Muda sahihi wa kumuaga mtu aliyekufa ni wakati yuko hai, sio kwenye jeneza. Msimamo wangu mpya

matunduizi

JF-Expert Member
Aug 20, 2018
7,469
17,990
Mwanzoni mwa mwaka huu niliboresha mifumo yangu ya kijamii kwa kukitoa kipengere cha kumuaga marehemu mara ya mwisho kama ni kitu cha lazima kwangu. Sifanyi hicho kitu tena.

Naamini muda sahihi wa kumuaga mtu mara ya mwisho ni wakati akiwa hai, kama hutapata nafasi basi jitahidi kukumbuka mazuri yake inatosha.

Mtu akifa hajui kitu chochote. Kilio, unyenyekevu na huzuni unayoionyesha kwa maiti haimuhusu chochote muhusika wala haimuathili chochote. Vitu vivyo vinapaswa kufanyika akiwa katika hatua za mwisho.

Katika hili naungana na wayahudi na waislamu katika kutoaga kwa kuangalia sura ya maiti.

Faida ya huu utaratibu mpya kwangu, nimekuwa mwepesi sana kuwaona wagonjwa, watu wanaopitia nyakati ngumu hata kwa kupiga simu maana najua ndio muda wa thamani sana kwao maana ikitokea wamelala sinanafasi hiyo. Hivyo siwezi kuweka picha ya mtu aliyekufa status, au social media au kutembea na tshirt maana kwangu ni njia potofu ya kumkumbuka.

Natambua ni utaratibu mzuri kwa wanaoupenda ila kwa tukio la kupuuza kumuona rafiki yangu na jirani mgonjwa baada ya masaa mawili akafa na sikuwa na sababu ya msingi kutomuona nimeachana na utamaduni wa kuona maiti.


Ni hayo tu.

Mtumishi Matunduizi.
 
MTU anapokufa anakuwa umekufa mwili wa nyama Ila yeye binafsi anakuwa yupo anaedndelea ku-exist

Ukifika kuhudhuria katika nyakati zote tatu utakuwa umefanya vzr.

Akiwa mzima
Akiwa ktk nyakati zake ngumu
Akiwa tayari roho imeacha mwili.
 
NI HERI KUFA KATIKA KRISTO YESU UKIWA MTU SAFI MAANA KILA ALIE KATIKA KRISTO ANA UZIMA NDANI YAKE

(NAISUBIRIA JERUSALEM MPYA,)
Yesu mwenyewe hakumuaga Lazaro rafiki yake kipenzi. Alisubiri afe aoze ndio akaja kutoa rambirambi na pole kwa wakina Martha na Mariam. Utaratibu huu wa kuaga hasa kwa wakristo umetoka kwa tamaduni za wazungu sio biblia.

Mcha Mungu akifa ni baraka maana anapumzika akisubiri kula maisha Mbinguni, ila hasara tu kwa Mungu maana anakuwa amepungukiwa manpower.
"Heri wafu wafao katika Bwana"
 
Kwani kwenye mazishi anaenda kuagwa MTU au wanaenda kuaga/kutoa heshma za mwisho kwa MWILI wa Mtu?
Heshima qnapewa mtu aliye hai. Heshima zile ni tamaduni tu ambazo haziiathiri maiti kwa chochote. Ni suala lq maarifa tu.
 
MTU anapokufa anakuwa umekufa mwili wa nyama Ila yeye binafsi anakuwa yupo anaedndelea ku-exist

Ukifika kuhudhuria katika nyakati zote tatu utakuwa umefanya vzr.

Akiwa mzima
Akiwa ktk nyakati zake ngumu
Akiwa tayari roho imeacha mwili.
Kwa nini uage kitu ambacho kipo na kinakuona. Hapo ni sawa na kusema mtu amehamia sehemu nyingine. Wakati gani bora wa kumuaga mtu anayetaka kuhama. Wakati anahama au wakati akiwa ameshahama na ukaaga pocha zake?. Kwa kuzingatia uelewa huo wa mtu kuhama.
 
