Mpira bongo ni kama imani za dini za manabii wa kisasa, hakuna kitu tofauti utawaambia watu wakakuelewa.

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
41,701
55,050
Kwa jinsi mashabiki wa mpira hapa bongo walivyojitolea maisha, akili, hisia, muda na rasilimali zao katika mpira kwa hakika tunaweza kusema mpira ni zaidi ya dini.

Watu wanalala na kuamka wakizungumza mpira, wanashinda wakizungumza mpira.

Jana mchana kwenye East Africa radio kuna kundi la wana Yanga walikuwa wanachangisha pesa za kumpa mchezaji anaitwa Halidi Aucho kwa sababu eti amekuwa hatambuliki kwenye tuzo nyingi nchi hii lakini ni muhimu sana kwa Yanga, hapo wachangiaji ni hadi masikini wenye maisha ya kuunga unga, hii aina tofauti na waumini wa Mwamposa.

Nilikuwa mahali asubuhi kwenye foleni ya huduma, kuna watu watatu pembeni ambao walikuwa hata hawajawanya chai wanajadiliana mkataba wa Kibu Dennis na wanamwagiana details kama vile wanasheria wa mikataba!

Huu mpira bongo kwa hakika umewabamba sana watu, ni zaidi ya dini.
 
Kwa jinsi mashabiki wa mpira hapa bongo walivyojitolea maisha, akili, hisia, muda na rasilimali zao katika mpira kwa hakika tunaweza kusema mpira ni zaidi ya dini.

Watu wanalala na kuamka wakizungumza mpira, wanashinda wakizungumza mpira.

Jana mchana kwenye East Africa radio kuna kundi la wana Yanga walikuwa wanachangisha pesa za kumpa mchezaji anaitwa Halidi Aucho kwa sababu eti amekuwa hatambuliki kwenye tuzo nyingi nchi hii lakini ni muhimu sana kwa Yanga, hapo wachangiaji ni hadi masikini wenye maisha ya kuunga unga, hii aina tofauti na waumini wa Mwamposa.

Nilikuwa mahali asubuhi kwenye foleni ya huduma, kuna watu watatu pembeni ambao walikuwa hata hawajawanya chai wanajadiliana mkataba wa Kibu Dennis na wanamwagiana details kama vile wanasheria wa mikataba!

Huu mpira bongo kwa hakika umewabamba sana watu, ni zaidi ya dini.
Burudani burudani burudaniii...!!!
 
Kwa jinsi mashabiki wa mpira hapa bongo walivyojitolea maisha, akili, hisia, muda na rasilimali zao katika mpira kwa hakika tunaweza kusema mpira ni zaidi ya dini.

Watu wanalala na kuamka wakizungumza mpira, wanashinda wakizungumza mpira.

Jana mchana kwenye East Africa radio kuna kundi la wana Yanga walikuwa wanachangisha pesa za kumpa mchezaji anaitwa Halidi Aucho kwa sababu eti amekuwa hatambuliki kwenye tuzo nyingi nchi hii lakini ni muhimu sana kwa Yanga, hapo wachangiaji ni hadi masikini wenye maisha ya kuunga unga, hii aina tofauti na waumini wa Mwamposa.

Nilikuwa mahali asubuhi kwenye foleni ya huduma, kuna watu watatu pembeni ambao walikuwa hata hawajawanya chai wanajadiliana mkataba wa Kibu Dennis na wanamwagiana details kama vile wanasheria wa mikataba!

Huu mpira bongo kwa hakika umewabamba sana watu, ni zaidi ya dini.
Umegonga pale pale. Hii ni hatari sana. Na kama ulivyosema. Mafukara ndiyo wako mstari wa mbele.
 
Bongo mpira upo kisiasa zaidi kuliko kibiashara au kiuwekezaji. Mashabiki hawafaidiki hata na mia mbovu kutoka timu au vilabu vyao.

Waache walale usingizi mzito wazungumze soka wakati sisi, familia zetu na marafiki zetu tunanufaika ndivyo wasemavyo wanasiasa.
 
Sasa kama hawa masikini waliokuwa wanachangishana jana kumchangia Halidi Aucho wanapata faraja gani ya kupunguza stress za maisha?!
Nayo ni sehemu ya burudani...halafu bongo stress za maisha hazisababishwi tu na ukosefu wa pesa bali kuna matatizo mengi kama matatizo ya ndoa na Ukosefu wa huduma muhimu kama maji....kwahiyo watu wanapambania furaha katika dimbwi la shida
 
Ni Kama fisi amepewa Mfupa apambane nao kuula.

Kuwa shabiki wa mpira sio vibaya Ila kupoteza hela na muda kisa mpira hilo ni tatizo.
 
Kwa jinsi mashabiki wa mpira hapa bongo walivyojitolea maisha, akili, hisia, muda na rasilimali zao katika mpira kwa hakika tunaweza kusema mpira ni zaidi ya dini.

Watu wanalala na kuamka wakizungumza mpira, wanashinda wakizungumza mpira.

Jana mchana kwenye East Africa radio kuna kundi la wana Yanga walikuwa wanachangisha pesa za kumpa mchezaji anaitwa Halidi Aucho kwa sababu eti amekuwa hatambuliki kwenye tuzo nyingi nchi hii lakini ni muhimu sana kwa Yanga, hapo wachangiaji ni hadi masikini wenye maisha ya kuunga unga, hii aina tofauti na waumini wa Mwamposa.

Nilikuwa mahali asubuhi kwenye foleni ya huduma, kuna watu watatu pembeni ambao walikuwa hata hawajawanya chai wanajadiliana mkataba wa Kibu Dennis na wanamwagiana details kama vile wanasheria wa mikataba!

Huu mpira bongo kwa hakika umewabamba sana watu, ni zaidi ya dini.
Ongezea,na mamiziki

Ova
 
Tatizo ni maisha magumu tunayoyapitia katika nchi yetu....kwahiyo watu wanaitumia yanga na simba kama sehemu ya kupunguza stress za maisha
Ungekuwa karibu na mm ningekununulia nyama kilo mbili ukale na shemeji!!
Huo ndio ukweli!! Maisha magumu mno watu hawana burudan nyingine wanajifanya ni wapenda soka mno! Nimekaa UK kwenye uasisi wa Mpira huwezi Kuta mtu anajadili Mpira siku,week nzima kama huku!!
 
Hatuwafikii warabu Misri, Tunisia, Morocco
Hata Ulaya , America kusini nk.
Mpira ushateka watu duniani kama dini na siasa.
Kwani mshabiki wa siasa anafaidika nini kushabikia wanasiasa ?
Kuna watu huko USA apite trump au Haris haitabadili maisha yao ila wanashabikia na kuwachangia hela.
Dunia imeamua kuchagua haya mambo, na yasipokuwepi haya yataibuka mengine.
Mimi binafsi nayachukulia mambo ya dunia kama upuuzi fulani uiokubalika without one's purpose na kuwanyang'anya binadamu uhuru wao na kuwafanya kuwa wafuasi au zombie automatic.
 
Bongo mpira upo kisiasa zaidi kuliko kibiashara au kiuwekezaji. Mashabiki hawafaidiki hata na mia mbovu kutoka timu au vilabu vyao.

Waache walale usingizi mzito wazungumze soka wakati sisi, familia zetu na marafiki zetu tunanufaika ndivyo wasemavyo wanasiasa.

Ni wapi mashabiki wanapokea pesa toka kwenye timu wanazoshabikia?
 
Back
Top Bottom