the guardian 17
JF-Expert Member
- Aug 15, 2024
- 353
- 515
Kutokana na mkutano wa nishati wa viongozi wa Afrika barabara zikafungwa, kazi zikasitishwa, wanafunzi wakasalia majumbani. Tukayaficha matatizo ya jiji la Dar es salaam kwa muda. Ingawa nayo ilituchoresha kwa kuonesha namna gani hatuna miundombinu ya kutosha hadi kusitisha baadhi ya huduma.
Leo changamoto zimerudi palepale, foleni ndefu, adha ya usafiri kwa wanafunzi, msongamano kwenye vyombo vya usafairi wa umma.
Nadhani sasa ni wakati wa kuboresha miundombinu tuliyonayo kwa kiwango kikubwa kuendana na kasi ya ukuaji wa Jiji hili la hekaheka, na kibiashara ili tuachane na hizi mambo za kuficha matatizo kwa muda ukija ugeni mkubwa kwa kujidanganya kuwa hayapo.
Leo changamoto zimerudi palepale, foleni ndefu, adha ya usafiri kwa wanafunzi, msongamano kwenye vyombo vya usafairi wa umma.
Nadhani sasa ni wakati wa kuboresha miundombinu tuliyonayo kwa kiwango kikubwa kuendana na kasi ya ukuaji wa Jiji hili la hekaheka, na kibiashara ili tuachane na hizi mambo za kuficha matatizo kwa muda ukija ugeni mkubwa kwa kujidanganya kuwa hayapo.