Mch. Peter Msigwa, kwanini umekubali kuingia kwenye mtego kirahisi hivi? Tubu, omba radhi yaishe. Mungu atakusamehe

The Palm Beach

JF-Expert Member
Dec 30, 2015
1,404
2,895
Moderator, tafadhali kwa heshima na taadhima, naomba Uzi huu ujitegemee, usiunganishwe. Nataka rafiki yangu Mch. Peter Msigwa au washauri wake wa karibu wauone kirahisi pengine naweza kumsaidia. Ni rafiki na ndugu yangu, akinisoma tu ananielewa kwa code zetu...

=====================================

Ndugu yangu na rafiki yangu Mch. Peter Msigwa;

Bwana Yesu Kristo apewe sifa mchungaji wangu...!

Hapa ulifanyaga vizuri sana kuomba radhi ulipogundua kuwa umerusha tuhuma za uongo dhidi ya Abdulhaman Kinana mwaka 2020. Hata kwa hili, unayo fursa ya kurekebisha mambo kabla hayajakuharibikia...
=====================================

Mimi hata hivyo najiuliza, ni kwanini umekubali shetani akuingize kwenye mtego rahisi lakini hatari kiasi hiki. Kwanini unajipeleka kwenye mauti ya kama afavyo mpumbavu mfano wa Abneri wa kwenye Biblia....?

‭2 Samwel 3:32-34 SUV‬​
".....Wakamzika Abneri katika Hebroni; naye mfalme akapaza sauti yake, akalia kaburini kwa Abneri, nao watu wote wakalia. Ndipo mfalme akamwomboleza Abneri, akasema, Ilimpasaje Abneri kufa afavyo mpumbavu? Mikono yako haikufungwa, Wala miguu yako haikutiwa pingu; Aangukavyo mtu mbele ya wana wa uovu, ndivyo ulivyoanguka. Na watu wote wakaongeza kumlilia....."


Mch. Peter Msigwa, usife kipumbavu kama kamanda wa Jeshi la Mfalme Saudi, Capt. Abneri alivyokufa na Daud kumshangaa kufa vile. Mikono, akili na ufahamu wako havijafungwa. Unaweza kujiponya sasa kwa maamuzi ya hekima maana hii ndiyo silaha yako kwa sasa. Hekima na kuomba radhi, basi....

Fahamu kuwa, kuhama chama cha siasa na kujiunga na kingine wala siyo tatizo hapa......

Tatizo ni kukosa kwako kuenenda kwa hekima baada ya hapo. Na sasa ukikaa vibaya tu na ukishupaza shingo yako tu kwa sababu ya fahari ya dunia hii; pesa, umaarufu nk, nakuhakikishia jambo moja kuwa, unakwenda kuangamia kiroho na kimwili moja kwa moja muda si mrefu ...!

Mchungaji wangu hebu soma maandiko haya ktk Biblia yako👇;

Wagalatia 6:7-8 SUV‬
"......Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa cho chote apandacho mtu, ndicho atakachovuna. Maana yeye apandaye kwa mwili wake, katika mwili wake atavuna uharibifu; bali yeye apandaye kwa Roho, katika Roho atavuna uzima wa milele..."

Mchungaji wangu, usidanganyike, Mungu hadhihakiwi. Unachokipanda, ndicho unachovuna maana yeye Mungu keshasema hivyo.....

Nimeona "demand notice" uliyotumiwa na wanasheria wa uliyeamua kupambana naye. Ni ngumu kwako. Imeandaliwa kitaalamu kweli ikibeba kila shutuma na tuhuma zako.....

Nafsi na roho yangu mimi inaniambia, ulivuka mstari wa siasa zako na kuanza kumshambulia mtu. Na ni dhahiri kabisa kuwa, huna ushahidi wa tuhuma zako hizi......

Bahati mbaya kuwa, wewe unadhani ulikuwa unafanya siasa. Lakini siasa yako hukuiwekea mpaka kutenganisha kati ya freeman Mbowe - CHADEMA kama taasisi na Freeman Mbowe kama mtu binafsi, mwana familia na mfanyabiashara.....

Ukubali kuwa ulitoka kwenye kuishambulia taasisi na badala yake ukaanza kum - defame mtu binafsi. Kuuvuka mpaka huo ni lazima uingie kwenye mgogoro wa kisheria iwapo mtu huyo ataamua kukushughulikia. Na hivi ndivyo ilivyo Sasa......

