Mzazi mwenzangu hataki mtoto apate Elimu nzuri, nadhani hajui elimu ni kwa faida ya mtoto sio mimi wala yeye

kiredio Jr

JF-Expert Member
Jul 8, 2024
956
1,763
Habarini ndugu

Mimi na mzazi mwenzangu bado hatuna ndoa, ila tumebahatika kupata mtoto mmoja, kwa sasa wamerudi mkoani baada ya kuja na kukaa nyumbani kwetu kwa lengo la kumleta mtoto familia yangu imtambue.

Baada ya mtoto kufikisha miaka mitatu na nusu, nikamwambia mama yake itabidi mtoto aanze shule, na natamani mwanangu arudi Dar asome shule nzuri na ya kisasa.

Mzazi mwenzangu anadai hawezi kuruhusu hilo, ni afadhali mtoto abaki kijijini asome shule za kawaida (serikali). Nikamwambia utamsomesha wewe huko, mimi nilitaka aje Dar asome shule nzuri na tofauti na hapo sitahusika na maswala ya shule endapo atasoma tofauti na nilivyotaka.

Nadhani labda bado anachuki au kinyongo dhidi ya familia yangu, lakini hajui Elimu bora ina faida kwa mtoto na maisha yake ya baadaye, sio mimi wala yeye.

Je ni sahihi nikikataa kutoa huduma za shule endapo atasoma kijijini? Kwani lengo langu lilikuwa aje asome Dar, akae na Bibi yake (Mama yangu) na yupo tayari kwa hilo.
 
Tatizo hapo si yeye kutopenda elimu bora kwa mtoto. Shida iko katika mahusiano yenu. Lifanyieni kazi hilo kwanza.

Anajua ukimsomesha wewe ni sawa na kumpoka mwanaye (au mwanao?!), na pengine asimpate tena kamwe. Anapiga hesabu kali za kalkyulasi yule! Ohoooo!
 
Kwanini mmetengana nazani tatizo lipo hapa nyinyi sio kitu kimoja mmetengana alafu mme zaa lazima kuwe na vuta nikuvute hapo na sio kwamba mwenzako hqtaki mtoto apate elimu bora
Sababu ya kutengana ni makosa aliyofanya yeye, anayajua na kweli alikosea sana....

Lakini hatakama bado anachuki, lazima atambue lengo ni kwa faida ya mtoto wala sio mimi wala yeye.
 
Habarini ndugu

Mimi na mzazi mwenzangu bado hatuna ndoa, ila tumebahatika kupata mtoto mmoja, kwa sasa wamerudi mkoani baada ya kuja na kukaa nyumbani kwetu kwa lengo la kumleta mtoto familia yangu imtambue.

Baada ya mtoto kufikisha miaka mitatu na nusu, nikamwambia mama yake itabidi mtoto aanze shule, na natamani mwanangu arudi Dar asome shule nzuri na ya kisasa.

Mzazi mwenzangu anadai hawezi kuruhusu hilo, ni afadhali mtoto abaki kijijini asome shule za kawaida (serikali). Nikamwambia utamsomesha wewe huko, mimi nilitaka aje Dar asome shule nzuri na tofauti na hapo sitahusika na maswala ya shule endapo atasoma tofauti na nilivyotaka.

Nadhani labda bado anachuki au kinyongo dhidi ya familia yangu, lakini hajui Elimu bora ina faida kwa mtoto na maisha yake ya baadaye, sio mimi wala yeye.

Je ni sahihi nikikataa kutoa huduma za shule endapo atasoma kijijini? Kwani lengo langu lilikuwa aje asome Dar, akae na Bibi yake (Mama yangu) na yupo tayari kwa hilo.

pia soma: Mzazi wangu hajaridhika na mchumba wangu, hajasema lakini nimeona ishara
Ukishaanza kuwa na habari za mzazi mwenzako yuko na mtoto hamuishi panoja ushafeli malezi ya mtoto tayari.

Huyo mtoto ushamuweka katika disadvantage ya kutoishi na baba yake hata akienda shule nzuri.

Vijana jiepusheni na hali hii.
 
Tatizo hapo si yeye kutopenda elimu bora kwa mtoto. Shida iko katika mahusiano yenu. Lifanyieni kazi hilo kwanza.

Anajua ukimsomesha wewe ni sawa na kumpoka mwanaye (au mwanao?!), na pengine asimpate tena kamwe. Anapiga hesabu kali za kalkyulasi yule! Ohoooo!
Hatuna tena mahusiano, kila mtu anafanya mambo yake lakini bado huduma natoa, na shule ni jukumu langu ila kama akikataa atamsomesha yeye.
 
Ukishaanza kuwa na habari za mzazi mwenzako yuko na mtoto hamuishi oanoja ushafeli malezi ya mtoto tayari.

Huyo mtoto ushamuweka katika disadvantage ya kutoishi na baba yake hata akienda shule nzuri.

Vijana jiepusheni na hali hii.
Natambua tayari hawezi kuishi na wazazi wawili, nime accept hiyo circumstance na najitahidi kuhakikisha angalau anapata elimu nzuri.

Vijana hawana haja ya kujiepusha na lolote, Sometimes maisha yana flow out of our comfort zone, tunakubali hali na kusonga mbele.
 
