KERO Misugusugu Kibaha: Kiwanda cha kutengeneza pombe kinatiririsha maji machafu na kuzalisha harufu kali eneo lote linalozungukwa na Kiwanda

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

The Watchman

JF-Expert Member
Nov 7, 2023
1,141
1,944
1745309393120.png
Wananchi na wakazi katika eneo la Mleleguo kata ya Misugusugu, Kibaha mkoa wa Pwani tumekuwa na hali ngumu sana ilinayosababishwa na uchafuzi wa mazingira unaofanywa na kiwanda cha wahindi kinachozalisha Pombe kali, kwani muda wote eneo zima la Mleleguo limetawaliwa na harufu kali ya pombe kiasi hewa tunayoivuta ni hiyo harufu mapaka vichwa vinauma na kupata vizunguzungu.

Nyakati za usiku ni kama hiyo harufu inafunguliwa maradufu mtu huwezi kupata usingizi ukigeuka kulia, kushoto umelala unavuta harufu ya pombe kali.
1745309446465.png

Wamiliki wa kiwanda hajali usalama wa wakazi walio karibu na kiwanda kwani yanatiririshwa maji machafu yenye harufu kali ya pombe, ambayo moja ya madhara yaliyosababishwa na maji hayo ni kuuliwa kwa samaki zilizokuwa zikifugwa na mtanzania mmoja baada ya maji hayo kufikia bwawa la samaki.


Maji yanayotiririshwa si salama na hayadhibitiwi inavyotakiwa, liko wapi Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) mnafanya kazi gani wakuu tunasikia tu kuwa NEMC walikuja hapo kiwandani lakini hakuna dalili inayoonesha kuwa changamoto hii itatatuliwa karibuni.
 
Back
Top Bottom