Kwa nini uage kitu ambacho kipo na kinakuona. Hapo ni sawa na kusema mtu amehamia sehemu nyingine. Wakati gani bora wa kumuaga mtu anayetaka kuhama. Wakati anahama au wakati akiwa ameshahama na ukaaga pocha zake?. Kwa kuzingatia uelewa huo wa mtu kuhama.



MTU anapkufa anakuwa yupo maana MTU ni roho na sio huo mwili wa nyama.

Japo nimekuelewa
 
Mwanzoni mwa mwaka huu niliboresha mifumo yangu ya kijamii kwa kukitoa kipengere cha kumuaga marehemu mara ya mwisho kama ni kitu cha lazima kwangu. Sifanyi hicho kitu tena.

Naamini muda sahihi wa kumuaga mtu mara ya mwisho ni wakati akiwa hai, kama hutapata nafasi basi jitahidi kukumbuka mazuri yake inatosha.

Mtu akifa hajui kitu chochote. Kilio, unyenyekevu na huzuni unayoionyesha kwa maiti haimuhusu chochote muhusika wala haimuathili chochote. Vitu vivyo vinapaswa kufanyika akiwa katika hatua za mwisho.

Katika hili naungana na wayahudi na waislamu katika kutoaga kwa kuangalia sura ya maiti.

Faida ya huu utaratibu mpya kwangu, nimekuwa mwepesi sana kuwaona wagonjwa, watu wanaopitia nyakati ngumu hata kwa kupiga simu maana najua ndio muda wa thamani sana kwao maana ikitokea wamelala sinanafasi hiyo. Hivyo siwezi kuweka picha ya mtu aliyekufa status, au social media au kutembea na tshirt maana kwangu ni njia potofu ya kumkumbuka. Natambua no utaratibu mzuri kwa wanaoupenda ila kwa tukio la kupuuza kumuona rafiki yangu na jirani mgonjwa baada ya masaa mawili akafa na sikuwa na sababu ya msingi kutomuona nimeachana na utamaduni wa kuona maiti.


Ni hayo tu.

Mtumishi Matunduizi.

Hata ukimuaga akiwa mzima, anasema mtumishi wa Mungu:

"Yote ni ubatili mtupu na kujilisha upepo."

Au anasema uongo ndugu yangu?
 
Ukweli mtupu hata hivyo tulio wengi tunajisahau sana kuwa karibu na walio na thamani kwetu.
 
Kama mtu ni roho unadhani kwa nini tuage mwili badala ya kudili na roho inayoishi

Yaani MTU anaendelea kuwepo katika spiritual realm (ulimwengu wa roho)

Hata ukiwa kuna mambo unataka akujuze unaweza kujiungajisha nae .

Kuaga mwili wa marehemu ni utaratibu uliopo tu.

Unaweza kuamua kutomuaga marehemu Ila ikakuletea shida ,familia yake wakapata shida.


Binadamu huwa hafi Ila kinachokufa ni mwili wa nyama tu.

Kama unavyosema Jesus Christ au Mungu yakobo n.k means those guys are still alive in spiritual realm.

Even ur ancestors they are still alive in spiritual realm.

Ukisikia ur mama is gone or anybody who is closed to you nenda umuage wewe hauoni kuwa anaona Ila yeye anaona.
 
Ukweli mtupu hata hivyo tulio wengi tunajisahau sana kuwa karibu na walio na thamani kwetu.
Tunakusanya nguvu kubwa kwenye kuonyesha ubora wakati mtu hayupo kuliko akiwepo.

Sisi wakriato tunaamini Yesu akija hatatuhukumu kwa wema na huzuni tulioionyesha wakati wa msiba na umati wa wapendwa wetu, bali wakati wakiwa hai.
Nilikiwa gerezani hamkuja kunionq.
Nilikuwa uchi hamkunipa nguo.
Nilikuwa mgonjwa hamkuja kunuona.
Mnapofanya hayo mnamfanyia Mungu sio muhusika.
 
Back
Top Bottom