Mwanza wamebaki na milima yenye mawe, Dhahabu, Geita, Kwa jicho la ndani, Kufurahia kuzaliwa mkoa mpya Geita,ni maumivu kwa jiji la Mwanza!

Bulelaa

JF-Expert Member
Jun 28, 2024
589
1,414
Kuna jambo ambalo ni mhimu na turufu kubwa sana katika nyanja ya kiuchumi, ni pamoja na kuwa na wanasiasa wenye ushawishi mkubwa, Arusha ilishajiweka vizuri sana kwenye eneo hili, Arusha inaongoza kwa kutoa Mawaziri wakuu nchini, hii ni nzuri kwao katika kuishawishi serikali kupeleka maendeleo huko, lakini jambo lingine ni kwamba, Arusha imekuwa na wanasiasa wanaojali kwao, tofauti kabisa na ilivyo mikoa mingine kama Mwanza, Mbeya na kwingineko, Tunapokuwa tunasema, Nchi inahitaji viongozi wasomi wenye, ushawishi na wenye uchungu na maendeleo, muwe mnatuelewa, mfano mdogo, wanasiasa wa Mwanza, ni wanasiasa wanaosubiri mipango ya serikali tu tofauti na wanasiasa wa maeneo mengine ambao licha kwamba kuna mipango ya serikali, lakini bado wanakuwa ni wepesi wa kuishawishi serikali ili iingize mipango inayotokana na nguvu ya ushawishi na iliyosahaulika katika kupanua wigo wa naendelea katika eneo husika

Wanasiasa, ni kiungo mhimu sana katika kushawishi serikali ili ipelekee maendeleo, Yaani utakuta jiji la mwanza, licha ya kuwa na ukaribu wa ziwa Victoria, kuna maeneo hayana maji! Huu ni uzembe wa viongozi na siyo serikali, maji hayo hayo ya Victoria yamefika Dodoma ilihali yanapoanzia, hayajaenezwa, Wana Mwanza, timueni wote wabunge mlionao, hao ndiyo wanaochangia Mwanza iwe ya hovyo

Ikumbukwe, Jiji la Mwanza, na Jiji la Arusha, watu wake wanakawaida ya kushindana kimaendeleo, jambo ambalo ni la kuigwa, ni zuri na linafaa, hii inamaanisha kwamba, hamuwezi kuwa mnachagua viongozi legelege ili hali mnapenda jiji lenu liwe juu

Sifahamu agenda ya mkoa wa Mwanza kukatwa na kuzaliwa Geita ilitoka kwa nani, usikute pia ni siasa na ushawishi wa mkoa shindani wenu waliwazidi mbinu, bila kufahamu madhala ya badaye, mkaona ni sawa tu, Mwanza kijiografia ni ndogo kuliko Tabora, Dodoma, Morogoro n.k, lakini mikoa hiyo haikugawanywa mpaka leo

Hii maana yake nini,??

Nikirudi kwenye mada

Mkoa wa mwanza, kwa siku za usoni, utapitwa na kila mkoa kiuchumi kwa sababu mapato mengi ambayo yalikuwa yakiuinua mkoa huo na kushika nafasi ya pili kitaifa katika kuliingizia Taifa mapato yake, mengi yapo katika mkoa mpya wa Geita iliyokuwa wilaya ya Mkoa huo

Sioni ajabu mkoa wa Mwanza kwa sasa kushushwa nafasi yake na mikoa kama Njombe, Kilimanjaro, Arusha n.k kwa sababu imebaki na sifa moja tu ya milima milima yenye mawe

Ukija kwenye Ziwa, hata Geita ziwa lipo, na hata hivyo, Ziwa hili kwa nyakati tofauti limekuwa likiendeshwa kisiasa tupu

Wana Mwanza kufurahia kuzalisha mkoa mpya wa Geita huku wakisahau sehemu kubwa ya maeneo yote ya mkoa wa Mwanza, haina resources zozote zaidi ya ziwa ambalo nalo samaki zilishapungua, kunaifanya Mwanza iwe ni mji usiochangamka mbeleni

Ingawa kwa upande mwingine kwa serikali ni kusogeza huduma na miundombini kwa haraka kwa wananchi katika mikoa mipya, hata hivyo, Ukweli unapembuka kwamba, mwisho wa tambo za wana Mwanza kuwa ndilo jiji ambalo huchangia pakubwa zaidi kimapato ya serikali umewadia
 
Ukweli ndio huo

Mkoa wa mwanza, kwa siku za usoni, utapitwa na kila mkoa kiuchumi kwa sababu mapato mengi ambayo yalikuwa yakiuinua mkoa huo na kushika nafasi ya pili kitaifa katika kuliingizia Taifa mapato yake, mengi yapo katika mkoa mpya wa Geita iliyokuwa wilaya ya Mkoa huo

