Mke Ukiachika, Ukapata Bwana Mpya, Ni Sawa Kumzungumzia Bwana wa Zamani Kila Uchao? Wanasiasa Hamahama, Wanachofanya ni Sawa Kuponda Tuu Walipotoka?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
51,616
116,845
Wanabodi,

Usingizi ukikata, huwa nashuka jf anytime, leo nauliza Mke au Mume ukiachika, au ukaachwa, kisha ukapata bwana mpya, au chombo kipya, je ni sawa kumzungumzia bwana wako wa zamani kila uchao mbele ya bwana mpya au bibi mpya?.

Je hiki kinachofanywa na wanasiasa hamahama, kila saa ni kuponda tuu vyama vyao vya zamani, is it right?. Hii ni sawa?

Kule nyuma niliwahi kutoa angalizo hili Angalizo kwa Wanasiasa hamahama; Japo ni haki yenu lakini msisahau fadhila. Kuweni watu wa shukrani, mtabarikiwa sana, vinginevyo karma Itawahusu!

As days go by, nimeona baadhi ya wanasiasa hama hama walio defect kutoka Chadema hivi karibuni, na kujiunga CCM, kila wakisimamishwa na kutambulishwa kwenye mikutano ya hadhara, wao ni kuisema tuu Chadema, Chadema Chadema in a negative way!.

Edward Lowassa alihama CCM, akajiunga Chadema, mliwahi kumsikia akiizungumzia CCM negatively akiwa Chadema?. Na baada ya kurejea CCM, mmewahi kumsikia akiizungumzia Chadema negatively?.

Stephen Wasira, Lawrence Masha, Njelu Kasaka, na wengine wengi, walikuwa CCM, wakahamia Chadema na kurejea CCM, mliwahi kuwasikia wakizungumza negatively kuhusu upande wowote?.

Mke ukiachika, ukapata bwana mpya, acha kumzungumzia bwana wako wa zamani mbele ya bwana wako mpya kila uchao!.

The same applies to Bwana, bibi umemuacha, sasa una chombo kipya acha kumzungumzia yule bibi wa zamani, mbele ya bibi mpya!, utaonekana bado unampenda, hivyo kumzungumzia negatively all the time, lengo lako ni to inflict pain ili aumie, utajikuta sio tuu unaumia mwenyewe, bali pia unamuumiza huyo bwana mpya au bibi mpya.

Naendelea kuwasisitiza hawa wanasiasa hamahama, wenye tabia hizi Mwalimu Nyerere alizozizungumza,
View: https://youtu.be/Qc-nXKcZbbc?si=06keCte9MvrSj3Jf

Ukihama mahali, achana na ulipohama, zungumzieni bwana wenu mpya!, zungumzieni vyama vyenu vipya!, achaneni kuzungumzia vyama vyenu mlivyovihama, vinginevyo mtaonekana na wanasiasa muflis!.

Jitahidini muwe na civility na shukrani ya mlipotoka!, karma ipo and is real!. Angalizo kwa Wanasiasa hamahama; Japo ni haki yenu lakini msisahau fadhila. Kuweni watu wa shukrani, mtabarikiwa sana, vinginevyo karma Itawahusu!

Hawa wanasiasa hamahama mimi nawaita kama Nyerere alivyowaita Tanzania nchi ya ajabu!, Badala ya wanawake kutongozwa, ni Wanaume!, wanawake wanaotongozeka kirahisi ni malaya, Je, hawa wa'ume tuwawaiteje?

Politics is a very dirty game, hakuna rafiki wa kudumu wala adui wa kudumu, only a common interest!.

Kuna watu wana kinyaa na mtu kutapika halafu kulamba matapishi!, mbwa hana kinyaa, anatapika na analamba matapishi yake!, the same applies kwa Wanasiasa hamahama Swali Kuhusu Kulamba Matapishi: Kwanini Iwe ni Kinyaa Wakati Matapishi ni Chakula Kile Kile?!.

Ijumaa Kareem
Paskali.
 
Sio sawa hata kidogo. Ni umaskini wa mawazo na fikra. Mfano kwa Mch. Msigwa kama hakuweza kujijenga kipindi yupo CDM kama kiongozi kwa ngazi mbalimbali ilimpasa kama amehama, aachane na siasa au ajikite kwenye investment zake la hasha basi chama alichoenda angejikita kwenye kunadi sera za CCM. Kitendo cha kusema madhaifu ya sehemu ulikotoka tena kwa mwanaume inaleta tafakuri sana na ni mtu ambaye hana akili na mpumbavu ndiyo anaweza kufanya hivyo.​
 
Chadema hivi Chadema vile lawama za alikotoka hawaziwasaidii wa upande alioenda cha ajabu wale wananchi waomsikiliza wanashangilia na kupiga makofi unabaki kujiuliza haya ni mazuzu?

Msigwa alipaswa kueleza namna atasaidiana na viongozi wa ccm kuwaletea wanchi maendeleo sio kueleza kasoro za alikotoka hizo kasoro kwa muda aliokaa chadema hakuziona au kuzitatua?

Awam ya 5 ange-surrender wala isingekuwa ajabu kuinua mikono awamu ya mama kumechangia kuonyesha namna alivyo dhaifu.

Kwa ujumla Peter Msigwa hana shukrani!
 
