanisha "Mungu anaokoa", na Kristo ni cheo (status) cha Yesu linalomaanisha kuwa ni Mteule au Mtiwa Mafuta wa Mungu.
Hivyo, jina YESU KRISTO
linamaanisha Yesu Masihi au Yesu Mtiwa Mafuta au Yesu Mteule wa Mungu.
 
Neno Yesu na neno Kristo Inamaanisha Nini

Neno Yesu

YESU ni jina la kiuanadamu la Bwana, alilopewa na Mariamu na malaika Gabrieli (Luka 1:31). “Yesu” maana yake ni “Mungu anaokoa”. Hili ndilo neno la Kigiriki linalofanana na neno la Kiebrania “Mashiak”au "Masihi."

Kuna vifungu vingi vya kinabii katika Agano la Kale ambavyo vinalenga kuja kwa Masihi ambaye atakomboa watu wake (Isaya 61:1; Danieli 9:26).

Hili lilikuwa jina la kawaida, na Yesu alizaliwa katika hali duni, mwanadamu, Mwana wa Adamu. Na ilikuwa kwa njia yake kwamba ulimwengu ungeokolewa! Dhambi ilikuwa imekuja ulimwenguni kupitia kutotii na kiburi cha mwanadamu wa kwanza, Adamu. Lakini ndani ya Mwanadamu Yesu, dhambi ilishindwa kupitia unyenyekevu na utii wake kwa Mungu. Kwa kutokubali kamwe kutenda dhambi alipojaribiwa, alishinda nguvu za mauti. Sasa tunaweza kuokolewa kutoka kwa dhambi kupitia kifo cha Yesu msalabani na kupata matunda ya Roho kwa kufuata maisha yake.

Israeli ya kale ilidhani Masihi wao angekuja na nguvu za kijeshi ili kuwaokoa kutoka utumwa wa miongo mingi na wafalme mbalimbali wa dunia hii (ikiwa ni pamoja na wafalme wa Kirumi). Lakini, Agano Jipya linaonyesha ukombozi bora zaidi anaoutoa Kristo Masihi, ni ukombozi kutoka kwa nguvu na adhabu ya dhambi (Luka 4:18; Warumi 6:23).

Wayahudi wa wakati wa Yesu walitarajia Masihi kukomboa Israeli kwa kupindua utawala wa Warumi na kuanzisha ufalme wa kidunia (Matendo ya Mitume 1:6). Baada ya kufufuka kwa Yesu, ndipo hatimaye wanafunzi wake walianza kuelewa ambacho unabii katika Agano la Kale ulimaanisha Masihi angefanya (Luka 24:25-27). Masihi "aliwekwa wakfu" kwanza kuwaokoa watu wake kiroho; kuwakomboa kutoka kwenye dhambi (Yohana 8:31-36). Alikamilisha wokovu huu kupitia kifo na kufufuka kwake (Yohana 3:16, Yohana 12:32).

Agano la Kale lilitabiri kuhusu Mkombozi ajaye, aliyechaguliwa na Mungu kukomboa Israeli (Isaya 42:1; 61:1-3). Mkombozi huyu alijulikana na Wayahudi kama Masihi. Yesu wa Nazareti alikuwa ndiye Masihi aliyetabiriwa (Luka 4:17-21; Yohana 4:25-26).

Neno Kristo
KRISTO ni jina la cheo chake, likiashiria kuwa Yesu alitumwa kutoka kwa Mungu kuwa Mfalme na Mkombozi
(Danieli 9:25; Isaya 32:1).

Kristo siyo jina la mwisho (la ukoo) la Yesu, la hasha. Kristo linatoka kwenye neno la Kigiriki Kristos, maana yake "mtiwa mafuta", au "aliyetiwa wakfu" au "mteule".

Katika Israeli ya kale, wakati mtu alipopewa nafsi ya mamlaka, mafuta yalimiminwa kichwani mwake, ikiwa ni ishara kuwa ametiwa wakfu kwa kazi ya Mungu, yaani ni mteule wa Mungu. Wafalme, makuhani, na manabii walitiwa wakfu namna hiyo. Kutiwa mafuta lilikuwa ni tendo la ishara kuonyesha chaguo la Mungu (1Samwel 10:1, 1Samwel 24:6).

