Sexer
JF-Expert Member
- Oct 22, 2014
- 8,432
- 8,140
Saudi Arabia imesitisha uhusiano wa kidiplomasia na nchi ya Iran na huku kukiwa na hali mbaya ya mvutano kufuatia utekelezaji adhabu ya kifo kwa mhubiri maarufu wa dini ya Kiislamu.
Waziri wa mambo ya kigeni wa Saudia, Adel al-Jubeir, ameishutumu serikali ya Iran kwa kusambaza silaha na kuanzisha jela na kuwafunga watu wanaodhaniwa magaidi katika ukanda wake .
Waziri huyo amesema wanadiplomasia wa Iran wanatakiwa kuondoka Saudia ndani ya saa arobaini.
Mwishoni mwa wiki iliyopita, waandamanaji mjini Tehran waliuvamia ubalozi wa Saudia mjini Tehran, huku wakilaani utekelezaji wa hukumu ya kifo kwa Sheikh Nimr al-Nimr na watu wengine 46.
Watu hao waliouawa inasadikiwa walikuwa na hatia ya makosa yanayohusiana na ugaidi.
Kiongozi mkuu wa Iran alimweleza Sheikh huyo kama shahidi ambaye alikuwa akitetea amani na kufanya maandamano ya amani.
==============
==============
UPDATE
Washirika kadha wa Saudi Arabia wamejiunga na taifa hilo katika kuvunja uhusiano na Iran huku mvutano ukizidi kuhusu kuuawa kwa mhubiri wa Kishia.
Mataifa hayo ni Bahrain, Sudan na Jumuiya ya Milki za Kiarabu (UAE).
Saudi Arabia ilikuwa imewapa wanabalozi wa Iran siku mbili kuondoka nchini Saudi Arabia kufuatia mvutano uliotokana na kuuawa kwa mhubiri maarufu wa Kishia.
Bahrain, ambayo hutawaliwa na Mfalme Msuni lakini raia wengi ni wa dhehebu la Shia, nayo ilifuata wa kuvunja uhusiano.
Ufalme huo pia uliwapa wanabalozi wa Iran saa 48 wawe wameondoka nchini humo.
Sudan nayo ilimfukuza balozi wa Iran kutoka Khartoum huku UAE nayo ikipunguza idadi ya maafisa wa ubalozi. Waislamu wengi nchini Sudan ni Wasuni.
Taarifa ya wizara ya ammbo ya nje ya Sudan imesema: "Kufuatia mashambulio ya kikatili dhidi ya ubalozi wa Saudi Arabia mjini Tehran na afisi yake ya ubalozi Mashhad... Sudan inatakaza kwamba imevunja uhusiano na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran."
Mhubiri huyo Sheikh Nimr al-Nimr aliuawa pamoja na watu wengine 46 baada ya kupatikana na makosa yanayohusiana na ugaidi.
Washia walishutumu hatua hiyo na maandamano yalishuhudia maeneo yenye Washia wengi.
Mjini Tehran, waandamanaji waliteketeza majengo ya ubalozi wa Saudi Arabia.
Saudi Arabia na Iran ndiyo mataifa makuu ya Kisuni na Kishia mtawalia Mashariki ya Kati, na yamekuwa yakiunga mkono pande pinzani katika mizozo inayoendelea Syria na Yemen.
Kuna wasiwasi huenda machafuko yakatokea kanda hiyo.
Jumatatu, misikiti miwili ya Wasuni ilishambuliwa na imam mmoja akauawa.
Saudi Arabia ilitangaza kwamba imekatiza uhusiano wake na Iran baada ya maandamano yaliyotokea ubalozi wake mjini Iran. Ilisema pia kwamba imemwagiza balozi wake arejee nyumbani.
Wizara ya mambo ya nje ya Iran imesema Saudi Arabia inaendeleza sera ya kuzidisha chuki na makambiliano katika kanda hiyo.
Msemaji wa wizara hiyo Hossein Jaber Ansari alisema Jumatatu kwamba Saudi Arabia inajaribu kusuluhisha matatizo yake ya kinyumbani kwa “kuyatoa nje kwa mataifa mengine”.
Chanzo: BBC Swahili
Waziri wa mambo ya kigeni wa Saudia, Adel al-Jubeir, ameishutumu serikali ya Iran kwa kusambaza silaha na kuanzisha jela na kuwafunga watu wanaodhaniwa magaidi katika ukanda wake .
Waziri huyo amesema wanadiplomasia wa Iran wanatakiwa kuondoka Saudia ndani ya saa arobaini.
Mwishoni mwa wiki iliyopita, waandamanaji mjini Tehran waliuvamia ubalozi wa Saudia mjini Tehran, huku wakilaani utekelezaji wa hukumu ya kifo kwa Sheikh Nimr al-Nimr na watu wengine 46.
