Tetesi: MutliChoice yamteua Mwangaza Mollel kuwa Mkurugenzi mpya Maisha Magic Bongo, DSTV

Nifah

JF-Expert Member
Feb 12, 2014
32,746
71,978
Kama mnakumbuka vyema, Novemba ya mwaka jana niliwaletea hapa taarifa kuhusiana na aliyekuwa Mkurugenzi wa vipindi Maisha Magic Bongo, Barbara Kambogi kusimamishwa kazi kwa tuhuma zilizowasilishwa makao makuu ya DSTV Afrika ya Kusini na mtayarishaji wa tamthilia za Kiswahili Bwana Isike Samwel.

Baada ya tuhuma hizo zenye ushahidi usio na shaka, DSTV walimsimamisha kazi Barbara Kambogi na msaidizi wake kupisha uchunguzi na hivi sasa umefanyika uteuzi wa Mkurugenzi mpya, Bibie Mwangaza Mollel.

CV yake huko DSTV imeshiba kwelikweli!
Kwa taarifa za kiutendaji imefahamika kwamba uteuzi huu ni makini. Mwangaza amefanya kazi DSTV kwa kipindi kisichopungua miaka 10!

Alianza kufanya kazi kitengo cha huduma kwa wateja kuanzia mwaka 2014 alikohudumu kwa miaka 7, kisha akahamishiwa kitengo cha masoko na baadaye akawa mwendeshaji wa ofisi ya DSTV hadi alipoukwaa Ukurugenzi wa kitengo cha tamthilia za Kiswahili hivi karibuni.

Ni mchapakazi hodari!
Mwangaza anafahamika kwa uchapaji kazi wake usio na mashaka. Hilo linadhihirika kwa tuzo aliyopokea mwaka juzi kwenye kitengo hichohicho cha tamthilia za Kiswahili.

IMG_5592.jpeg


Hongera Mwangaza, matumaini yetu tulio wengi ni juu yako kuona ukifanya tofauti na wenzio Barbara pamoja na msaidizi wake waliogeuka Miungu watu katika kitengo hichohicho ulichoteuliwa.
Kila la kheri

Mwangaza Evarest Mollel pichani…
IMG_5589.jpeg


Hii ni taarifa mpya, DSTV watatangaza kuhusu uteuzi huo hivi karibuni.

Chanzo changu nyeti, nami ndiye
Nifah.
 
Ahakikishe Huba na Juakali zinafika mwisho sasa ili kupisha tamthilia nyingine.
Mkuu nimecheka sana. Mkurugenzi aliyepita alikuwa na 'percent' yake kwenye hizo tamthilia ndio maana zimegeuka Isidingo.

Barbara alifanya mengi ya hovyo, alivuka hadi mipaka kwa kuuza haki za tamthilia za Kiswahili kwa Wakenya ambao ndio waandaaji wa tamthilia mpya ya Jiya.
 
Mkuu nimecheka sana. Mkurugenzi aliyepita alikuwa na 'percent' yake kwenye hizo tamthilia ndio maana zimegeuka Isidingo.

Barbara alifanya mengi ya hovyo, alivuka hadi mipaka kwa kuuza haki za tamthilia za Kiswahili kwa Wakenya ambao ndio waandaaji wa tamthilia mpya ya Jiya.
Nakumbuka ulileta kisa cha huyo Mkurugenzi aliyepita na sarakasi alizokuwa anafanya kwenye hizo Tamthilia,
ila naimani huyu wa sasaivi ameshajua kichwa cha nyoka kikwapi kwahiyo kazi kwake tu.
 
Kama mnakumbuka vyema, Novemba ya mwaka jana niliwaletea hapa taarifa kuhusiana na aliyekuwa Mkurugenzi wa vipindi Maisha Magic Bongo, Barbara Kambogi kusimamishwa kazi kwa tuhuma zilizowasilishwa makao makuu ya DSTV Afrika ya Kusini na mtayarishaji wa tamthilia za Kiswahili Bwana Isike Samwel...
Nimependa sana pua yake
 
Back
Top Bottom