Mgomo wa Wafanyabiashara wafika Mbeya, Mwanza, Dodoma, Arusha, Mtwara, Tunduma, Iringa

Wild Flower

JF-Expert Member
Jul 20, 2023
241
542
IMG-20240626-WA0002.jpg
IMG-20240626-WA0006.jpg


Manzese
Picha ikionyesha baadhi ya maduka eneo la Manzese Tiptop, jijini Dar es Salaam leo asubuhi Jumatano Juni 26, 2024 yakiwa yamefungwa kutokana na mgomo wa wafanyabiashara unaoendelea katika baadhi ya mikoa nchini.

Madai ya wafanyabiashara ni pamoja na utitiri wa kodi unaotozwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Kariakoo
Wafanyabiashara wa Kariakoo, jijini Dar es Salaam wameingia katika siku ya tatu mgomo wa kufungua maduka waliouanza Jumatatu ya Juni 24, 2024 wakipinga tozo na kamatakamata inayofanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Hadi saa 3:30 asubuhi ya leo Jumatano, Juni 26, 2024, baadhi ya maduka hayajafunguliwa kama ilivyokuwa juzi na jana. Baadhi ya wafanyabiashara waliofungua maduka ni wale wanaouza vipodozi, simu na dawa.

Baada kuanza kwa mgomo huo, Serikali ilifanya kikao na viongozi wa wafanyabiashara hao na kutangaza kusitisha kwa muda ukaguzi wa risiti za kielektroniki za EFD inayofanywa na TRA, lakini wafanyabiashara wameendelea na mgomo

Mbeya
Mgomo wa wafanyabiashara wa maduka jijini Mbeya umeendelea leo Jumatano, Juni 26, 2024 ikiwa ni siku ya pili, huku baadhi ya maduka ya pembeni yakifunguliwa.

Wafanyabiashara hao wameanza kugoma jana JUni 25, wakishinikiza Serikali kuondoa utitiri wa kodi na tozo mbalimbali ambazo si rafiki kwa wafanyabiashara.

Mwananchi Digital ambayo ipo maeneo ya Soko la Sido, Mwanjelwa na Kabwe imeshuhudiwa maduka makubwa yakiwa yamefungwa, huku madogo ya pembeni yakiwa wazi yakitoa huduma.

Pia wafanyabiashara wanauza bidhaa zao nje, wanaendelea, ingawa ni kwa kificho.

Hata hivyo, hakuna mfanyabiashara aliyeeleza kuhusu hatima ya mgomo huo, iwapo utaendelea au kusitishwa kwa kipindi hiki.

Mwanza
Wakati mgomo wa wafanyabiashara jijini Mwanza ukiingia siku ya pili, maofisa wa Jeshi la Polisi wanaotembea na waliopo kwenye magari wameonekana wakipita katika mitaa mbalimbali ya jijini hilo, huku maduka yakiwa hayajafunguliwa.

Kamera ya Mwananchi Digital iliyoko mtaani kuanzia saa 12:30 hadi saa 3:00 asubuhi ya leo Jumatano Juni 26, 2024, imeshuhudia magari yaliyojaa askari wa Jeshi la Polisi yakikatiza, huku baadhi ya askari polisi wakitembea kwa miguu kuzunguka mitaa ya jiji hilo.

Alipoulizwa kuhusu askari hao, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Wilbroad Mutafungwa amethibitisha kuwasambaza askari katika mitaa ya jiji hilo, huku akidokeza kuwa jukumu lao ni kuimarisha ulinzi kwa wafanyabiashara watakaofungua maduka, ili wasifanyiwe fujo na waliogoma.

Kamanda Mutafungwa amesema ulinzi na doria hizo zitakuwa endelevu hadi hali itakaporejea katika utimamu, huku akionya watakaojaribu kuwafanyia vurugu wafanyabiashara walioridhia kufungua maduka yao.

Dodoma
Picha ikionyesha baadhi ya maduka katika Mtaa wa One way, leo Jumatano Juni 26, 2024 jijini Dodoma ambapo wafanyabiashara wamefunga maduka yao, ikiwa ni siku ya pili ya mgomo.

Madai ya wafanyabiashara ni pamoja na utitiri wa kodi unaotozwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Mtwara
Wafanyabiashara katika soko kuu lililopo Karibu na Stendi ya zamani mkoani Mtwara wamefunga maduka yao leo Jumatano, Juni 26, 2024.

Tunduma
Maduka katika soko kuu la Manzese, Halmashauri ya mji wa Tunduma mkoani Songwe yakiwa yamefungwa.

Wafanyabiashara hao wamefunga maduka kushinikiza kupunguzwa kwa utitiri wa kodi wanaotozwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Arusha
Maduka mkoani Arusha yakiwa yamefungwa leo Alhamisi Juni 26, 2024, ikiwa ni hatua ya kuunga mkono mgomo wa wafanyabiashara, kushinikiza kupunguzwa kwa utitiri wa kodi wanazotozwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Pia soma:
 
Mgomo wa kutofungua Maduka ulianza Juni 24, 2024 jijini Dar es Slaam baada ya kutangazwa kupitia kipeperushi kilichosambazwa kwenye Mitandao ya Kijamii tangu Jumamosi ya Juni 22, 2024, wakidai kuchoshwa na vitendo wanavyofanyiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)

Wafanyabiashara wa Iringa nao wamefunga maduka leo Juni 26,2024 wakiungana na wenzao wa Dar es salaam, Arusha, Mbeya, Mwanza na Mtwara kushinikiza Serikali kusikiliza malalamiko yao juu ya kodi zisizo rafiki wanazokumbana nazo TRA.
Hata wagome Kila mahala,njaa itafanya wafungue maduka bila shuruti.

Serikali ingetikisika kama transit na banks zingegoma sio hao wachuuzi.

Fungeni maduka hata mwaka muone kama Serikali itashindwa kulipa Wafanyakazi wa Umma.
 
Hata wagome Kila mahala,njaa itafanya wafungue maduka bila shuruti.

Serikali ingetikisika kama transit na banks zingegoma sio hao wachuuzi.

Fungeni maduka hata mwaka muone kama Serikali itashindwa kulipa Wafanyakazi wa Umma.
Unadhani hizo bank zinakosa mapato kiasi gani biashara zilivofungwa, uwezo wa kufikiri uliouonesha hata mwanangu wa babyclass anakushinda
 
Unadhani hizo bank zinakosa mapato kiasi gani biashara zilivofungwa, uwezo wa kufikiri uliouonesha hata mwanangu wa babyclass anakushinda
Nasisitiza, wachuuzi hawawezi tingisha Serikali.Hajuna hasara yeyote ya maana inaletwa na wachuuzi Kwa Serikali au banks yaani impacts Yao ni insignificance.

Wao wanaweza goma hata mwaka mzima kama Wana hiyo jeuri ila Serikali itatukisika kama transit na banks ndio watagoma,wachuuzi gomeni hata mwaka njaa itawatoa tuu ndio maana kwenye mgomo ni sections ya vieneo tena wafanyabiashara wa Jumla wachache na sio wengine.
 
Kama huu ndo uwezo wako wa mwisho kabisa wa kufikiri jishike kalioni na ujinuse huenda akiri Yako itanzinduka upya!

Bank bila wafanyabiashara Kuna bank Sasa? Yaani isubiri waajiriwa mara Moja Kwa mwezi
Hata wagome Kila mahala,njaa itafanya wafungue maduka bila shuruti.

Serikali ingetikisika kama transit na banks zingegoma sio hao wachuuzi.

Fungeni maduka hata mwaka muone kama Serikali itashindwa kulipa Wafanyakazi wa Umma.
 
Hata wagome Kila mahala,njaa itafanya wafungue maduka bila shuruti.

Serikali ingetikisika kama transit na banks zingegoma sio hao wachuuzi.

Fungeni maduka hata mwaka muone kama Serikali itashindwa kulipa Wafanyakazi wa Umma.
Transit wanasafirisha nini na benk pia wanawateja gani?
 
Sisi kama wafanyabiashara tumepanga tugome mwezi mzima.na ikitokea Hawa vyura viziwi wataendelea kuziba masikio basi kitakachofuata tu aanza na bunge kama walivyofanya wakenya ambalo ndilo kichochoro Cha kupitisha Sheria za hovyo na tutamalizia magogoni kumfurusha chura Hadi alie ooh ooh ooh.
 
Kwa hiyo mizigo ya Nje ya Nchi inafungashwa Kariakoo? 😂😂🤣

Ona boya hili.Nyie wa fremu fungeni kabisa Hadi mwaka mzima tuone
Na ulivokosa akili ungekua unajua umuhimu wa kkoo kwa gvt wasingekuwa na ofisi kuu ya kukusanya kodi ya tra mkoa wa kodi kkoo haipo mahali popote mkoa wa kodi kkoo kwa tz hiii pimbi mla bure wewe.
 
Na ulivokosa akili ungekua unajua umuhimu wa kkoo kwa gvt wasingekuwa na ofisi kuu ya kukusanya kodi ya tra mkoa wa kodi kkoo haipo mahali popote mkoa wq kodi kkoo kwa tz hiii pimbi mla bure wewe.
Ona hili punga,msijipe umuhimu ambao hamna,hapo Mkoa wa Kodi wa Kariakoo unakusanya less than 150bln Kwa mwaka,yaani Ngorongoro ni muhimu kushinda Hilo Gulio.

So acha ujinga,fungeni hata mwaka muone kama Nchi itasimama.
 
Wewe ndo boya unaonekana unalala kwa shemeji yako fuatilia mgomo upo kariakoo tu kingine unatakiwa ujue kkoo ni Cbd ww kula kulala ngapoya.
Mnajipa umuhimu ambao hamna 😁😁
Kwani bila Kariakoo Nchi haipati bidhaa? Kwamba Viwanda vitafunga kisa Kariakoo au? Kwani hawana outlets zingine? Mbona Mimi naagiza bidhaa za bati kiwandani au tiles kiwandani bila kuja Kariakoo? Yaani hayo maulembo ndio mnatisha watu? Wacha ujinga
 
Back
Top Bottom