Mtaji wa milioni 3 nifanye biashara gani? Nilikuwa nakopesha vyombo, wakopaji wasumbufu kulipa

kinywanyuku

JF-Expert Member
Jul 13, 2015
3,688
2,832
Wadau nina mtaji wa milioni 3 unatoka na kazi ya kukopesha vyombo nifanye biashara gani maana hasa hivi wakopaji wamekuwa wasumbufu hawalipi na nimefanya miaka 5. Nataka nifanye biashara nyingine usiyohusiana na mikopo. Nipo Dar Gongo la Mboto.
 
Katika huko kukopesha watu, ni kwamba ulikuwa unatembelea maeneo tofauti tofauti. Hujaona au kujifunza biashara yeyote tofauti na yako?

Je wewe unapenda nini zaidi au ulitamani kufanya nini, ukipata mtaji zaidi ya 1m. Tuanzie hapo kwanza...
 
Wadau nina mtaji wa milioni 3 unatoka na kazi ya kukopesha vyombo nifanye biashara gani maana hasa hivi wakopaji wamekuwa wasumbufu hawalipi na nimefanya miaka 5 nataka nifanye biashara nyingine usito husiana na mikopo nipo Dar gongo la mboto
Mkuu Nakushauri Uendelee kukopesha ila kwa njia tofauti, mtu akitaka laki mkopeshe yeye aweke bondi kitu chake chenye thamani zaidi. Uwe na ofisi ambapo watu watakuwa wanakupatia, Tengeneza mkataba maalumu, mtu akivusha tu muda wa kulipa uza kitu chake kwa faida kazi yako iendelee, Usikopeshe bila bondi.
 
Katika huko kukopesha watu, ni kwamba ulikuwa unatembelea maeneo tofauti tofauti. Hujaona au kujifunza biashara yeyote tofauti na yako?
Je wewe unapenda nini zaidi au ulitamani kufanya nini, ukipata mtaji zaidi ya 1m. Tuanzie hapo kwanza...
Nilitamani biashara ya kuuza sendo zile za wanaume dior au viainishi vya magari
 
Mkuu Nakushauri Uendelee kukopesha ila kwa njia tofauti, mtu akitaka laki mkopeshe yeye aweke bondi kitu chake chenye thamani zaidi. Uwe na ofisi ambapo watu watakuwa wanakupatia, Tengeneza mkataba maalumu, mtu akivusha tu muda wa kulipa uza kitu chake kwa faida kazi yako iendelee, Usikopeshe bila bondi.
Mikopo usumbufu hapana
 
Wadau nina mtaji wa milioni 3 unatoka na kazi ya kukopesha vyombo nifanye biashara gani maana hasa hivi wakopaji wamekuwa wasumbufu hawalipi na nimefanya miaka 5. Nataka nifanye biashara nyingine usiyohusiana na mikopo. Nipo Dar Gongo la Mboto.
Kalime karanga, alizeti au funga sungura ukauze Russia ukiwa serious miaka miwili inatosha kuwa millionea.

Russia kuna vita tangu 2022 demand ya vyakula ni kubwa mno anza sasa usisahau kuja kutoa ushuhuda ili vijana wengine wahamasike.
 
Wadau nina mtaji wa milioni 3 unatoka na kazi ya kukopesha vyombo nifanye biashara gani maana hasa hivi wakopaji wamekuwa wasumbufu hawalipi na nimefanya miaka 5. Nataka nifanye biashara nyingine usiyohusiana na mikopo. Nipo Dar Gongo la Mboto.
Tandika mkeka mechi ya Argentina na Canada, ipe argentina, weka stake milioni 3
 
Wadau nina mtaji wa milioni 3 unatoka na kazi ya kukopesha vyombo nifanye biashara gani maana hasa hivi wakopaji wamekuwa wasumbufu hawalipi na nimefanya miaka 5. Nataka nifanye biashara nyingine usiyohusiana na mikopo. Nipo Dar Gongo la Mboto.
Hiyo biashara ya kukopesha vyombo wanaiweza waha pekee na wamesambaa Tanzania nzima.
 
Back
Top Bottom