Kwema Wakuu?
Niko mahali hapa nasikia taarifa zisizo njema kuhusu huyu Mzee, zina ukweli wowote?
=====
Mwanamuziki mkongwe wa muziki wa dansi nchini Boniface Kikumbi Mwanza Mpango maarufu King Kikii amefariki dunia.
Amefariki Dunia Usiku wa kuamkia leo katika Hospital ya Taifa ya Muhimbili ambako alikuwa amelazwa.
Mwanamuziki King Kiki Alikuwa Kwa Muda Mrefu akisumbuliwa na Maradhi Mara Kwa Mara
Bwana Ametoa, Bwana Ametwaa Jina Lake Lihimidiwe, Amen
Chanzo Cha Habari:TBC RADIO
Hapa chini ni baadhi ya kazi zake.
King Kikii
Kikumbi Mwanza Mpango, maarufu kwa jina la King Kiki au Bwana Mukubwa, aliingia nchini akitokea Zaire (DRC) mwanzoni mwa miaka ya 1970 akiwa na Orchestra Fouvette na tangu wakati huo amekuwa mkuzi, mwalimu na mlezi wa vipaji vingi vya muziki.
Kiki alizaliwa Januari 1, 1947, Lubumbashi, DRC.
King ni mtoto wa tano kwa Katambo Wabando Paulino na mama yake Mwanza Jumban,” anasema Kiki.
Akiwa shuleni, darasa la tano, Kiki na wenzake watatu walianzisha kikundi cha muziki wa dansi; wakiimba na kucheza kiasi cha kukubaliwa na uongozi wa shule na kualikwa katika kila sherehe shuleni kwao.
Sifa zao zikazagaa mitaani hasa kutokana na umri wao na ukubwa wa ‘kazi’ waliyokuwa wakiifanya.
Akiwa na umri wa miaka sita tu, Kiki alibahatika kuhudhuria onyesho la mkongwe wa muziki wa Afrika Kusini, Miriam Makeba, na kwa hakika mama huyu ndiye aliyemvutia kuupenda muziki.
Akiwa bado masomoni, mwaka 1958 alianzisha kikundi cha Bantu Negro kilichoubadili muziki wa Afrika Kusini kuwa muziki wa rhumba.
Aliachana na masomo mwaka 1962 na kujiunga na Norvella Jazz, bendi iliyomfikisha Kasai (Mbudji Mai) na kupaunua uzoefu wake kwa kukutana na wanamuziki mahiri kutoka Kinshasa.
Hata hivyo, wazazi wake hawakupenda awe mwanamuziki, hivyo kuwa kizingiti kikubwa katika safari yake ya sanaa.
Kiki na mwanamuziki mwingine maarufu nchini, Fred Ndala Kasheba, walikutana kwa mara ya kwanza huko Katanga, DRC mwaka 1968 katika bendi ya Orchestra Fouvette.
Ni bendi hiyo ndiyo iliyowaleta wakubwa hao nchini kwa mara ya kwanza miaka ya 1970 mwanzoni.
Kiki alihamia rasmi Tanzania mwaka 1977 baada ya kufuatwa na Chibangu Katayi ‘Mzee Paul’ na kujiunga na bendi ya Maquis du Zaire ya jijini Dar es Salaam.
Kutoka DRC, Kiki aliongozana na Nkashama Kanku Kelly, Mutombo Sozy na mpiga besi gitaa maarufu wa Maquis, Ilunga Banza ‘Mchafu’; bila kumsahau mnenguaji, Ngalula Tshiandanda.
Kiki ndiye muasisi wa mtindo maarufu wa Kamanyola ulioacha urithi wa jina la kituo kimojawapo cha daladala katika Barabara ya Shekilango, Sinza.
‘Kamanyola bila jasho’, kwamba unacheza kwa kujidai,”
Miongoni mwa vibao maarufu vilivyotungwa na King Kiki ni ‘Nimepigwa Ngwala’, ‘Kiongo’, ‘Kyembe’, ‘Sababu ya Nini’ na ‘Krisimasi Bonane’.