Katika Agano la Kale, watu walitiwa wakfu kwa majukumu ya nabii, kuhani na mfalme. Mungu alimwambia Eliya amtie mafuta Elisha ili awe nabii wa Israeli (1Wafalme 19:16). Haruni aliwekwa wakfu kama kuhani mkuu wa kwanza wa Israeli (Walawi 8:12). Samwel aliweka wakfu Sauli na Daudi kuwa wafalme wa Israeli (1Samweli 10:1; 16:12-13). Wanaume hawa wote walikuwa na majukumu "yaliyotiwa wakfu".

Katika Agano Jipya tunaona thibitisho kwamba Yesu ndiye Mteule: "Lakini hizi zimeandikwa ili mpate kuamini ya kwamba Yesu ndiye Kristo, Mwana wa Mungu; na kwa kuamini muwe na uzima kwa jina lake" (Yohana 20:31). Tunasikia ushuhuda kwamba Yesu ni "Masihi, Mwana wa Mungu aliye hai" (Mathayo 16:16).

Biblia inasema kuwa Yesu alitiwa wakfu kwa mafuta katika matukio mawili tofauti, na wanawake wawili tofauti (Mathayo 26:6-7; Luka 7:37-38). Lakini wakfu muhimu ulikuja wa Roho Mtakatifu (Matendo 10:38). "Kristo" kuwa jina la Yesu inamaanisha Yeye Yesu mwokozi, ndiye Mtiwa Mafuta wa Mungu, yule mmoja aliyetimiza nabii za Agano la Kale, Mwokozi mteule ambaye alikuja kukomboa wenye dhambi (1Timotheo 1:15).

Hii ndiyo sababu Yesu pia alipewa jina la cheo “Kristo”, linalomaanisha “Mtiwa-Mafuta” au “Mteule” au “Masihi”, aliyetumwa na Mungu Baba Yake kwa kazi kubwa ya kuokoa mwanadamu kutoka kwenye dhambi na mauti.

Yesu ni jina linalomaanisha "Mungu anaokoa", na Kristo ni cheo (status) cha Yesu linalomaanisha kuwa ni Mteule au Mtiwa Mafuta wa Mungu.
Hivyo, jina YESU KRISTO
linamaanisha Yesu Masihi au Yesu Mtiwa Mafuta au Yesu Mteule wa Mungu.
Kwa hekima na uwezo alokuwa nao Mungu hakuona njia nyingine yoyote ya kumkomboa mwanadamu ila kwa kupitia njia ya hovyo aliyoitumia! Kwamba amtume mwanawe aingie tumboni mwa mwanamke (kwa njia ya roho), azaliwe, ahubiri na kutenda miujiza kadhaa, kisha ateswe na kuuawa kikatili. Halafu afufuke baada ya siku 3 (kila mtume aliyeelezea tukio la ufufuko wake ana stori tofauti) na kurudi kwa babaye kwa kupaa kama ndege. Halafu mtu unajiuliza: kama kwa mlolongo huu wa matukio mwanadamu amekombolewa kwa kuondolewa dhambi, hawa mitume na manabii wa kila uchwao ni wa nini?
 
Yesu: ni moja ya majina ya Mungu ambalo alimrithisha mwanae. Huyu tunayemjua na kumjita Yesu, ili jina alirithishwa na Babaye Mumgu Baba.

Neno Kristo (Christ) maana yake "mpakwa mafuta". Kiroho huwezi kufanya kazi ya Mungu bila kupakwa mafuta! Kupakwa mafuta ndo kunamuwezesha Roho mtakatifu kukupa nguvu
 
Yesu ni jina lake..
Kristu ni cheo chake.
Abraham ni Kristu.
Moses ni Kristu.
Buddha ni Kristu.
 
Kwa hekima na uwezo alokuwa nao Mungu hakuona njia nyingine yoyote ya kumkomboa mwanadamu ila kwa kupitia njia ya hovyo aliyoitumia! Kwamba amtume mwanawe aingie tumboni mwa mwanamke (kwa njia ya roho), azaliwe, ahubiri na kutenda miujiza kadhaa, kisha ateswe na kuuawa kikatili. Halafu afufuke baada ya siku 3 (kila mtume aliyeelezea tukio la ufufuko wake ana stori tofauti) na kurudi kwa babaye kwa kupaa kama ndege. Halafu mtu unajiuliza: kama kwa mlolongo huu wa matukio mwanadamu amekombolewa kwa kuondolewa dhambi, hawa mitume na manabii wa kila uchwao ni wa nini?
Hebu ndugu wewe suggest njia gani ingekuwa bora kwa Mungu kuitumia ili kumkomboa mwanadamu ambaye tayari alikuwa ameanguka dhambini.
 
