Mgonjwa wa akili aliingia saluni na kujifuta kichwa na taulo kisha akaondoka

machiaveli

JF-Expert Member
Jun 4, 2016
2,107
4,693
Habari wakuu?

Iko hivi kwa ufupi, Mimi sio muandishi mzuri Kuna saloon napenda kunyoa pande flani za Sakina Arusha(nimetaja jina Ili kama kuna Wana JF walioona wajazie nyama)

Pale saloon tulikua watu watano kinyozi alikua akimnyoa dogo mmoja na sisi watatu tumekaa kwenye sofa huku tukisubiria dogo anyolewe tufuate.

Mlango wa kuingia saloon uko kwa nyuma yetu so ukiangalia kule mbele kwa kinyozi unaona nyuma mtu anayezama ndani.

Sasa Mimi kuangalia mbele nikaona Kuna jomba mmoja mlemavu wa akili sisi tunaitaga vichaaa amevaa manguo mengi ametua mizigo yake hapo mlangoni machupa, mifupa na vitu sijui nini.

Taratibu akasukuma mlango wa saloon akatinga ndani, alikua amenyoa nywele kama na wembe hivi upara ila kama amejikataka kichwani manake Kuna damu damu na mabaki ya nywele kama matuta.

Sasa alivyotimba tu wale wenzangu na mimi wote tukashtuka tukanyanyuka na kufreez tukasimama upande wa kinyozi.

Yule jomba akakaa kweli like sofa akajaa pale na manguo yake, hakuna aliyeongea zaidi ya kinyozi kuzima mashine na dogo aliyenyolewa upande wa kushoto na shuka lake na wote sisi kutoka nje ya saloon.

Baadae ya kutoka kinyozi anashika simu sijui anaupiga polisi au wapi, ikabidi niite raia kumchungulia jomba tunamuona kashika zile taulo za saloon anafuta kichwa chake,taulo zote zikawa nyeusi tiii.

Mwenyekiti akasema tumvungie, akatoka bila kugusa chochote akaokota mzigo wake hapo nje, mzito niliutesti haukosi kilo 20 akatembea zake.

Jamaa ilibidi afunge saloon saa ile ile juzi akaenda tafuta wachungaji na mafuta na machumvi anahisi ni mashetani!

Ndio hivyo ila mi sielewi
 
Habari wakuu?
Iko hivi kwa ufupi,Mimi sio muandishi mzuri Kuna saloon napenda kunyoa pande flani za sakina arusha(nimetaja jina Ili kama Kuna Wana jf walioona wajazie nyama)
Pale saloon tulikua watu watano kinyozi alikua akimnyoa dogo mmoja na sisi watatu tumekaa kwenye sofa huku tukisubiria dogo anyolewe tufuate.
Mlango wa kuingia saloon uko kwa nyuma yetu so ukiangalia kule mbele kwa kinyozi unaona nyuma mtu anayezama ndani!
Sasa Mimi kuangalia mbele nikaona Kuna jomba mmoja mlemavu wa akili sisi tunaitaga vichaaa amevaa manguo mengi ametua mizigo yake hapo mlangoni machupa,mifupa na vitu sijui nini!!
Taratibu akasukuma mlango wa saloon akatinga ndani,alikua amenyoa nywele kama na wembe hivi upara ila kama amejikataka kichwani manake Kuna damu damu na mabaki ya nywele kama matuta!
Sasa alivyotimba tu wale wenzangu na mimi wote tukashtuka tukanyanyuka na kufreez tukasimama upande wa kinyozi!
Yule jomba akakaa kweli like sofa akajaa pale na manguo yake,hakuna aliyeongea zaidi ya kinyozi kuzima mashine na dogo aliyenyolewa upande wa kushoto na shuka lake na wote sisi kutoka nje ya saloon!
Baadae ya kutoka kinyozi anashika simu sijui anaupiga polisi au wapi,ikabidi niite raia kumchungulia jomba tunamuona kashika zile taulo za saloon anafuta kichwa chake,taulo zote zikawa nyeusi tiii!
Mwenyekiti akasema tumvungie,akatoka bila kugusa chochote akaokota mzigo wake hapo nje,mzito niliutesti haukosi kilo 20 akatembea zake!!!

Jamaa ilibidi afunge saloon saa ile ile juzi akaenda tafuta wachungaji na mafuta na machumvi anahisi ni mashetani!
Ndio hivyo ila mi sielewi
Yani wanaume wanne mnamkimbia mtu mmoja!!

Hizi aibu zingine msiwe mnasimulia maana inaonekana hata angewaambia bong'oeni awapige pipe wote mngetii sheria bila shuruti.

Vijana mnatia aibu sana mpo legelege sana.
 
Mimi hapo naona Kinyozi na wateja wake ndio vichaa na huyo kichaa ndio mzima,

Kama alifika akakaa kwenye sofa,kwanini wasingemuuliza kua anataka nini? Kwa vile walimu ignore,akaamua kujihudumia mwenyewe na kusepa bila kumdhuru mtumk
Ac
Mimi hapo naona Kinyozi na wateja wake ndio vichaa na huyo kichaa ndio mzima,

Kama alifika akakaa kwenye sofa,kwanini wasingemuuliza kua anataka nini? Kwa vile walimu ignore,akaamua kujihudumia mwenyewe na kusepa bila kumdhuru mtu.
Acha ushujaa wa kuandika mkuu!
 
Back
Top Bottom