Sioni ajabu mkoa wa Mwanza kwa sasa kushushwa nafasi yake na mikoa kama Njombe, Kilimanjaro, Arusha n.k kwa sababu imebaki na sifa moja tu ya milima milima yenye mawe

Ukija kwenye Ziwa, hata Geita ziwa lipo, na hata hivyo, Ziwa hili kwa nyakati tofauti limekuwa likiendeshwa kisiasa tupu

Wana Mwanza kufurahia kuzalisha mkoa mpya wa Geita huku wakisahau sehemu kubwa ya maeneo yote ya mkoa wa Mwanza, haina resources zozote zaidi ya ziwa ambalo nalo samaki zilishapungua

Ingawa kwa upande mwingine kwa serikali ni kusogeza huduma na miundombini kwa haraka kwa wananchi katika mikoa mipya, hata hivyo, Ukweli unapembuka kwamba, mwisho wa tambo za wana Mwanza kuwa ndilo jiji ambalo huchangia pakubwa zaidi kimapato ya serikali umewadia
Tufute utaratibu wa mikoa uliopo hivi sasa badala yake tuanzishe utaratibu Mpya wa Serikali za Majimbo ili kuifanya miji yetu kuendelea kwa kasi ya haraka zaidi.
 
Pamoja na kuwa serikali iliyopo madarakani imeisahau mwanza katika miji iliyoipa vipaumbele lakini mtoa mada tukutoe wasiwasi mwanza kuitoa kwenye hiyo rank ya miji inayoendelea ni kazi kubwa sana.

Pamoja na mwanza kuachwa na serikali lakin bado inawaumiza vichwa
UKifuatilia mji wa mwanza wala mapato yake hayapatikan kupitia chanzo kimoja,kaangalie mwingiliano uliopo kati ya mwanza na mikoa ya jirani pamoja na nchi za jirani ndio utajua kuwa dhahabu haikuwa chanzo pekeake.
Kuifananisha mwanza na njombe ni utovu wa nidhamu.
 
Mnaandika hapa sijui mmefika huko au...
Juzi nilikuwa mikoa ya kanda ya ziwa...
Huduma nyingi unapata mwanza,
Spare nyingi tuliambiwa mpk mwanza..
Wafanyabiashara mizigo wanachukua mwanza..
Garage yenyewe tulkuwa tunarud mwanza...
Hospital kubwa...
Huko Geita niliona kikubwa walichojaaliwa ni vumbi tu
 
Mzazi mzuri siku zote ufuraia maendeleo ya mwanae hasa pale anapomzidi kimaendeleo.
😅😅

Hivi unajua Kasikazini na Kanda ziwa ni maeneo ambapo watu wake wanapenda ushindani wa kimaendeleo chief

Kitu ambacho si kibaya hata kidogo, shida inakuja pale Mikoa ya Kasikazini inapowazidi hawa watu wa kanda ya nyonyo kwa mambo ambayo wao walikuwa wanawapita kwa hatua hasa katika kuliingizia pato kubwa Taifa letu?
 
😅😅

Hivi unajua Kasikazini na Kanda ziwa ni maeneo ambapo watu wake wanapenda ushindani wa kimaendeleo chief

Kitu ambacho si kibaya hata kidogo, shida inakuja pale Mikoa ya Kasikazini inapowazidi hawa watu wa kanda ya nyonyo kwa mambo ambayo wao walikuwa wanawapita kwa hatua hasa katika kuliingizia pato kubwa Taifa letu?
Kaskazini wanabebwa na Utalii jombaa.
 
Mwanza ni mkoa unaotoa huduma kwa mikoa yote ya kanda ya ziwa kwamba huduma nying zinapatikana kwa urahisi iwe kibiashara, burudani zinapatikana pale kusema mkoa utasinyaa kiuchumi sidhani kama uko sahihi pale kuna mwingiliano wa biashara nyingi na hata watu wa mikoa mingine kanda ya ziwa matumizi yao hupenda kwenda kuyafanyia Mwanza.
 
Wewe unaijua Mwanza au unaongea tu..yaani Geita sijui Njombe zije ziipite Mwanza? ukiwa unaandika usiwe na haraka.

Mwanza ni ndoto ya kila mwanakanda ile kufika kwenye lile jiji, Mwanza haitegemei madini mjomba lile ni jiji la kibiashara acha chuki za ajabu.

Hiyo Geita imekuwa mkoa takea lini mbona haijaipita..halafu Mwanza kuanzia mwakani mgodi mkubwa wa dhahabu hapa TZ wa Nyanzaga unaanza uzalishaji sijui itakuaje.
 
Back
Top Bottom