Wanabodi,

Usingizi ukikata, huwa nashuka jf anytime, leo nauliza Mke au Mume ukiachika, au ukaachwa, kisha ukapata bwana mpya, au chombo kipya, je ni sawa kumzungumzia bwana wako wa zamani kila uchao mbele ya bwana mpya au bibi mpya?.

Je hiki kinachofanywa na wanasiasa hamahama, kila saa ni kuponda tuu vyama vyao vya zamani, is it right?. Hii ni sawa?

Kule nyuma niliwahi kutoa angalizo hili Angalizo kwa Wanasiasa hamahama; Japo ni haki yenu lakini msisahau fadhila. Kuweni watu wa shukrani, mtabarikiwa sana, vinginevyo karma Itawahusu!

As days go by, nimeona baadhi ya wanasiasa hama hama walio defect kutoka Chadema hivi karibuni, na kujiunga CCM, kila wakisimamishwa na kutambulishwa kwenye mikutano ya hadhara, wao ni kuisema tuu Chadema, Chadema Chadema in a negative way!.

Edward Lowassa alihama CCM, akajiunga Chadema, mliwahi kumsikia akiizungumzia CCM negatively akiwa Chadema?. Na baada ya kurejea CCM, mmewahi kumsikia akiizungumzia Chadema negatively?.

Stephen Wasira, Lawrence Masha, Njelu Kasaka, na wengine wengi, walikuwa CCM, wakahamia Chadema na kurejea CCM, mliwahi kuwasikia wakizungumza negatively kuhusu upande wowote?.

Mke ukiachika, ukapata bwana mpya, acha kumzungumzia bwana wako wa zamani mbele ya bwana wako mpya kila uchao!.

The same applies to Bwana, bibi umemuacha, sasa una chombo kipya acha kumzungumzia yule bibi wa zamani, mbele ya bibi mpya!, utaonekana bado unampenda, hivyo kumzungumzia negatively all the time, lengo lako ni to inflict pain ili aumie, utajikuta sio tuu unaumia mwenyewe, bali pia unamuumiza huyo bwana mpya au bibi mpya.

Naendelea kuwasisitiza hawa wanasiasa hamahama, wenye tabia hizi Mwalimu Nyerere alizozizungumza,
View: https://youtu.be/Qc-nXKcZbbc?si=06keCte9MvrSj3Jf

Ukihama mahali, achana na ulipohama, zungumzieni bwana wenu mpya!, zungumzieni vyama vyenu vipya!, achaneni kuzungumzia vyama vyenu mlivyovihama, vinginevyo mtaonekana na wanasiasa muflis!.

Jitahidini muwe na civility na shukrani ya mlipotoka!, karma ipo and is real!. Angalizo kwa Wanasiasa hamahama; Japo ni haki yenu lakini msisahau fadhila. Kuweni watu wa shukrani, mtabarikiwa sana, vinginevyo karma Itawahusu!

Hawa wanasiasa hamahama mimi nawaita kama Nyerere alivyowaita Tanzania nchi ya ajabu!, Badala ya wanawake kutongozwa, ni Wanaume!, wanawake wanaotongozeka kirahisi ni malaya, Je, hawa wa'ume tuwawaiteje?

Politics is a very dirty game, hakuna rafiki wa kudumu wala adui wa kudumu, only a common interest!.

Kuna watu wana kinyaa na mtu kutapika halafu kulamba matapishi!, mbwa hana kinyaa, anatapika na analamba matapishi yake!, the same applies kwa Wanasiasa hamahama Swali Kuhusu Kulamba Matapishi: Kwanini Iwe ni Kinyaa Wakati Matapishi ni Chakula Kile Kile?!.

Ijumaa Kareem
Paskali.

Bottom line: Mbowe ni tatizo akubali tu!
 
Wanakera sana walitakiwa wajikite kutuelezea malengo yao tu mtu wa namna hiyo sio wa kumuamini rohoni huwa anaumia kwa kuwa bado anakipenda kile chama chake cha zamani!
Tuwe wakweli bwashee; Anachofanya Msigwa ni UPUMBAVU mkubwa.

Lakini Hilo haliondoi Ukweli kwamba Watanzania wamemchoka Mbowe!

Imani Kwa wapenda mageuzi iliisha pale Mbowe alipoanza kujipendekeza ikulu na kuwa Sehemu ya Machawa.

Huu Ukweli mchungu lazima tuukubali, Mbowe awajibike tu na apumzike
 
Wanasiasa uchwara wana mengi ya kujifunza kwa marehemu Edward Ngoyai Lowassa. Pamoja na kufanyiwa figisu kwenye mchakato wa kura za maoni 2015, na baadaye kuhamia CHADEMA!

Pamoja na kutukanwa, kukejeliwa kubagazwa, nk! Hakuwahi kumtukana mtu, wala chama chake cha ccm! Badala yake alijikita kwenye kutangaza sera zake tu iwapo angechaguliwa kuwa Rais!!

Kwa hiyo Mchungaji Msigwa na wenzake wasio na shukrani, wana cha kujifunza! Uungwana ni vitendo na siyo vijembe na majibizano yasiyo na kichwa wala miguu. Na CHADEMA nao waoneshe ukomavu kwa kumpuuzia. Na wasiendelee kujibizana naye.
 
Back
Top Bottom