A
Anonymous
Guest
Habari Mimi ni kijana nipo Njombe Mjini, Hivi Karibuni Halmashauri ya Mji wa Njombe ilitoa Mikopo Kwa vikundi vya wanawake,Vijana na watu wenye ulemavu zaidi ya Billion 1.8, Kikundi chetu Cha vijana tulipokea zaidi ya Milioni 30
Mchakato wa kupata mkopo wa Halmashauri huwa unapitia kwa mtendaji wa mtaa Ili apitishe na kututambua kama vijana tunaofanya shughuli za Ujasiliamali kwenye mtaa wake.
Lakini Cha kushanganza hadi naandika hapa ni kwamba Mmoja wa Watendaji wa mtaa hapa Njombe analazimisha tumpatie Milioni 10 kama Posho ya kutusaidia kupitisha mkopo Wetu. Amekuwa akiwatukana na kuwatishia viongozi wa kikundi ili wakati mwingine tusipate tena.
Kwa idadi yetu hata kama tungegawana hatuwezi kupata hata Milioni 3 kila mmoja , na hizi pesa tuliandikia mradi wa kikundi.
Sasa amesababisha Kikundi tupo Njipanda hatujui tufanye nini anatishia hadi kuturoga,tumeamua kukaa kimya na Pesa bado zipo banki na hatujua tuende kulalamika kwa nani.
Nashauri Mkurugenzi afanye uchunguzi kwa hawa watendaji wa mitaa na vijiji kwasababu wanakwamisha ndoto za vijana
Mwisho wa siku marejesho tunatakiwa kufanya sisi, tukimpatia hiyo Milioni 10 manakae hatuwezi kufanyia shughuli yoyote na hii pesa itapotea bila kufanya kazi.
Mhusika ni Mtendaji wa Mtaa mmoja upo Njombe Mjini,Naomba unisaidie kupaza Sauti ,Nimeficha jina lake Ili ujumbe huu ukimfikia aache hiyo tabia mara moja mana anahatarisha na Kazi yake.
Mchakato wa kupata mkopo wa Halmashauri huwa unapitia kwa mtendaji wa mtaa Ili apitishe na kututambua kama vijana tunaofanya shughuli za Ujasiliamali kwenye mtaa wake.
Lakini Cha kushanganza hadi naandika hapa ni kwamba Mmoja wa Watendaji wa mtaa hapa Njombe analazimisha tumpatie Milioni 10 kama Posho ya kutusaidia kupitisha mkopo Wetu. Amekuwa akiwatukana na kuwatishia viongozi wa kikundi ili wakati mwingine tusipate tena.
Kwa idadi yetu hata kama tungegawana hatuwezi kupata hata Milioni 3 kila mmoja , na hizi pesa tuliandikia mradi wa kikundi.
Sasa amesababisha Kikundi tupo Njipanda hatujui tufanye nini anatishia hadi kuturoga,tumeamua kukaa kimya na Pesa bado zipo banki na hatujua tuende kulalamika kwa nani.
Nashauri Mkurugenzi afanye uchunguzi kwa hawa watendaji wa mitaa na vijiji kwasababu wanakwamisha ndoto za vijana
Mwisho wa siku marejesho tunatakiwa kufanya sisi, tukimpatia hiyo Milioni 10 manakae hatuwezi kufanyia shughuli yoyote na hii pesa itapotea bila kufanya kazi.
Mhusika ni Mtendaji wa Mtaa mmoja upo Njombe Mjini,Naomba unisaidie kupaza Sauti ,Nimeficha jina lake Ili ujumbe huu ukimfikia aache hiyo tabia mara moja mana anahatarisha na Kazi yake.