Ushauri wangu ni huu. Ishinde AIBU na FEDHEHA kama mchungaji wako mkuu Yesu Kristo alivyoishinda aibu na fedheha ya msalaba. Soma Biblia yako 👇 👇 tena;

‭Waebrani 12:1-3 SUV‬
"........Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu, tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu. Maana mtafakarini sana yeye aliyeyastahimili mapingamizi makuu namna hii ya watendao dhambi juu ya nafsi zao, msije mkachoka, mkizimia mioyoni mwenu...."

Ukifanikiwa hili, omba tu radhi yaishe na endelea na siasa zako huko CCM lakini ukiwa na umakini zaidi safari hii......

Tumia hekima yako ya kichungaji kufanya siasa zako. Jifunze kwa wenzio kina Tundu Lissu. Wanajua kucheza mchezo ktk mpaka wa sheria za mchezo ndio maana watesi wake wakimpeleka kwenye sheria, huwashinda kirahisi au wenyewe huzitelekeza kesi.......

Watu aina ya Tundu Lissu wanajua kudhibiti midomo yao kuwaingiza ktk migogoro ya kisheria. Wewe sijui umepagawa na nini maana aada ya kuhama CHADEMA na kwenda huko umekuwa kama kichaa fulani asiye na udhibiti hata kama atafungwa kamba za mkatale kwani miropoko yako huishangaza dunia nzima......!

Mungu akubariki, akurehemu na akupe neema ya kukufungua ufahamu wako urudi katika hali yako ya kawaida.
PIA SOMA

- Kuelekea 2025 - Freeman Mbowe amtaka Mchungaji Peter Msigwa kumuomba radhi kwenye Magazeti na kulipa fidia ya Tsh. Bilioni 5 kwa kumkashifu na kumchafua jina
 
Mbowe amefanya vizuri sana, kwa hatua yake aliyochukua dhidi ya Mch. Peter Msigwa, sasa anaenda kubadilisha taswira nzima ya namna wanasiasa wetu wanavyofanya shughuli zao.

Ile tabia ya kuropoka hovyo uongo kila mwanasiasa anapokuwa kwenye majukwaa ya siasa, sasa ni dhahiri inakwenda kwisha, kuanzia sasa wakipanda majukwaani lazima wawe na facts za kuzungumza, sio uongo tena.
 
Moderator, tafadhali kwa heshima na taadhima, naomba Uzi huu ujitegemee, usiunganishwe. Nataka rafiki yangu Mch. Peter Msigwa au washauri wake wa karibu wauone kirahisi pengine naweza kumsaidia. Ni rafiki na ndugu yangu, akinisoma tu ananielewa kwa code zetu...

=====================================

Ndugu yangu na rafiki yangu Mch. Peter Msigwa;

Bwana Yesu Kristo apewe sifa...!

Ni kwanini umekubali shetani akuingize kwenye mtego rahisi lakini hatari kiasi hiki. Kwanini unajipeleka kwenye mauti ya kijinga hivi kama Jonathan wa kwenye Biblia....?

Fahamu kuwa, kuhama chama cha siasa na kujiunga na kingine wala siyo tatizo hapa......

Tatizo ni kukosa kwako kuenenda kwa hekima baada ya hapo. Na sasa ukikaa vibaya tu na ukishupaza shingo yako tu kwa sababu ya fahari ya dunia hii; pesa, umaarufu nk, nakuhakikishia jambo moja kuwa, unakwenda kuangamia kiroho na kimwili moja kwa moja muda si mrefu ...!

Mchungaji wangu hebu soma maandiko haya ktk Biblia yako👇;

Wagalatia 6:7-8 SUV‬
"......Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa cho chote apandacho mtu, ndicho atakachovuna. Maana yeye apandaye kwa mwili wake, katika mwili wake atavuna uharibifu; bali yeye apandaye kwa Roho, katika Roho atavuna uzima wa milele..."

Mchungaji wangu, usidanganyike, Mungu hadhihakiwi. Unachokipanda, ndicho unachovuna maana yeye Mungu keshasema hivyo.....

Nimeona "demand notice" uliyotumiwa na wanasheria wa uliyeamua kupambana naye. Ni ngumu kwako. Imeandaliwa kitaalamu kweli ikibeba kila shutuma na tuhuma zako.....

Nafsi na roho yangu mimi inaniambia, ulivuka mstari wa siasa zako na kuanza kumshambulia mtu. Na ni dhahiri kabisa kuwa, huna ushahidi wa tuhuma zako hizi......

Bahati mbaya kuwa, wewe unadhani ulikuwa unafanya siasa. Lakini siasa yako hukuiwekea mpaka kutenganisha kati ya freeman Mbowe - CHADEMA kama taasisi na Freeman Mbowe kama mtu binafsi, mwana familia na mfanyabiashara.....

Ukubali kuwa ulitoka kwenye kuishambulia taasisi na badala yake ukaanza kum - defame mtu binafsi. Kuuvuka mpaka huo ni lazima uingie kwenye mgogoro wa kisheria iwapo mtu huyo ataamua kukushughulikia. Na hivi ndivyo ilivyo Sasa......

Ushauri wangu ni huu. Ishinde AIBU na FEDHEHA kama mchungaji wako mkuu Yesu Kristo alivyoishinda aibu na fedheha ya msalaba. Soma Biblia yako 👇 👇 tena;

‭Waebrani 12:1-3 SUV‬
"........Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu, tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu. Maana mtafakarini sana yeye aliyeyastahimili mapingamizi makuu namna hii ya watendao dhambi juu ya nafsi zao, msije mkachoka, mkizimia mioyoni mwenu...."

Ukifanikiwa hili, omba tu radhi yaishe na endelea na siasa zako huko CCM lakini ukiwa na umakini zaidi safari hii......

Tumia hekima yako ya kichungaji kufanya siasa zako. Jifunze kwa wenzio kina Tundu Lissu. Wanajua kucheza mchezo ktk mpaka wa sheria za mchezo ndio maana watesi wake wakimpeleka kwenye sheria, huwashinda kirahisi au wenyewe huzitelekeza kesi.......

Watu aina ya Tundu Lissu wanajua kudhibiti midomo yao kuwaingiza ktk migogoro ya kisheria. Wewe sijui umepagawa na nini maana aada ya kuhama CHADEMA na kwenda huko umekuwa kama kichaa fulani asiye na udhibiti hata kama atafungwa kamba za mkatale kwani miropoko yako huishangaza dunia nzima......!

Mungu akubariki, akurehemu na akupe neema ya kukufungua ufahamu wako urudi katika hali yako ya kawaida....
nadhani mchungaji hana haja ya kuomba radhi kwa yeyote dhidi ya ukweli bayana aliubainisha dhidi ya mwamba wa kaskazini kuhusu wajibu wake binafsi katika kujinufaisha na rasilimali za chama kibinafsi...

Jambo la pili,
all the allegations and accusations are just politics statements and comments. there is no serious case at all on this, with my daed body 🐒
 
nadhani mchungaji hana haja ya kuomba radhi kwa yeyote dhidi ya ukweli bayana aliubainisha dhidi ya mwamba wa kaskazini kuhusu wajibu wake binafsi katika kujinufaisha na rasilimali za chama kibinafsi...

Jambo la pili,
all the allegations and accusations are just politics statements and comments. there is no serious case at all on this, with my daed body 🐒
Mjazeni ujinga tu alafu mtakuja muacha peke yake kizimbani

Ni bahati yake tu sometimes mahakama zinakuwa compromised ila hakika Msigwa angelipa hii fidia. Anajivunia sababu anajua ni simu tu zitatembea kwa majaji na serekali plus mahakama hazitafanya kitu
 
Mmeanza mambo yenu ya kiimani hapa sisi wana chadema tunataka majibu sahihi, aliyepo mtegoni ni mwenyekiti salama ni aachane na suala hili mara moja! na yeye ndiye aombe radhi kuwa kumtishia Bw. Msigwa!
Docs, zimeanza kukusanywa, pia fedha za join the chain zipo wapi?
 
Mbowe amefanya vizuri sana, kwa hatua yake aliyochukua dhidi ya Mch. Peter Msigwa, sasa anaenda kubadilisha taswira nzima ya namna wanasiasa wetu wanavyofanya shughuli zao.

Ile tabia ya kuropoka hovyo uongo kila mwanasiasa anapokuwa kwenye majukwaa ya siasa, sasa ni dhahiri inakwenda kwisha, kuanzia sasa wakipanda majukwaani lazima wawe na facts za kuzungumza, sio uongo tena.
Mch. Peter Msigwa anakosa hekima ya kufanya siasa zake......

CCM wamempagawisha kiasi cha kuwa kama kichaa asiye na udhibiti wowote hata kama mtamfunga mnyororo.....

Kuna wana - CHADEMA wengi very popular and influential wamehama chama mfano Dr Slaa, Dr Mashinji, Zito Kabwe, Dr Kitila Mkumbo na wengine...

Walisema waliyosema lakini walikuwa ktk ufahamu na akili zao.....

Walijua mipaka ya "hapa napiga siasa" na ule wa "hapa naingilia kushambulia mtu binafsi" na akiamua kunishughulikia kisheria, sitapona...

Huyu mchungaji yeye ni totally kupagawa. Hana hekima kabisa ya namna ya kuenenda....
 
nadhani mchungaji hana haja ya kuomba radhi kwa yeyote dhidi ya ukweli bayana aliubainisha dhidi ya mwamba wa kaskazini kuhusu wajibu wake binafsi katika kujinufaisha na rasilimali za chama kibinafsi...

Jambo la pili,
all the allegations and accusations are just politics statements and comments. there is no serious case at all on this, with my daed body 🐒
Mch. Msigwa ni mjinga, nimeona kwenye majibu yake kufuatia hatua ya Mbowe kwenda mahakamani ametumia maneno " a political problem, need a political solution".

Hizo quote huwa anapenda sana kuzitumia, lakini sidhani kama anajua kuzitafsiri maana yake.

Kwenye hiyo quote ya Mch. Msigwa, kwa haraka anadhani mahakamani ni uwanja wa siasa, hajui kama mahakamani ni uwanja wa sheria, unaohitaji ushahidi, sasa ngoja aende mahakamani na ngonjera zake za kisiasa akavune alichopanda.
 
Mch. Msigwa ni mjinga, nimeona kwenye majibu yake kufuatia hatua ya Mbowe kwenda mahakamani ametumia maneno " a political problem, need a political solution".

Hizo quote huwa anapenda sana kuzitumia, lakini sidhani kama anajua kuzitafsiri maana yake.

Kwenye hiyo quote ya Mch. Msigwa, kwa haraka anadhani mahakamani ni uwanja wa siasa, hajui kama mahakamani ni uwanja wa sheria, unaohitaji ushahidi, sasa ngoja aende mahakamani na ngonjera zake za kisiasa akavune alichopanda.
Mch. Msigwa ni mjinga, nimeona kwenye majibu yake kufuatia hatua ya Mbowe kwenda mahakamani ametumia maneno " a political problem, need a political solution".

Hii ni dalili ya Toba. Mwacheni atarudi tu kwenye mstari. Otherwise atakufa kifo cha kipumbavu kwelikweli kama kamanda wa Mfalme Daudi, Capt. Abneri....
 
Mch. Peter Msigwa anakosa hekima ya kufanya siasa zake......

CCM wamempagawisha kiasi cha kuwa kama kichaa asiye na udhibiti wowote hata kama mtamfunga mnyororo.....

Kuna wana - CHADEMA wengi very popular and influential wamehama chama mfano Dr Slaa, Dr Mashinji, Zito Kabwe, Dr Kitila Mkumbo na wengine...

Walisema waliyosema lakini walikuwa ktk ufahamu na akili zao.....

Walijua mipaka ya "hapa napiga siasa" na ule wa "hapa naingilia kushambulia mtu binafsi" na akiamua kunishughulikia kisheria, sitapona...

Huyu mchungaji yeye ni totally kupagawa. Hana hekima kabisa ya namna ya kuenenda....
Mch. Msigwa wanamtumia, anachofanya sio mapenzi yake.

Ndio maana hata siku ile akitambulishwa walimpa karatasi waliyomuandikia asome, badala ya Msigwa mwenyewe kuongea kile alichopanga.
 
Mch. Msigwa ni mjinga, nimeona kwenye majibu yake kufuatia hatua ya Mbowe kwenda mahakamani ametumia maneno " a political problem, need a political solution".

Hizo quote huwa anapenda sana kuzitumia, lakini sidhani kama anajua kuzitafsiri maana yake.

Kwenye hiyo quote ya Mch. Msigwa, kwa haraka anadhani mahakamani ni uwanja wa siasa, hajui kama mahakamani ni uwanja wa sheria, unaohitaji ushahidi, sasa ngoja aende mahakamani na ngonjera zake za kisiasa akavune alichopanda.
Mchungaji msigwa Yuko sahihi sana,

na mashtaka ya mbowe dhidi ya Msigwa are just political statements and comments, na hilo jibu la Msigwa kwamba masuala ya kisiasa yatatuliwe kisiasa ndio utakua uamuzi wa mahakama pia 🐒
 
Mjazeni ujinga tu alafu mtakuja muacha peke yake kizimbani

Ni bahati yake tu sometimes mahakama zinakuwa compromised ila hakika Msigwa angelipa hii fidia. Anajivunia sababu anajua ni simu tu zitatembea kwa majaji na serekali plus mahakama hazitafanya kitu
hakuna cha bahati wala kesi pale,

na huna haja ya kuanza kusense kushindwa tulia tu na urilax 🐒
 
Mch. Msigwa ni mjinga, nimeona kwenye majibu yake kufuatia hatua ya Mbowe kwenda mahakamani ametumia maneno " a political problem, need a political solution".

