Uzalendo wa Kitanzania

JF-Expert Member
Mar 8, 2020
3,098
6,909
RAIS Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amesema amani na utulivu ambayo nchi nyingi duniani na bara hili wanayaona nchini ni matokeo ya msingi imara ambao umejengwa chini ya uongozi wa Baba Taifa hayati Mwalimu Julius Nyerere na kuongeza kuwa ni jukumu la kila Mtanzania kulinda na kuenzi.

Ameyasema hayo wakati akifungua Kongamano la Maadhimisho ya Kumuenzi Mwalimu Julius Nyerere chini ya kaulimbiu “Mwalimu Nyerere na Vuguvugu la Ukombozi: Tafakari Mshikamano, Uongozi, Pan-Africanism na Umoja wa Afrika”, iliyofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere ya Mjini Kibaha mkoani Pwani.

Amesema moja ya njia sahihi ya kumuenzi Muasisi wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Nyerere ni kwa kutekeleza kwa vitendo aliyoyafanya wakati wa uhai wake kuleta maendeleo katika nyanja mbalimbali hususani katika uongozi.

“Mwalimu alikuwa mtu wa aina hiyo ambaye aliishi maneno yake na alijitolea maisha yake kwa ajili ya maisha ya watu wachache”.

“Hatuwezi kuzungumza juu ya uhuru na maendeleo katika eneo hili la Afrika bila kumtaja mtu huyu ambaye bado tunayo mengi ya kujifunza. kutoka, na njia pekee ya kumtukuza ni kufanya yale aliyotufundisha wakati wa uhai wake,” alisema.

“Leo, tumekusanyika hapa, watu kutoka nchi mbalimbali kutafakari maisha ya kiongozi wetu ambaye aliuthibitishia ulimwengu kwamba binadamu wanaweza kuishi kwa kuheshimiana na kwamba Ubaguzi wa rangi, ukoloni mamboleo na aina zote za dhuluma za kijamii zinaweza kupigwa vita tu. ya watu kufanya kazi chini ya umoja na dhamira”, alieleza.

Dkt. Kikwete alisema pia tuna cha kujifunza kwa Baba wa taifa ni alikuwa mzalendo wa kweli mwenye kuamini katika misimamo yake ambayo hakukatishwa tamaa Wala kuvunjwa Moyo katika harakati za kupigania uhuru wa nchi yetu licha ya kupitia changamoto mbalimbali ikiwemo kushitakiwa, kufikishwa mahakamani na kuhukumiwa kulipa faini sambamba na kudhihakiwa na wakoloni kwa ajili ya kupigania uhuru wa nchi yetu.

#KitengeUpdates
 
RAIS Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amesema amani na utulivu ambayo nchi nyingi duniani na bara hili wanayaona nchini ni matokeo ya msingi imara ambao umejengwa chini ya uongozi wa Baba Taifa hayati Mwalimu Julius Nyerere na kuongeza kuwa ni jukumu la kila Mtanzania kulinda na kuenzi.

Ameyasema hayo wakati akifungua Kongamano la Maadhimisho ya Kumuenzi Mwalimu Julius Nyerere chini ya kaulimbiu “Mwalimu Nyerere na Vuguvugu la Ukombozi: Tafakari Mshikamano, Uongozi, Pan-Africanism na Umoja wa Afrika”, iliyofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere ya Mjini Kibaha mkoani Pwani.

Amesema moja ya njia sahihi ya kumuenzi Muasisi wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Nyerere ni kwa kutekeleza kwa vitendo aliyoyafanya wakati wa uhai wake kuleta maendeleo katika nyanja mbalimbali hususani katika uongozi.

“Mwalimu alikuwa mtu wa aina hiyo ambaye aliishi maneno yake na alijitolea maisha yake kwa ajili ya maisha ya watu wachache”.

“Hatuwezi kuzungumza juu ya uhuru na maendeleo katika eneo hili la Afrika bila kumtaja mtu huyu ambaye bado tunayo mengi ya kujifunza. kutoka, na njia pekee ya kumtukuza ni kufanya yale aliyotufundisha wakati wa uhai wake,” alisema.

“Leo, tumekusanyika hapa, watu kutoka nchi mbalimbali kutafakari maisha ya kiongozi wetu ambaye aliuthibitishia ulimwengu kwamba binadamu wanaweza kuishi kwa kuheshimiana na kwamba Ubaguzi wa rangi, ukoloni mamboleo na aina zote za dhuluma za kijamii zinaweza kupigwa vita tu. ya watu kufanya kazi chini ya umoja na dhamira”, alieleza.

Dkt. Kikwete alisema pia tuna cha kujifunza kwa Baba wa taifa ni alikuwa mzalendo wa kweli mwenye kuamini katika misimamo yake ambayo hakukatishwa tamaa Wala kuvunjwa Moyo katika harakati za kupigania uhuru wa nchi yetu licha ya kupitia changamoto mbalimbali ikiwemo kushitakiwa, kufikishwa mahakamani na kuhukumiwa kulipa faini sambamba na kudhihakiwa na wakoloni kwa ajili ya kupigania uhuru wa nchi yetu.

#KitengeUpdates

Baadhi ya mabaya au ubovu wa Mwl. Nyerere:-
1. Kuiga, Kuanzisha na kuendeleza Sera na Itikadi Mbaya kabisa ya Siasa za Ukomunisti/Ujamaa hapa Tanzania.

Huu ndio ulikuwa mwanzo wa Kujenga Msingi mbovu wa Taifa la hovyo kabisa lililopo hivi sasa.
Itikadi na Sera ya Ukomunisti/Ujamaa ikaja kushindwa vibaya Sana huku yeye mwenyewe akishuhudia kwa macho yake kushindwa kwa itikadi yake aliyoileta hapa Tanzania kutoka kwa marafiki zake wa China, Urusi na Cuba.

2. Kutengeneza Taifa la Watu waoga, Wanyonge, dhaifu wa fikra wasiojitambua na Wala wasioweza kuhoji. Taifa la watu 'misukule'.

3. Kutengeneza au kuunda nchi isiyokuwa na Mipango-miji, hususani kupitia kwenye Sera yake mbaya kabisa ya ujamaa/Ukomunisti. Sera au Itikadi hiyo ya Ujamaa/Ukomunisti ndio ilikuwa chanzo Cha Kuanzishwa kwa Azimio la Arusha na Operesheni Vijiji, the Worse Operation that completely destroyed the Country and Town Planning process within the Country.
Arusha Declaration and Operation Vijiji also led to the Death of Real Estate Industry and its development.

Kupitia Itikadi hiyo ya Ujamaa/Ukomunisti, Azimio la Arusha na Operesheni Vijiji, Watu wengi sana walinyang'anywa Ardhi zao pamoja na majumba yao waliyokuwa wakimiliki. Nyumba nyingi sana za Watu zilitaifishwa, Leo hii nyumba hizo zinamilikiwa na Shirika la Nyumba (NHC).

4. Kutuletea Katiba ya nchi ambayo ni mbaya kabisa, isiyofaa na ambayo imesababisha na inaendelea kusababisha madhara makubwa sana kwa Raia. Katiba mbaya ambayo imewatengeneza Watawala wa nchi hii kuwa 'Miungu Watu.'
 
Back
Top Bottom