Watu hao waliouawa inasadikiwa walikuwa na hatia ya makosa yanayohusiana na ugaidi.
Kiongozi mkuu wa Iran alimweleza Sheikh huyo kama shahidi ambaye alikuwa akitetea amani na kufanya maandamano ya amani.
==============
Saudi Arabia yavunja uhusiano wa kidiplomasia na Iran
Saudi Arabia imevunja uhusiano wake wa kidiplomasia na Iran jana, baada ya waandamanaji kuuvamia ubalozi wake mjini Tehran, kupinga kuuawa kwa kiongozi wa Kishia mwishoni mwa wiki. Waziri wa mambo ya nje wa Saudi Arabia Adel al-Jubeir ametoa tangazo hilo katika mkutano na waandishi habari mjini Riyadh, na kusema wanadiplomasia wa Iran wana muda wa masaa 48 kuondoka nchini humo.
Mzozo huo wa kidiplomasia unakuja wakati kiongozi wa juu wa Iran akisema Saudi Arabia italipiziwa kisasi haraka kwa kumuuwa Sheikh Nimr al-Nimr, na wakati Marekani ikiwataka viongozi wa kanda hiyo kutuliza mvutano kati ya Waislamu wa madhehebu ya Sunni na Shia. Siku ya Jumamosi, kundi la waandamanaji liliuvamia ubalozi wa Saudi Arabia mjini Tehran, na pia ubalozi mdogo katika mji wapili wa Mashhad katika maandamano ya kupinga kuuawa kwa Nimr mwenye umri wa miaka 56. Nimr aliuawa pamoja na watu wengine 46, wakiwemo wanaharakati wa Kishia na wapiganaji wa Kisunni, ambao wizara ya mambo ya ndani ya Saudi inasema walishiriki katika mashambulizi ya Alqaeda yaliyouwa watu wengi mwaka 2003 na 2004.
==============
UPDATE
Washirika kadha wa Saudi Arabia wamejiunga na taifa hilo katika kuvunja uhusiano na Iran huku mvutano ukizidi kuhusu kuuawa kwa mhubiri wa Kishia.
Mataifa hayo ni Bahrain, Sudan na Jumuiya ya Milki za Kiarabu (UAE).
Saudi Arabia ilikuwa imewapa wanabalozi wa Iran siku mbili kuondoka nchini Saudi Arabia kufuatia mvutano uliotokana na kuuawa kwa mhubiri maarufu wa Kishia.
Bahrain, ambayo hutawaliwa na Mfalme Msuni lakini raia wengi ni wa dhehebu la Shia, nayo ilifuata wa kuvunja uhusiano.
Ufalme huo pia uliwapa wanabalozi wa Iran saa 48 wawe wameondoka nchini humo.
Sudan nayo ilimfukuza balozi wa Iran kutoka Khartoum huku UAE nayo ikipunguza idadi ya maafisa wa ubalozi. Waislamu wengi nchini Sudan ni Wasuni.
Taarifa ya wizara ya ammbo ya nje ya Sudan imesema: "Kufuatia mashambulio ya kikatili dhidi ya ubalozi wa Saudi Arabia mjini Tehran na afisi yake ya ubalozi Mashhad... Sudan inatakaza kwamba imevunja uhusiano na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran."
Mhubiri huyo Sheikh Nimr al-Nimr aliuawa pamoja na watu wengine 46 baada ya kupatikana na makosa yanayohusiana na ugaidi.
Washia walishutumu hatua hiyo na maandamano yalishuhudia maeneo yenye Washia wengi.
Mjini Tehran, waandamanaji waliteketeza majengo ya ubalozi wa Saudi Arabia.
Saudi Arabia na Iran ndiyo mataifa makuu ya Kisuni na Kishia mtawalia Mashariki ya Kati, na yamekuwa yakiunga mkono pande pinzani katika mizozo inayoendelea Syria na Yemen.
Kuna wasiwasi huenda machafuko yakatokea kanda hiyo.
Jumatatu, misikiti miwili ya Wasuni ilishambuliwa na imam mmoja akauawa.
Saudi Arabia ilitangaza kwamba imekatiza uhusiano wake na Iran baada ya maandamano yaliyotokea ubalozi wake mjini Iran. Ilisema pia kwamba imemwagiza balozi wake arejee nyumbani.
Wizara ya mambo ya nje ya Iran imesema Saudi Arabia inaendeleza sera ya kuzidisha chuki na makambiliano katika kanda hiyo.
Msemaji wa wizara hiyo Hossein Jaber Ansari alisema Jumatatu kwamba Saudi Arabia inajaribu kusuluhisha matatizo yake ya kinyumbani kwa “kuyatoa nje kwa mataifa mengine”.
Chanzo: BBC Swahili
Last edited by a moderator: