Nashauri kamati ya kufanya tathmini iwe na wajumbe wafanyabiashara na wamiliki wa viwanda badala ya kuundwa na watumishi wa umma wasiofanya biashara

Resilience

JF-Expert Member
Jan 4, 2023
1,005
4,664
Nampongeza Mhe. Rais kwa kuunda kamati ya kufanya mapitio ya mfumo wa kodi nchini.

Natambua wafanyabiashara na wamiliki wa viwanda, migodi na maeneo mengine ya uwekezaji watakuwa respondent kwenye kamati lakini nashauri kwenye timu ya wajumbe wawepo pia.

Wanaolalamika ni wafanyabiashara na hivyo unapotaka kufanya utafiti na kuandika facts tunapaswa kuwapa nafasi pia.

Lakini pia jambo la kodi lina mirengo miwili, kuna kodi za ndani na kuna kodi na mazingira ya kibiashara ya kimataifa. Kwa maana hiyo wanaopaswa kufanya tathmini ya kodi siyo watanzania pekee bali wageni pia kulingana na uwekezaji wao wanapaswa kushiriki.

Nimeona timu, imejaa watumishi wa umma na ikakosa watu wenye business mind. Naamini kwa muundo bora wa tax reform tuone pia namna wafanyabiashara na wawekezaji watakuwa sehemu ya tume na sehemu ya kamati ya wataalamu.

Once again, nimpongeze Mhe. Rais kwamba mambo mengi anayofanya yamekaa kitaaluma na yanalenga kubomoa na kuunda sera zetu kuendana na mahitaji ya miaka ijayo. She working hardly on doing oway with traditional ways of running government to modern ways of copying with changing global dynamics
 
Umeniwahi tu...naunga mkono hoja. Binafsi ningeshauri wajumbe wengine watano.

1. Mwakilishi vyama vya wafanyakazi
2. Mwakilishi sekta ya viwanda
3. Mwakilishi wa wakulima
4. Mwakilishi Madini
5. Mwakilishi sekta ya utalii

Lengo lisiwe kuangalia kodi kwa macho ya kitaaluma bali kihalisia na inavyogusa maisha ya sekta mbalimbali.
 
Umeniwahi tu...naunga mkono hoja. Binafsi ningeshauri wajumbe wengine watano.

1. Mwakilishi vyama vya wafanyakazi
2. Mwakilishi sekta ya viwanda
3. Mwakilishi wa wakulima
4. Mwakilishi Madini
5. Mwakilishi sekta ya utalii

Lengo lisiwe kuangalia kodi kwa macho ya kitaaluma bali kihalisia na inavyogusa maisha ya sekta mbalimbali.
Bila kusahau Mwakilishi wa wqfanyabiashara wadogo na wa kati
 
Back
Top Bottom