Neno Yesu na neno Kristo Inamaanisha Nini

Neno Yesu

YESU ni jina la kiuanadamu la Bwana, alilopewa na Mariamu na malaika Gabrieli (Luka 1:31). “Yesu” maana yake ni “Mungu anaokoa”. Hili ndilo neno la Kigiriki linalofanana na neno la Kiebrania “Mashiak”au "Masihi."

Kuna vifungu vingi vya kinabii katika Agano la Kale ambavyo vinalenga kuja kwa Masihi ambaye atakomboa watu wake (Isaya 61:1; Danieli 9:26).

Hili lilikuwa jina la kawaida, na Yesu alizaliwa katika hali duni, mwanadamu, Mwana wa Adamu. Na ilikuwa kwa njia yake kwamba ulimwengu ungeokolewa! Dhambi ilikuwa imekuja ulimwenguni kupitia kutotii na kiburi cha mwanadamu wa kwanza, Adamu. Lakini ndani ya Mwanadamu Yesu, dhambi ilishindwa kupitia unyenyekevu na utii wake kwa Mungu. Kwa kutokubali kamwe kutenda dhambi alipojaribiwa, alishinda nguvu za mauti. Sasa tunaweza kuokolewa kutoka kwa dhambi kupitia kifo cha Yesu msalabani na kupata matunda ya Roho kwa kufuata maisha yake.

Israeli ya kale ilidhani Masihi wao angekuja na nguvu za kijeshi ili kuwaokoa kutoka utumwa wa miongo mingi na wafalme mbalimbali wa dunia hii (ikiwa ni pamoja na wafalme wa Kirumi). Lakini, Agano Jipya linaonyesha ukombozi bora zaidi anaoutoa Kristo Masihi, ni ukombozi kutoka kwa nguvu na adhabu ya dhambi (Luka 4:18; Warumi 6:23).

Wayahudi wa wakati wa Yesu walitarajia Masihi kukomboa Israeli kwa kupindua utawala wa Warumi na kuanzisha ufalme wa kidunia (Matendo ya Mitume 1:6). Baada ya kufufuka kwa Yesu, ndipo hatimaye wanafunzi wake walianza kuelewa ambacho unabii katika Agano la Kale ulimaanisha Masihi angefanya (Luka 24:25-27). Masihi "aliwekwa wakfu" kwanza kuwaokoa watu wake kiroho; kuwakomboa kutoka kwenye dhambi (Yohana 8:31-36). Alikamilisha wokovu huu kupitia kifo na kufufuka kwake (Yohana 3:16, Yohana 12:32).

Agano la Kale lilitabiri kuhusu Mkombozi ajaye, aliyechaguliwa na Mungu kukomboa Israeli (Isaya 42:1; 61:1-3). Mkombozi huyu alijulikana na Wayahudi kama Masihi. Yesu wa Nazareti alikuwa ndiye Masihi aliyetabiriwa (Luka 4:17-21; Yohana 4:25-26).

Neno Kristo
KRISTO ni jina la cheo chake, likiashiria kuwa Yesu alitumwa kutoka kwa Mungu kuwa Mfalme na Mkombozi
(Danieli 9:25; Isaya 32:1).

Kristo siyo jina la mwisho (la ukoo) la Yesu, la hasha. Kristo linatoka kwenye neno la Kigiriki Kristos, maana yake "mtiwa mafuta", au "aliyetiwa wakfu" au "mteule".

Katika Israeli ya kale, wakati mtu alipopewa nafsi ya mamlaka, mafuta yalimiminwa kichwani mwake, ikiwa ni ishara kuwa ametiwa wakfu kwa kazi ya Mungu, yaani ni mteule wa Mungu. Wafalme, makuhani, na manabii walitiwa wakfu namna hiyo. Kutiwa mafuta lilikuwa ni tendo la ishara kuonyesha chaguo la Mungu (1Samwel 10:1, 1Samwel 24:6).