Wanamuziki alioshirikiana nao wakati huo ni akina Mbuya Makonga ‘Adios’, Mutombo Lufungula ‘Audax’, Mukumbule Lolembo ‘Parashi’, Kasongo Mpinda ‘Clyton’, Mbombo wa Mbomboka, Tshimanga Kalala Assosa, Kiniki Kieto, Masiya Radi ‘Dikuba Kuba’, Issa Nundu na Tabia Mwanjelwa.
Baadaye Kiki akajiunga na Orchestra Safari Sound (OSS) iliyokuwa na makao yake Kimara Resort na kukutana na akina Skassy Kasambula, Monga Stani Liki, Mobali Jumbe, Kalala Mbwembwe, Tshibanda Sony na Kabeya Badu.
Huko akaibuka na mtindo wa ‘Masantula Ngoma ya Mpwita’ na kushiriki kuimba na kutunga nyimbo kama ‘Mimi Msafiri’, ‘Mama Kabibi’ na nyingine nyingi, kabla ya kuanzisha bendi yake ya King Kiki Double O, iliyokuwa ikitumia mtindo wa ‘Embalasasa’.
Mwaka 1994 akaungana na Kasheba kuunda bendi ya Zaita Musica iliyopata umaarufu kwa wimbo wa ‘Kesi ya Kanga’ na ni hapo ndipo mtindo wa ‘Kitambaa Cheupe’ ulipozaliwa.
Mtindo huu uliipa umaarufu mkubwa bendi ya La Capitale (Wazee Sugu) aliyoiunda mwaka 2003, baada ya kifo cha Kasheba.
Mwaka 1997, Kiki alipata uraia wa Tanzania baada ya kuishi nchini kwa miaka mingi.
Bwana Mukubwa Kikumbi Mwanza Mpango ‘King Kiki’ ni baba wa watoto kadhaa, huku binti mmoja pekee ndiye aliyefuata nyayo zake.
Mwandishi wa makala hii anapatikana kwa simu namba: 0784331200,
Niko mahali hapa nasikia taarifa zisizo njema kuhusu huyu Mzee, zina ukweli wowote?
=====
Mwanamuziki mkongwe wa muziki wa dansi nchini Boniface Kikumbi Mwanza Mpango maarufu King Kikii amefariki dunia.
Amefariki Dunia Usiku wa kuamkia leo katika Hospital ya Taifa ya Muhimbili ambako alikuwa amelazwa.
Mwanamuziki King Kiki Alikuwa Kwa Muda Mrefu akisumbuliwa na Maradhi Mara Kwa Mara
Bwana Ametoa, Bwana Ametwaa Jina Lake Lihimidiwe, Amen
Chanzo Cha Habari:TBC RADIO
Hapa chini ni baadhi ya kazi zake.
Your browser is not able to display this video.
Your browser is not able to display this video.
King Kikii
Kikumbi Mwanza Mpango, maarufu kwa jina la King Kiki au Bwana Mukubwa, aliingia nchini akitokea Zaire (DRC) mwanzoni mwa miaka ya 1970 akiwa na Orchestra Fouvette na tangu wakati huo amekuwa mkuzi, mwalimu na mlezi wa vipaji vingi vya muziki.
Kiki alizaliwa Januari 1, 1947, Lubumbashi, DRC.
King ni mtoto wa tano kwa Katambo Wabando Paulino na mama yake Mwanza Jumban,” anasema Kiki.
Akiwa shuleni, darasa la tano, Kiki na wenzake watatu walianzisha kikundi cha muziki wa dansi; wakiimba na kucheza kiasi cha kukubaliwa na uongozi wa shule na kualikwa katika kila sherehe shuleni kwao.
Sifa zao zikazagaa mitaani hasa kutokana na umri wao na ukubwa wa ‘kazi’ waliyokuwa wakiifanya.
Akiwa na umri wa miaka sita tu, Kiki alibahatika kuhudhuria onyesho la mkongwe wa muziki wa Afrika Kusini, Miriam Makeba, na kwa hakika mama huyu ndiye aliyemvutia kuupenda muziki.