Hatuna tena mahusiano, kila mtu anafanya mambo yake lakini bado huduma natoa, na shule ni jukumu langu ila kama akikataa atamsomesha yeye.
Unajua maisha ya kukomoana si mazuri hata kidogo, hasa kwa watu ambao tayari mnashea kiumbe duniani.

Tumia ushawishi wako kumwelimisha, nadhani naye huenda elimu ni kiduchu au anashauriwa vibaya.

Hata angempeleka wapi, haiwezi kufuta ukweli kuhusu nani ni baba na mama mtoto. Kuna watu wana visa si haba.
 
Back to topic:
Uyo mzazi mwenzio Bado anaitaka child support yako au Bado anahitaji ukaribu na Wewe.

Ni kwamba:
ukishamchukua Mtoto mikononi mwake, mirija ya pesa toka KWAKO itakua imekata rasmi na mawasiliano baina yenu yatakua yamekufa rasmi.
Mimi nitaongea na Baba yake, najua yule mzee ni mtu anayependa Elimu, nitamwambia kama wakikataa nimsomeshe mtoto, basi watamsomesha wao.
 
Habarini ndugu

Mimi na mzazi mwenzangu bado hatuna ndoa, ila tumebahatika kupata mtoto mmoja, kwa sasa wamerudi mkoani baada ya kuja na kukaa nyumbani kwetu kwa lengo la kumleta mtoto familia yangu imtambue.

Baada ya mtoto kufikisha miaka mitatu na nusu, nikamwambia mama yake itabidi mtoto aanze shule, na natamani mwanangu arudi Dar asome shule nzuri na ya kisasa.

Mzazi mwenzangu anadai hawezi kuruhusu hilo, ni afadhali mtoto abaki kijijini asome shule za kawaida (serikali). Nikamwambia utamsomesha wewe huko, mimi nilitaka aje Dar asome shule nzuri na tofauti na hapo sitahusika na maswala ya shule endapo atasoma tofauti na nilivyotaka.

Nadhani labda bado anachuki au kinyongo dhidi ya familia yangu, lakini hajui Elimu bora ina faida kwa mtoto na maisha yake ya baadaye, sio mimi wala yeye.

Je ni sahihi nikikataa kutoa huduma za shule endapo atasoma kijijini? Kwani lengo langu lilikuwa aje asome Dar, akae na Bibi yake (Mama yangu) na yupo tayari kwa hilo.

pia soma: Mzazi wangu hajaridhika na mchumba wangu, hajasema lakini nimeona ishara
Kwani si mna familia huku jukwaani kwanini mwanaume ana maliza changamoto zake mwenyewe!
 
Back to topic:
Uyo mzazi mwenzio Bado anaitaka child support yako au Bado anahitaji ukaribu na Wewe.

Ni kwamba:
ukishamchukua Mtoto mikononi mwake, mirija ya pesa toka KWAKO itakua imekata rasmi na mawasiliano baina yenu yatakua yamekufa rasmi.
Unamshauri au unamwamurisha? Unawezaje kusema hivyo wakati yeye ni baba halali wa mtoto? You're better than this.
 
Habarini ndugu

Mimi na mzazi mwenzangu bado hatuna ndoa, ila tumebahatika kupata mtoto mmoja, kwa sasa wamerudi mkoani baada ya kuja na kukaa nyumbani kwetu kwa lengo la kumleta mtoto familia yangu imtambue.

Baada ya mtoto kufikisha miaka mitatu na nusu, nikamwambia mama yake itabidi mtoto aanze shule, na natamani mwanangu arudi Dar asome shule nzuri na ya kisasa.

Mzazi mwenzangu anadai hawezi kuruhusu hilo, ni afadhali mtoto abaki kijijini asome shule za kawaida (serikali). Nikamwambia utamsomesha wewe huko, mimi nilitaka aje Dar asome shule nzuri na tofauti na hapo sitahusika na maswala ya shule endapo atasoma tofauti na nilivyotaka.

Nadhani labda bado anachuki au kinyongo dhidi ya familia yangu, lakini hajui Elimu bora ina faida kwa mtoto na maisha yake ya baadaye, sio mimi wala yeye.

Je ni sahihi nikikataa kutoa huduma za shule endapo atasoma kijijini? Kwani lengo langu lilikuwa aje asome Dar, akae na Bibi yake (Mama yangu) na yupo tayari kwa hilo.

pia soma: Mzazi wangu hajaridhika na mchumba wangu, hajasema lakini nimeona ishara
Kwanza naww unamatatizo , samahan kwa hilo kwan majukumu yako kama baba huyajui kwa mtoto wako kwahiyo umeona uje huku uombe ushaur kuwa ukikataa itakuaje?? be humble lea mwanao Acha kuomba ushaur
 
Unajua maisha ya kukomoana si mazuri hata kidogo, hasa kwa watu ambao tayari mnashea kiumbe duniani.

Tumia ushawishi wako kumwelimisha, nadhani naye huenda elimu ni kiduchu au anashauri vibaya.

Hata angempeleka wapi, haiwezi kufuta ukweli kuhusu nani ni baba na mama mtoto. Kuna watu wana visa si haba.
Sio kwamba namkomoa, hata yeye ana elimu kiasi, lakini bado ana chuki kwanini sijamuoa, na mimi siwezi kuoa mwanamke mshirikina.
 
Back
Top Bottom