Katika Agano la Kale, watu walitiwa wakfu kwa majukumu ya nabii, kuhani na mfalme. Mungu alimwambia Eliya amtie mafuta Elisha ili awe nabii wa Israeli (1Wafalme 19:16). Haruni aliwekwa wakfu kama kuhani mkuu wa kwanza wa Israeli (Walawi 8:12). Samwel aliweka wakfu Sauli na Daudi kuwa wafalme wa Israeli (1Samweli 10:1; 16:12-13). Wanaume hawa wote walikuwa na majukumu "yaliyotiwa wakfu".

Katika Agano Jipya tunaona thibitisho kwamba Yesu ndiye Mteule: "Lakini hizi zimeandikwa ili mpate kuamini ya kwamba Yesu ndiye Kristo, Mwana wa Mungu; na kwa kuamini muwe na uzima kwa jina lake" (Yohana 20:31). Tunasikia ushuhuda kwamba Yesu ni "Masihi, Mwana wa Mungu aliye hai" (Mathayo 16:16).

Biblia inasema kuwa Yesu alitiwa wakfu kwa mafuta katika matukio mawili tofauti, na wanawake wawili tofauti (Mathayo 26:6-7; Luka 7:37-38). Lakini wakfu muhimu ulikuja wa Roho Mtakatifu (Matendo 10:38). "Kristo" kuwa jina la Yesu inamaanisha Yeye Yesu mwokozi, ndiye Mtiwa Mafuta wa Mungu, yule mmoja aliyetimiza nabii za Agano la Kale, Mwokozi mteule ambaye alikuja kukomboa wenye dhambi (1Timotheo 1:15).

Hii ndiyo sababu Yesu pia alipewa jina la cheo “Kristo”, linalomaanisha “Mtiwa-Mafuta” au “Mteule” au “Masihi”, aliyetumwa na Mungu Baba Yake kwa kazi kubwa ya kuokoa mwanadamu kutoka kwenye dhambi na mauti.

Yesu ni jina linalomaanisha "Mungu anaokoa", na Kristo ni cheo (status) cha Yesu linalomaanisha kuwa ni Mteule au Mtiwa Mafuta wa Mungu.
Hivyo, jina YESU KRISTO
linamaanisha Yesu Masihi au Yesu Mtiwa Mafuta au Yesu Mteule wa Mungu.
Kwanini jina la Yesu lilibadilishwa kutoka jina lake halisi kwenda kwenye jina hili linalotumika sasa?

Manake lile jina lake halisi ndio lilikua na maana hiyo uliyoisema, na sio hili la sasa ambalo halina maana yoyote.
 
Kwa hekima na uwezo alokuwa nao Mungu hakuona njia nyingine yoyote ya kumkomboa mwanadamu ila kwa kupitia njia ya hovyo aliyoitumia! Kwamba amtume mwanawe aingie tumboni mwa mwanamke (kwa njia ya roho), azaliwe, ahubiri na kutenda miujiza kadhaa, kisha ateswe na kuuawa kikatili. Halafu afufuke baada ya siku 3 (kila mtume aliyeelezea tukio la ufufuko wake ana stori tofauti) na kurudi kwa babaye kwa kupaa kama ndege. Halafu mtu unajiuliza: kama kwa mlolongo huu wa matukio mwanadamu amekombolewa kwa kuondolewa dhambi, hawa mitume na manabii wa kila uchwao ni wa nini?
Ukiwa na akili kubwa sana ndiyo utagundua siri ya hayo mambo unayo ya shangaa ..kuna siri kubwa sana la sivyo utayaona haya eleweki ...kosa la kwanza ambalo wakristo wanalifanya na kusababisha wasielewe logic ni kutokujua SABABU YA KWELI YA KUSULUBIWA YESU wao wanapotosha kwa kusema ni DHAMBI YA ASILI ...huo ni uongo Yesu akusulubiwa kwa sababu ya DHAMBI YA ASILI ...kwanini ? kwa sababu hakuna dhambi ya asili ...je Yesu alisulubiwa kwa sababu ya DHAMBI ? jibu ni ndiyo ...hapa utaona kuna mambo mawili nayo ni DHAMBI YA ASILI NA DHAMBI ...Majibu yote ya maswali yako yapo kwenye logic ya kusulibiwa Yesu kwa sababu ya dhambi na siyo uongo wa dhambu ya asili mnayo potoshwa makanisani .
 
Ukiwa na akili kubwa sana ndiyo utagundua siri ya hayo mambo unayo ya shangaa ..kuna siri kubwa sana la sivyo utayaona haya eleweki ...kosa la kwanza ambalo wakristo wanalifanya na kusababisha wasielewe logic ni kutokujua SABABU YA KWELI YA KUSUL8BIWA YESU wao wanapotosha kwa kusema ni DHAMBI YA ASILI ...huo ni uongo Yesu akusulubiwa kwa sababu ya DHAMBI YA ASILI ...kwanini ? ji kwa sababu hakuna dhambi ya asili ...je Yesu alisulubiwa kwa sababu ya DHAMBI ? jibu ni ndiyo ...hapa utaona kuna mambo mawili nayo ni DHAMBI YA ASILI NA DHAMBI ...Majibu yote ya maswali ysko yapo kwenye logic ya kusulibiwa tesu kwa sababu ya dhambi na siyo uongo wa dhambu ya asili mnayo poyoshwa makanisani .
Ukiisoma historia ya kusulubiwa kwa Yesu, alitundikwa msalabani kama adhabu, si kwa sababu ya ukombozi au dhambi za wanadamu.
Alifanya makosa na akatundikwa msalabani na wenzake wawili.
 
Ukiisoma historia ya kusulubiwa kwa Yesu, alitundikwa msalabani kama adhabu, si kwa sababu ya ukombozi au dhambi za wanadamu.
Alifanya makosa na akatundikwa msalabani na wenzake wawili.
Yesu alisulibiwa kwa sababu ya dhambi ...alitundikwa masalabani kuwa SADAKA TAKATIFU KWA MUNGU hapo ndiyo ilipo siri hiyo sadaka ilikuwa kwa kazi gani ukiweza kujua hiyo siri utajua kwanini iliandika 👉shetani alianguka kutoka juu mwenye uchungu mwingi ...pia utajua kwanini iliandikwa👉 kuwa kulikuwa na vita mbinguni ...pia utajua siri ya hasira ya mungu ..kabla ya yesu kusulubiwa ilikuwaje na baada ya yesu kusulubiwa ilikuwaje ? Kuna tofauti ilifanyika baada ya kusulubiwa kwa yesu ...pia utajua👉 kwanini siku ya kihama hakuna TOBA....pia unajua👉 kwanini imeandikwa kuwa mungu akakinywea kikombe cha ghadhabu yake ....pia utajua👉 hicho kikombe kimetoka wapi na zamani kilikuwa wapi ...pia utajua👉 kwa nini Paulo alionya kuhusu torati kwa kusema 👉 nyinyi mnao endelea kufuata torati...kwenye hiyo torati kuna JIWE LIKWAALO NA MWAMBA UZUIAO..

HAPO KUNA SIRI KUBWA SANA NA NDIYO SABABU MTUME MUHAMMAD WA WAISLAMU ANA PINGA SANA KUHUSU YESU KUSULIBIWA ...NDIYO MAANA YA YALE MAANDIKO KUWA SETANI KAANGUKA CHINI MWENYE UCHUNGU NA GHADHABU NYINGI ....swali kwanini muhammad anaumia sana kusikia kuwa Yesu alisulubiwa hapo pana siri maana mtume kuuliwa au kupalizwa mbinguni siyo dhambi hata kuwa na uchungu kwa muhammad kuusu yesu kusulibiwa kitu cha msingi ni kutokutenda dhambi aijalishi ulipaa mbinguni au ulikufa jinsi gani ....sasa kuna hasara kubwa sana kwa shetani kutokana na yesu kujitoa sadaka uhai wake kama alivyo sema yeye mwenyewe najitoa uhai sadaka mimi mwenyewe hakuna anitoaye nami ninao uwezo wa kujitoa sadaka uhai na ninao uwezo wa kuutwaa uhai tena ...hakuna anitoaye bali najitoa mwenyewe..

SITAKI KUKUTAFUNIENI KIRAHISI INJILI YA KWELI ILA NATAKA MJIFUNZE KUTUMIA AKILI KUTAMBUA MAMBO ...SASA NITAKUPA SIRI KIDOGO YA SABABU YA YESU KUSULIBIWA
1) YESU ALISULIBIWA KUJITOA SADAKA KWA MUNGU KWA AJILI YA DHAMBI ZETU
2) YESU ALISULIBIWA KWA AJILI YA DHAMBI ZETU NA KWA AJILI YA HASIRA YA MUNGU....hapo kwenye hasira ndiyo hiyo sadaka imesababisha kuwe na kikombe cha dhadhabu ya mungu nje ya nafsi ya mungu ...