Hii ni dalili ya Toba. Mwacheni atarudi tu kwenye mstari. Otherwise atakufa kifo cha kipumbavu kwelikweli kama kamanda wa Mfalme Daudi, Capt. Abneri....
Ni kweli hiyo quote tayari inaonesha Mch. Msigwa ameanza kuweweseka, anatoa majibu ya kisiasa ili kutuonesha anajiamini, lakini kimsingi hilo ni jibu jepesi sana kimantiki.
 
Wenzake wanamcheka maana amekuwa Spika ya redio ya mbao akiambiwa sema hivi yeye hapo hapo anasoma na KUROPOKA
Honestly, that's very terrible....

Mtu unabaki kumshangaa na kujiuliza huyu ni mchungaji wa Kanisa la Mungu yupi ambaye hata hekima ya kawaida tu inampiga chenga....?
 
Wao wenyewe wakikutana huko hawana shida, ila wapambe wanavyohangaika sasa!
 
nadhani mchungaji hana haja ya kuomba radhi kwa yeyote dhidi ya ukweli bayana aliubainisha dhidi ya mwamba wa kaskazini kuhusu wajibu wake binafsi katika kujinufaisha na rasilimali za chama kibinafsi...

Jambo la pili,
all the allegations and accusations are just politics statements and comments. there is no serious case at all on this, with my daed body 🐒
There is no serious case at all if you think on that perspective why you vagabonds and hooligans are crying herein as if you have been sued while you are not privy to the matter at issue, my advice to you and your fellow goons it is better you stay quiet to wait court determination, otherwise I urge you to keep clapping hands for your failed leaders of your dead party turned abductor.
 
Mmeanza mambo yenu ya kiimani hapa sisi wana chadema tunataka majibu sahihi, aliyepo mtegoni ni mwenyekiti salama ni aachane na suala hili mara moja! na yeye ndiye aombe radhi kuwa kumtishia Bw. Msigwa!
Docs, zimeanza kukusanywa, pia fedha za join the chain zipo wapi?
Akishindwa kufuata ushauri huu rahisi na wa hekima, majibu hayo labda mtayapata huko mahakamani baada ya kumsaidia kuwasilisha tuhuma zake hizo zenye ushahidi usio na shaka....

Lakini kumbuka mwenzako anajitetea hivi huko kwa Sasa, akisema;

"....a political problem, needs a political solution..."

Kama lugha hii inakupiga chenga, basi tafsiri isiyo rasmi ya kiswahili alichosema champion wenu ni;

"....matatizo na tuhuma za kisiasa zinapaswa kujibiwa kisiasa..."

Unaona jamaa asivyo na akili? Yaani una - defame watu huko halafu udai hilo ni tatizo la kisiasa...?

Mtu kama huyu unadhani anataka majibu gani kama siyo kuwa ameamua kuwa mzushi na mwongo tu...?

By the way, ninyi mnaotoa hizo tuhuma dhidi ya Freeman Mbowe na CHADEMA ni kwanini hamtoi na huo ushahidi kuthibitisha tuhuma zenu...?

Au hiyo ndiyo maana ya kauli ya mchungaji kuwa, "a political problem, needs a political solution...??"

Yaani mnataka Freeman Mbowe atoke kujibu uzushi kwa njia anayotumia Peter Msigwa? Really?
 
Ushauri mzuri kwa anayesikia. Shutuma za kweli kwa mafisadi haziwezi kulinganishwa na shambulio la Mtu binafsi au taasisi bila ushahidi.
Ni kweli...

Inauma na kushangaza kwani bado anajitetea kuwa yeye alikuwa anafanya siasa na hivyo Freeman Mbowe asikimbilie mahakamani na badala yake ajibizane naye kisiasa hivyohivyo...

Inashangaza kuwa kauli inatoka kwa "mchungaji wa Kanisa la Mungu aliye hai...!"
 
Back
Top Bottom