Msifadhaike jamani, yote haya karibu yatakwisha

Setfree

JF-Expert Member
Dec 25, 2024
2,645
3,590
Watu wengi wamejaa fadhaa kutokana na mambo mbalimbali yanayoendelea huku na kule duniani: vita, magonjwa ya kutisha, ukosefu wa ajira, njaa, uhalifu, matetemeko, gharama kubwa za maisha, nk.

Rafiki, usifadhaike. Hayo yote karibu yatakwisha. Biblia inatuhakikishia kuwa hayo si maisha ya milele. Mungu anaumba dunia mpya isiyo na maovu, mateso wala huzuni.

“Sasa, naumba mbingu mpya na dunia mpya, mambo ya zamani hayatakumbukwa tena. Furahini, mkashangilie milele, kwa ajili ya vitu hivi ninavyoumba.."(Isaya 65:17)

Katika mbingu mpya na dunia mpya:
Hakutakuwa na machozi tena wala maombolezo au kilio. (Ufunuo 21:4)
Hakutakuwa na magonjwa wala mauti. Haki itatawala, na amani itakuwa ya kudumu.

"Lakini, kulingana na ahadi yake, twatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake."(2 Petro 3:13).

Hayo sio maneno ya kukutia moyo tu, ni ahadi za kweli kutoka kwa Mungu ambaye hasemi uongo. Kwahiyo tunapoona mambo yanazidi kuwa mabaya duniani, ni ishara kuwa mwisho wa mambo hayo umekaribia.

"Basi mambo hayo yaanzapo kutokea, changamkeni, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu umekaribia."(Luka 21:28)
 
1 Petro 4:7-14
Mwisho wa mambo yote umekaribia; basi, iweni na akili, mkeshe katika sala. Zaidi ya yote iweni na bidii kubwa katika kupendana; kwa sababu upendano husitiri wingi wa dhambi.
 
Kama umeokoka. Endelea kumtumainia Bwana. Usiache maombi, usiache kusoma Biblia. Usikate tamaa. Mwisho wa mambo yote ya kufadhaisha umekaribia, na utukufu wa milele unawangojea wale wanaomwamini Mungu na kuishi maisha matakatifu(1 Petro 4:7).
 
Watu wengi wamejaa fadhaa kutokana na mambo mbalimbali yanayoendelea huku na kule duniani: vita, magonjwa ya kutisha, ukosefu wa ajira, njaa, uhalifu, matetemeko, gharama kubwa za maisha, nk.

Rafiki, usifadhaike. Hayo yote karibu yatakwisha. Biblia inatuhakikishia kuwa hayo si maisha ya milele. Mungu anaumba dunia mpya isiyo na maovu, mateso wala huzuni.

“Sasa, naumba mbingu mpya na dunia mpya, mambo ya zamani hayatakumbukwa tena. Furahini, mkashangilie milele, kwa ajili ya vitu hivi ninavyoumba.."(Isaya 65:17)

Katika mbingu mpya na dunia mpya:
Hakutakuwa na machozi tena wala maombolezo au kilio. (Ufunuo 21:4)
Hakutakuwa na magonjwa wala mauti. Haki itatawala, na amani itakuwa ya kudumu.

"Lakini, kulingana na ahadi yake, twatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake."(2 Petro 3:13).

Hayo sio maneno ya kukutia moyo tu, ni ahadi za kweli kutoka kwa Mungu ambaye hasemi uongo. Kwahiyo tunapoona mambo yanazidi kuwa mabaya duniani, ni ishara kuwa mwisho wa mambo hayo umekaribia.

"Basi mambo hayo yaanzapo kutokea, changamkeni, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu umekaribia."(Luka 21:28)
Sawa mkuu!
 
"Basi mambo hayo yaanzapo kutokea, changamkeni, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu umekaribia."(Luka 21:28)
Waebrania 10:23
"Na tushike kwa uthabiti ungamo la tumaini letu pasipo kuyumba-yumba, kwa kuwa yeye aliyeahidi ni mwaminifu."
 
Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi. Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali. Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo. Yoh 14:1-4.
 
Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi. Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali. Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo. Yoh 14:1-4.
Ameen, barikiwa sana
 
TRela tu hilo
1 Wakorintho 1:18-31
"Kwa maana ujumbe wa msalaba kwa wale wanaopotea ni upuzi, lakini kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu. Kwa maana imeandikwa: “Nitaiharibu hekima ya wenye hekima, na kubatilisha akili ya wenye akili.” Yuko wapi mwenye hekima? Yuko wapi msomi? Yuko wapi mwanafalsafa wa nyakati hizi? Je, Mungu hakufanya hekima ya ulimwengu huu kuwa upumbavu? Kwa kuwa katika hekima ya Mungu ulimwengu kwa hekima yake haukumjua yeye, ilimpendeza Mungu kuwaokoa walioamini kwa upuzi wa lile neno lililohubiriwa..."
 
Siku hizi mistari ya biblia imeanza kuniumiza macho yaan humo nakuta makabila ya wayahudi tu ila Wagalatia
Soma Biblia kwa makini. Jina “Wagalatia” linapatikana mara kadhaa katika Biblia, hasa kwenye waraka wa Paulo kwao — sio kama kabila, bali kama jamii ya kimataifa waliopokea Injili. Hii inaonyesha kwamba ujumbe wa Biblia haujafungwa kwa Wayahudi tu, bali upo kwa ajili yetu sote.
Warumi 1:16
“Kwa maana siionei haya Injili; kwa sababu ni uweza wa Mungu uletao wokovu kwa kila aaminiye; kwa Myahudi kwanza, kisha kwa Myunani pia.”

Matendo 10:34-35
“Hakika natambua kwamba Mungu hana upendeleo, bali katika kila taifa mtu amchaye na kutenda haki hukubaliwa na yeye.”
 
Soma Biblia kwa makini. Jina “Wagalatia” linapatikana mara kadhaa katika Biblia, hasa kwenye waraka wa Paulo kwao — sio kama kabila, bali kama jamii ya kimataifa waliopokea Injili. Hii inaonyesha kwamba ujumbe wa Biblia haujafungwa kwa Wayahudi tu, bali upo kwa ajili yetu sote.
Warumi 1:16
“Kwa maana siionei haya Injili; kwa sababu ni uweza wa Mungu uletao wokovu kwa kila aaminiye; kwa Myahudi kwanza, kisha kwa Myunani pia.”

Matendo 10:34-35
“Hakika natambua kwamba Mungu hana upendeleo, bali katika kila taifa mtu amchaye na kutenda haki hukubaliwa na yeye.”
Wathesalonike
 
Duh, unangoja uone kama yatakwisha?
Hesabu 23:19
Mungu si mtu, aseme uongo, wala si binadamu, abadili nia yake! Je, ataahidi kitu na asikifanye, au kusema kitu asikitimize?
Tatizo binadamu wa siku hizi ni wabishi sana...
 
Back
Top Bottom