💥💥Zamani kabla ya yesu kujitoa sadaka ghadhabu ya mungu ilikuwa inakaa nafsini mwa Mungu 💥💥 siku ambayo Mungu atakinyea kikombe cha ghadhabu yake na ndiyo hiyo ghadhabu itarudi mahali pake ..yaani nafsini mwa Mungu hapo ndiyo utakuwa mwisho wa toba kwa viumbe vyake hakutawezekana tena toba hata utubu kwa namna kuu kiasi gani....ndiyo maana ya yale maandiko yanayo sema 👉 Milango ya Hekalu itawekwa moto) huo moto ndiyo hasira ya Mungu hakuna hatakaye weza kuivuka kuingia ndani ya hekalu ...yaani hakutakuwa na toba tena kwa wenye dhambi .
 
Tutafanya makosa kama tutamhoji Mungu kama mwanadamu.Mungu ni Roho .Anayeweza kufanya mambo ya hovyo ni shetani kupitia rafiki zake wanadamu.Mungu anajidhihirisha kupitia wanadamu wanaomwamini na kuyarenda mapenzi yake.
 
Na Emmanuel ni nani?.
Ila Biblia inafurahisha sana, inasema mtoto atakayezaliwa na bikira Maria ataitwa Emmanuel halafu hakuna sehemu yoyote inayomtaja Yesu kwa jina la Emmanuel.

Hii maana yake ni nini?, msije mkasema ni fumbo la imani. Nataka majibu yanayoeleweka.
 
Kwa hekima na uwezo alokuwa nao Mungu hakuona njia nyingine yoyote ya kumkomboa mwanadamu ila kwa kupitia njia ya hovyo aliyoitumia! Kwamba amtume mwanawe aingie tumboni mwa mwanamke (kwa njia ya roho), azaliwe, ahubiri na kutenda miujiza kadhaa, kisha ateswe na kuuawa kikatili. Halafu afufuke baada ya siku 3 (kila mtume aliyeelezea tukio la ufufuko wake ana stori tofauti) na kurudi kwa babaye kwa kupaa kama ndege. Halafu mtu unajiuliza: kama kwa mlolongo huu wa matukio mwanadamu amekombolewa kwa kuondolewa dhambi, hawa mitume na manabii wa kila uchwao ni wa nini?
Wewe ni mkristo?
 
Na Emmanuel ni nani?.
Ila Biblia inafurahisha sana, inasema mtoto atakayezaliwa na bikira Maria ataitwa Emmanuel halafu hakuna sehemu yoyote inayomtaja Yesu kwa jina la Emmanuel.

Hii maana yake ni nini?, msije mkasema ni fumbo la imani. Nataka majibu yanayoeleweka.
Mbona hii haiitaji rocket science Kama unajua maana ya Emmamuel na ya ujio wa Yesu duniani.
 
Yesu: ni moja ya majina ya Mungu ambalo alimrithisha mwanae. Huyu tunayemjua na kumjita Yesu, ili jina alirithishwa na Babaye Mumgu Baba.

Neno Kristo (Christ) maana yake "mpakwa mafuta". Kiroho huwezi kufanya kazi ya Mungu bila kupakwa mafuta! Kupakwa mafuta ndo kunamuwezesha Roho mtakatifu kukupa nguvu
Morning_star mpakwa mafuta mana yake nini?
 
Mbona hii haiitaji rocket science Kama unajua maana ya Emmamuel na ya ujio wa Yesu duniani.
Unajua kwanini kuna madhehebu tofauti tofauti zaidi ya 45,000 ya Kikristo duniani?

Ni kwasababu Biblia inasema kitu straight kabisa, mfano; Matayo 1:23
"Tazama bikira atachukua mimba, naye atamzaa mtoto wa kiume nao watamwita Imanueli" maana yake, "Mungu pamoja nasi"

Halafu baadhi ya watu wananza kutafsiri hicho kilichosemwa, na kuanza kusema biblia haikumaanisha hivyo!

Hapa mleta mada anatuambia "Yesu" maana yake ni "Mungu anaokoa" kitu ambacho SIO KWELI! Neno YESU halina maana yoyote kwenye lugha yoyote, na silo jina alilokuwa akiitwa huyo tunaemuita leo YESU.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom