Mbeya Cement Company LTD yatoa gawio la Tsh bilioni 3 kwa Serikali

The Sunk Cost Fallacy 2

JF-Expert Member
Nov 8, 2022
8,759
10,207
Kampuni ya Mbeya Cemetent Kwa mara ya kwanza imetangaza kutoa Gawio kwa wana hisa wake ikiwemo Serikali na NSSF kufuatia kuanza kupata faida ,hii ni baada ya hasara ya miaka 10 mfululizo.

Hatua hii imefikiwa baada ya Kazi kubwa ikiyofanywa na Serikali ya Rais Samia Kupitia Msajili wa Makampuni kuunda Uongozi Mpya na kuifutia Madeni ya nyuma.

Aidha kampuni hii Sasa inamilokiwa na wazawa yaani Amsons Group , Serikali(Hazina) na NSSF.

View: https://www.instagram.com/p/C7zIQYpKhnk/?igsh=MWE4ajRwYTk4MnJjNA==

---
SERIKALI kupitia msajili wa hazina inatarajia kupokea Sh bilioni 3 za gawio kutoka katika kampuni ya Mbeya Cement Company Limited (MCCL) kutokana na umiliki wake wa asilimia 25 ya hisa zake.

Sambamba na hilo, kampuni hiyo pia imetangaza gawio la Sh 4,259 kwa kila hisa ambayo ni marejesho yaliyosubiriwa kwa muda mrefu.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na kampuni hiyo imeeleza kuwa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), mmiliki wa asilimia 10, ulitarajiwa kupata Sh bilioni 1.2 za gawio.

"Gawio hili kubwa linakuja kama msukumo wa kukaribishwa, likionyesha ufanisi mzuri wa kifedha wa kampuni na uwezo wa baadaye," inasomeka sehemu nyingine ya taarifa hiyo.

Hifadhi kubwa za migodi ya kampuni na uwezo wa kuongeza uzalishaji wa klinka vilikuwa vipengele muhimu, "pamoja na mkutano ukisisitiza haja ya uwekezaji wa kimkakati ili kuongeza matumizi ya rasilimali hizi.

"Uplift ya kifedha ya hivi karibuni ilisaidiwa zaidi na makubaliano muhimu yaliyofikiwa Novemba 2023, ambayo yalibadilisha mkopo uliopo kutoka Cemasco Limited, kupunguza mzigo wa madeni ya kampuni na kuruhusu uwekezaji upya katika maeneo ya ukuaji.

"Hivi sasa inashikilia asilimia sita ya soko, MCCL iko tayari kupanuka. Usimamizi wa kampuni unazingatia kuboresha mikakati ya vifaa na masoko ili kuhifadhi wateja waliopo na kuvutia wapya," inasomeka sehemu nyingine ya taarifa hiyo.

Chanzo: Habari Leo

My Take
Kazi nzuri ya Rais Samia aliposema atafuta na kuunganisha mashirika yote ya Umma yanayoleta hasara ,haya Sasa ndio sehemu tuu ya matunda yake.

Huu ni uji tu, nyama ziko chini. Hater wa Samia mpo?
 
Kampuni ya Mbeya Cemetent Kwa mara ya kwanza imetangaza kutoa Gawio Kwa Wana hisa wake ikiwemo Serikali na NSSF kufuatia kuanza kupata faida ,hii ni baada ya hasara ya miaka 10 mfululizo...
Hii nchi raha sana ukiweza kupenyeza kwenye pillars za nchi unaweza hata kuwapinga wanaosema Tanzania ni miongoni mwa nchi maskini kabisa duniani! Yaani ukiwa Serikalini unaonaje kwamba hakuna hela, huku mikopo inaingia,tozo zinaingia, gawio zinasoma, hela zinazoenda mikoani mnarudishiwa Serikalink kwamba hazina kazi!!! Yaan hela zinaingia na hakuna pakuzipeleka.

Viongozi wamekosa tu exposure na hawajui lugha ya kiingereza vizuri vinginevyo kila siku wangekuwa wanaenda BAHAMAS, MALDIVES, VENICE nk kuenjoy, shida lugha tu basi. Hela kama hizo zinaingia tu na ukichomoa kidogo hata CAG akikuona hakuna utakachofanywa😂😂
 
Safi sana .utashangaa CHADEMA wanapinga habari hii nzuri kabisa na kusema takwimu zimepikwa. Aliyewaroga CHADEMA aliwaonea sana maana hakukuwa na haja wala sababu ya kuwafanyia hivyo ,kwa kuwa walikuwa tayari wana matatizo yanayohitaji msaada wa kisaikolojia.
Mbona wewe ndo unatakiwa kuwepo Hospital ya magonjwa ya akili pale Mirembe-Dodoma.
 
Hii nchi raha sana ukiweza kupenyeza kwenye pillars za nchi unaweza hata kuwapinga wanaosema Tanzania ni miongoni mwa nchi maskini kabisa duniani! Yaani ukiwa Serikalini unaonaje kwamba hakuna hela, huku mikopo inaingia,tozo zinaingia, gawio zinasoma, hela zinazoenda mikoani mnarudishiwa Serikalink kwamba hazina kazi!!! Yaan hela zinaingia na hakuna pakuzipeleka.

Viongozi wamekosa tu exposure na hawajui lugha ya kiingereza vizuri vinginevyo kila siku wangekuwa wanaenda BAHAMAS, MALDIVES, VENICE nk kuenjoy, shida lugha tu basi. Hela kama hizo zinaingia tu na ukichomoa kidogo hata CAG akikuona hakuna utakachofanywa😂😂
Soma kiswahili uelewe vizuri 👇👇

View: https://www.instagram.com/p/C7zIQYpKhnk/?igsh=MWE4ajRwYTk4MnJjNA==
 
Kuna uji unaliwa na nyama? Nyie machawa!
Kampuni ya Mbeya Cemetent Kwa mara ya kwanza imetangaza kutoa Gawio kwa wana hisa wake ikiwemo Serikali na NSSF kufuatia kuanza kupata faida ,hii ni baada ya hasara ya miaka 10 mfululizo.

Hatua hii imefikiwa baada ya Kazi kubwa ikiyofanywa na Serikali ya Rais Samia Kupitia Msajili wa Makampuni kuunda Uongozi Mpya na kuifutia Madeni ya nyuma.

Aidha kampuni hii Sasa inamilokiwa na wazawa yaani Amsons Group , Serikali(Hazina) na NSSF.

View: https://www.instagram.com/p/C7zIQYpKhnk/?igsh=MWE4ajRwYTk4MnJjNA==

---
SERIKALI kupitia msajili wa hazina inatarajia kupokea Sh bilioni 3 za gawio kutoka katika kampuni ya Mbeya Cement Company Limited (MCCL) kutokana na umiliki wake wa asilimia 25 ya hisa zake.

Sambamba na hilo, kampuni hiyo pia imetangaza gawio la Sh 4,259 kwa kila hisa ambayo ni marejesho yaliyosubiriwa kwa muda mrefu.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na kampuni hiyo imeeleza kuwa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), mmiliki wa asilimia 10, ulitarajiwa kupata Sh bilioni 1.2 za gawio.

"Gawio hili kubwa linakuja kama msukumo wa kukaribishwa, likionyesha ufanisi mzuri wa kifedha wa kampuni na uwezo wa baadaye," inasomeka sehemu nyingine ya taarifa hiyo.

Hifadhi kubwa za migodi ya kampuni na uwezo wa kuongeza uzalishaji wa klinka vilikuwa vipengele muhimu, "pamoja na mkutano ukisisitiza haja ya uwekezaji wa kimkakati ili kuongeza matumizi ya rasilimali hizi.

"Uplift ya kifedha ya hivi karibuni ilisaidiwa zaidi na makubaliano muhimu yaliyofikiwa Novemba 2023, ambayo yalibadilisha mkopo uliopo kutoka Cemasco Limited, kupunguza mzigo wa madeni ya kampuni na kuruhusu uwekezaji upya katika maeneo ya ukuaji.

"Hivi sasa inashikilia asilimia sita ya soko, MCCL iko tayari kupanuka. Usimamizi wa kampuni unazingatia kuboresha mikakati ya vifaa na masoko ili kuhifadhi wateja waliopo na kuvutia wapya," inasomeka sehemu nyingine ya taarifa hiyo.

Chanzo: Habari Leo

My Take
Kazi nzuri ya Rais Samia aliposema atafuta na kuunganisha mashirika yote ya Umma yanayoleta hasara ,haya Sasa ndio sehemu tuu ya matunda yake.

Huu ni uji tu, nyama ziko chini. Hater wa Samia mpo?
 
Inafutiwa madeni ya nyuma kisha ina toa gawio. Kwanini asilipe madeni ya nyuma, na kama hawawezi makampuni yawe na insurance ziwalipie madeni wanaposhindwa hii ni ghiliba, hatuwezi kuendelea kwa mtindo huu.
 
hizo hela zionekane basi indirectly kwenye miradi na maendeleo,mbona mambo ni yapo AUTOPILOT!?
Unaropoka kama punguani,Kwa hiyo hela Zinaenda wapi? Kipi unakijua kuhusu miradi hapa Tanzania?

Kuna sekta Haina miradi? Mkoani kwako hakuna miradi ya Maendeleo? Autopilot ndio nini?
 
Inafutiwa madeni ya nyuma kisha ina toa gawio. Kwanini asilipe madeni ya nyuma, na kama hawawezi makampuni yawe na insurance ziwalipie madeni wanaposhindwa hii ni ghiliba, hatuwezi kuendelea kwa mtindo huu.
Debt restructuring,haijafutiwa Jana Wala juzi Bali miaka 3 iliyopita Ili ijipange na ndio maana Sasa imeanza kuoga faida maana miaka yote hiyo hakuna faida walipata na Madeni Juu.
 
Hiking ni kile kiwanda kikubwa Cha cement kilichoko songwe?Hiking sikilikuwaga kimebinafsisshwa kwa wasouth Africa kama ilivyo Tanga cement?
 
Back
Top Bottom