Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,242
- 34,903
Mbunge wa viti maalumu wa Mkoa wa Singida (CHADEMA) Mhe Jesca Kishoa, amepata ajali Dodoma muda wa saa nne, hali yake ni mbaya.
Tutawajuza kinachoendelea
==========
Dodoma. Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Jesca Kishoa amelazwa hospitali ya Bunge jijini Dodoma baada ya kupata ajali ya gari leo asubuhi Mei 11, 2018 wakati akienda bungeni.
Akizungumza na Mwananchi amesema; “Hapa nimelazwa hospitali ya Bunge, nasikia maumivu katika mguu wa kulia lakini naendelea vizuri.”
“Nimechomwa sindano ya kutuliza maumivu na ninaendelea vyema,” amesema Kishoa mke wa mbunge wa zamani wa Kigoma Kusini, David kafulila
Kuhusu mazingira ya ajali, Kishoa amesema; “katika mataa ya pale Area D, taa zilivyoruhusu, yule wa mbele yangu hakuwa ameonyesha kama atakata kona, sasa alivyokata kwa ghafla, mimi kufunga breki kwa nguvu ikafeli, nikaigonga kwa nyuma.
Chanzo: Mwananchi
Tutawajuza kinachoendelea
==========
Dodoma. Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Jesca Kishoa amelazwa hospitali ya Bunge jijini Dodoma baada ya kupata ajali ya gari leo asubuhi Mei 11, 2018 wakati akienda bungeni.
Akizungumza na Mwananchi amesema; “Hapa nimelazwa hospitali ya Bunge, nasikia maumivu katika mguu wa kulia lakini naendelea vizuri.”
“Nimechomwa sindano ya kutuliza maumivu na ninaendelea vyema,” amesema Kishoa mke wa mbunge wa zamani wa Kigoma Kusini, David kafulila
Kuhusu mazingira ya ajali, Kishoa amesema; “katika mataa ya pale Area D, taa zilivyoruhusu, yule wa mbele yangu hakuwa ameonyesha kama atakata kona, sasa alivyokata kwa ghafla, mimi kufunga breki kwa nguvu ikafeli, nikaigonga kwa nyuma.
Chanzo: Mwananchi