Akiwa bado masomoni, mwaka 1958 alianzisha kikundi cha Bantu Negro kilichoubadili muziki wa Afrika Kusini kuwa muziki wa rhumba.
Aliachana na masomo mwaka 1962 na kujiunga na Norvella Jazz, bendi iliyomfikisha Kasai (Mbudji Mai) na kupaunua uzoefu wake kwa kukutana na wanamuziki mahiri kutoka Kinshasa.
Hata hivyo, wazazi wake hawakupenda awe mwanamuziki, hivyo kuwa kizingiti kikubwa katika safari yake ya sanaa.
Kiki na mwanamuziki mwingine maarufu nchini, Fred Ndala Kasheba, walikutana kwa mara ya kwanza huko Katanga, DRC mwaka 1968 katika bendi ya Orchestra Fouvette.
Ni bendi hiyo ndiyo iliyowaleta wakubwa hao nchini kwa mara ya kwanza miaka ya 1970 mwanzoni.
Kiki alihamia rasmi Tanzania mwaka 1977 baada ya kufuatwa na Chibangu Katayi ‘Mzee Paul’ na kujiunga na bendi ya Maquis du Zaire ya jijini Dar es Salaam.
Kutoka DRC, Kiki aliongozana na Nkashama Kanku Kelly, Mutombo Sozy na mpiga besi gitaa maarufu wa Maquis, Ilunga Banza ‘Mchafu’; bila kumsahau mnenguaji, Ngalula Tshiandanda.
Kiki ndiye muasisi wa mtindo maarufu wa Kamanyola ulioacha urithi wa jina la kituo kimojawapo cha daladala katika Barabara ya Shekilango, Sinza.
‘Kamanyola bila jasho’, kwamba unacheza kwa kujidai,”
Miongoni mwa vibao maarufu vilivyotungwa na King Kiki ni ‘Nimepigwa Ngwala’, ‘Kiongo’, ‘Kyembe’, ‘Sababu ya Nini’ na ‘Krisimasi Bonane’.
Wanamuziki alioshirikiana nao wakati huo ni akina Mbuya Makonga ‘Adios’, Mutombo Lufungula ‘Audax’, Mukumbule Lolembo ‘Parashi’, Kasongo Mpinda ‘Clyton’, Mbombo wa Mbomboka, Tshimanga Kalala Assosa, Kiniki Kieto, Masiya Radi ‘Dikuba Kuba’, Issa Nundu na Tabia Mwanjelwa.
Baadaye Kiki akajiunga na Orchestra Safari Sound (OSS) iliyokuwa na makao yake Kimara Resort na kukutana na akina Skassy Kasambula, Monga Stani Liki, Mobali Jumbe, Kalala Mbwembwe, Tshibanda Sony na Kabeya Badu.
Huko akaibuka na mtindo wa ‘Masantula Ngoma ya Mpwita’ na kushiriki kuimba na kutunga nyimbo kama ‘Mimi Msafiri’, ‘Mama Kabibi’ na nyingine nyingi, kabla ya kuanzisha bendi yake ya King Kiki Double O, iliyokuwa ikitumia mtindo wa ‘Embalasasa’.
Mwaka 1994 akaungana na Kasheba kuunda bendi ya Zaita Musica iliyopata umaarufu kwa wimbo wa ‘Kesi ya Kanga’ na ni hapo ndipo mtindo wa ‘Kitambaa Cheupe’ ulipozaliwa.
Mtindo huu uliipa umaarufu mkubwa bendi ya La Capitale (Wazee Sugu) aliyoiunda mwaka 2003, baada ya kifo cha Kasheba.
Mwaka 1997, Kiki alipata uraia wa Tanzania baada ya kuishi nchini kwa miaka mingi.
Bwana Mukubwa Kikumbi Mwanza Mpango ‘King Kiki’ ni baba wa watoto kadhaa, huku binti mmoja pekee ndiye aliyefuata nyayo zake.
Mwandishi wa makala hii anapatikana kwa simu namba: 0784331200,