Mhubiri wa Injili awapa siku 14 'manabii' kuacha unabii wao, awaita matepeli wa kiroho

Daniel Mbega

JF-Expert Member
Mar 20, 2013
338
180
Muda huu kuna mhubiri wa Injili, Daudi Mashimo aka Komandoo wa Yesu, anaendelea na mkutano na waandishi wa habari kwenye Ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo akiwataka wanaojiita manabii nchini Tanzania waache mara moja kujiita hivyo kwa sababu unabii unatoka kwa Mungu na kwamba nabii wa kweli atakuja wakati utakapofika.

Amewapa siku 14 watubu, vinginevyo yuko tayari kutoa hadharani siri zao na nguvu wanazozitumia kwa sababu wanachofanya ni utapeli wa kiroho na kuwapotosha watu.

"Watanzania wengi wana hali ngumu kimaisha, sasa hawa matapeli wa kiroho wanatumia fursa hiyo kuwahadaa na kuwapotosha, nawataka waache mara moja vinginevyo baada ya siku 14 nitatoa siri zao na jinsi wanavyotumia nguvu za miujiza za 'Mngindo' ambazo ni za kichawi," anaeleza.
 

  • Naye tunaomba aache hilo jina lake bandia kwakuwa Yesu hatambui ukomandoo wake kwake Yesu
  • Nijuavyo ni kuwa roho hahusishwi na aina yoyote ya uchafu, labda aseme ni utapeli tu lakini si kiroho
  • Atuambie je asipoweza kuwapa hiyo adhabu katika hizo siku 14, tumchukulie naye ni tapeli au?
 
Nenda kasali popote male ila imaniyako ndo nguzo yako sifuati miujiza kanisani nafuata mafundisho pia ukion, mafundiyo hayo hayaendani na kiroho hurazimishwi.hama
 
1. Yeye ametumia kifungu kipi cha Biblia kusemea hayo?
2. Huduma zote ikiwemo yake imetoka kwa Mungu. Je! Huduma au karama ya unabii haipo?
3. Kama ipo, anasoma biblia ipi?
4. Ni kweli manabii/watumishi wa uongo wapo (ilitabiriwa) ... Ni jukumu lake kuzipambanua hizo roho na manabii wa ukweli. Kama ameshindwa na kuamua kugeneralize, je! uinjilisti wake hauna walakini?
5. Mambo ya kiroho huhusu roho, huamuliwa kiroho na ndio maana tumeambiwa vita hii si juu ya damu na nyama (mwilini). Je! Kitendo chake kwa kwenda HM ni cha kiroho? Je! Ameamua kupigana vita vya kimwili?
6. Mwisho, tumeamriwa kufundisha kuhusu KUMJUA MUNGU basi. Je! Anaposema anataka kufundisha kuhusu uchawi na njia zao ametumia maandiko yapi?
 
Nae ni jipu mbona kama anaweweseka isije ikawa kazidiwa kete hata baada ya siku hizo hato fanya lolote
 
Maadamu mtumish anahubiri kwa kufuata biblia na anahubiri maneno kutoka kwenye biblia na akanipa unabii na ukawa wa kweli mimi sina shida hapo na huyo nabii.
 
Komandoo ni mtu anayefanya kazi za mauaji ya ukatili na uharibifu mkubwa, sasa anapojiita kuwa yeye ni komandoo wa yesu sijui ana maana gani, wote hao ni matapeli tu
Komandoo sio muharifu, na wala sio muuaji. Ila yote kwa yote wanajiita makomando, wanajifananisha ushupafu ambao makomandoo wanao.
 
Maadamu mtumish anahubiri kwa kufuata biblia na anahubiri maneno kutoka kwenye biblia na akanipa unabii na ukawa wa kweli mimi sina shida hapo na huyo nabii.
.......... kama yule Nabii Bilionea ! Wagalatia mnapenda mzaha ...... mpaka na Mungu !?
 

Huyo mwinjilisti Biblia yake itakuwa ilinyofoka ukurasa wenye 1Wakorintho sura ya 12.
 
Unabii ndio ulikamilisha again jipya.....na nabii Wa kweli hawezi kutoka na kubishana na watu but anakuombea Mungu akusamehe pia atakupenda zaidi....the first thing is to love nomatter weakness he or she is ......maana who are you to judge...only GOD can judge us...not a human like me.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…