MWAMPOSA: Unforgettable overnight tutumalizana na HIV, Nuksi, Mikosi, Mabalaa, Siasa na kama kila unachokifanya hakifanikiwi Kawe inakuhusu

CM 1774858

JF-Expert Member
May 29, 2021
5,307
4,617
Nitumie jukwaa hili kuwaalika na kuwakaribisha kwenye mkesha mkubwa ambao wewe na jamaa yako hamtausahau kwenye maisha yenu yote kama anavyosema Apostle Boniface Godwin Mwamposa wa huduma ya maombi na maombezi ya Arise & Shine Kawe jijini Dar es salaam Tanzania.

Bila kujali dini yako fanya haya ;-

1. Kama unaumwa ugonjwa wowote ule hata kama madaktari Wamesema hautapona au ndugu yako anaumwa njoo na picha yake au njoo wewe uandike jina lake na ufute hiyo kesi utanishukuru.

2. Kama timu yako ya Mpira au wewe mwenyewe hauna bahati ya kufunga Magori kama Kibu Denis wa Simba njooni Ijumaa tukeshe Kawe.

3. Kama wewe ni bondia na unapigwa Kila shindano kama Dula Mbabe njoo na gloves zako tukeshe utanishukuru.

4. Kama wewe ni mwanafunzi na unafeli Kila mtihani njoo wewe au mzazi wako na matokeo yako tukeshe.

5. Kama ndoa au uchumba unazingua wenzako wote wameolewa wewe bado mchumba njoo tukeshe utanishukuru.

6. Kama huelewi elewi tu mambo yanayokupata au kutokea njoo tukeshe,

7. Kama unajenga nyumba haumalizi njoo na udongo wa hilo eneo tukeshe,

8. Kama unafanya Biashara na hupati wateja njoo na udongo wa eneo lako la biashara,

9. Kama unaboda na hupati wateja njoo na kadi ya pikipiki au funguo tukeshe.

9. Kama huna kazi au umefukuzwa kazi njoo na jina la mwajiri na nyaraka kama chetu au zozote tukeshe.

10. Kama unataka kwenda nje ya nchi njoo na jina la hiyo nchi.

11. Kama unataka kuwa tajiri njoo uandike level ya utajiri unayoitaka kama ni milionea, bilionea etc

12. Kama unataka kibali kwenye sanaa njoo tukeshe

13. Kama unataka waliokuloga wafe wote njoo tukeshe.

14. Kama unataka urudishiwe ulivyopoteza njoo na majina ya hivyo vitu vilivyopotea hata kama ni miaka 20.

15. Kama unataka kwenda Mbinguni ukiwa unatabasamu njoo tukeshe na Mtume Boniface Bulldozer Mwamposa.

16. Nakama unajambo lolote ambalo sijalitaja hapa Mungu atalifanya chini ya Mtumishi wake Mwaminifu Mwamposa.

17. Kama huamini pia njoo ufanye ku-test tu kama ni kweli utanishukuru Mimi kukupa hii taarifa.

Ni mimi na ni mimi tu kuwaleteeni taarifa hii ya Ukombozi wenu na watoto wenu na watoto wa watoto wenu na Mimi basi nitendewe kama alivyonena Mtumishi wa Mungu kuhusu kupeleka habari hii njema ya Ukombozi -Amen
#Nawewe sambaza taarifa hii kwa watu 12 utaona matokeo hata kabla ya mkesha huu.
IMG-20240630-WA0107.jpg

 
Bila shaka Watu watabubujikwa sana machozi ya furaha kwa kupata majibu ya maswali yao katika maisha yao yaliyoandamwa na changamoto mbalimbali.Nawasihi watu wanende wakakutane na mkono hodari wa Mungu wa Ibrahim ,ISaka na Yakobo.
Kaka wakenya wanajiita gen z wanaleta fujo huko Kenya Sisi gen Z wa Tanzania tunafuraha Sana mpaka tunabubujikwa na machozi na kugaragara mama Samia akiendelea kumwaga ajira za kutosha hakuna kijana asiekua na ajira Tanzania hii Nani kama Mama
 
Back
Top Bottom