Marejeo ya Simba na Al Ahly Tripoli dimba la Benjamin Mkapa

Kinau Michael

Member
Aug 18, 2023
7
12
Je, Simba anaweza kumfunga AA Tripoli kwa Mkapa?

Simba SC Tanzania inarejea Lupasa kwa Mkapa ikiwa inahitaji ushindi ili kutinga hatua ya makundi michuao ya Klabu Bingwa Afrika huku wengi wakiwa na matumaini kuwa inaweza ikafanya hivyo bila ubishi kutokana na rekodi yake katika uwanja huo.

Timu nyingi kubwa zikija kucheza na Simba SC Tanzania zimekuwa zikishindwa kupata matokeo hapo na hiii ndio jeuri ya mashabiki wengi wa klabu hiyo kuelekea mchezo huo.

Ni wazi kuwa kuna makosa mengi yamefanya na Simba SC Tanzania wakiwa katika mechi yao ugenini hasa kupoteza nafasi walizotengeneza kipindi cha kwanza na muda mwingi kupoteza mipira (kukosa umakini), haya ni makosa ambayo hawapaswi kuyarudia mchezo ujao wakiwa nyumbani

Historia ya wao kufanya vizuri diba la nyumbani isiwe kigezo cha wao kubweteka na kuamini kuwa wanaweza kupita bila kufanyia marekebisho makosa waliyofanya kwani historia hiyo hiyo inaweza kuwahukumu kama ilivyokuwa hivyo kwa UD Songo waliopata sare na kusonga mbele.

Jwaneng Galaxy pia wamewahi kusitisha ndoto za Simba SC Tanzania dimba la Mkapa kwa kuwatandika bao tatu licha ya ushindi waliopata ugenini.

NI HAYO TU KWA SASA
 
Kocha wa Simba ni mdogo timu kubwa.
Simba ikishinda kwa Mkapa basi ni kwa presha na hamasa za mashabiki na si kwa mbinu za kocha.
Tatizo letu mashabiki wa Bongo tunaamini tutashinda tu kila mechi. Yale mazingira ni hostile huwezi kucheza mpira wako na hauwezi kushinda kirahisi. Nakuhakikishia hata kama angeenda Al ahly pale asingeshinda kirahisi. Ubaya mwingine ni kulinganisha Simba na Yanga. Kwakuwa yanga kashinda ugenini basi na simba angetakiwa kushinda. Haiko hivyo kila mtu ashinde mechi zake

Unadhani ni nini kinamfanya Ahly akija Dar hashindi kirahisi? Unadhan ni ubora wa timu zetu? Mazingira huwa magumu sana kwake;

Droo yalikuwa matokeo mazuri mno kwa simba wanachotakiwa kufany sasa ninkuandaa mkakati wa game 2 hapa nyumbani.
 
kwa bongo ni Yanga tu ndio wenye uwezo wa kushinda nje ndani.ukubwa wa Simba Africa uko wapi kama kushinda ugenini sio muhimu!
 
kwa bongo ni Yanga tu ndio wenye uwezo wa kushinda nje ndani.ukubwa wa Simba Africa uko wapi kama kushinda ugenini sio muhimu!
Na hili ndio tatizo na umasikini wa watanzania. Huwezi kujiongelea wewe bila kumtaja mdogo wako. Penye kutaja simba taja simba sio urelate na yanga.

Hauoni positives zozote kwa kudhani yanga ni bora sana. Kwa taarifa mpira wa jana Simba kupata ile droo ilikuwa kitu bora kwao. There is the second leg to play.
 
Hiyo CBE na Vital'O ndiyo za kujigamba kushinda ugenini?
Timu hazina hata mashabiki serious halafu mnajinasibu kuwa nyie mnashinda ugenini?
Halafu kitu anatakiwa kukumbushwa hawa jamaa 2022 walifika semi final ya Confederation na sasa wameimarisha sana kikosi chao. Sio wepesi kama mashabiki ambavyo wangefikiri. Wana fanbase kubwa na wana wachezaji wa maana kweli kweli.
 
kwaio kusema ukweli ni kosa?
 
JF ni jukwaa la great thinkers. Ungetaka kuanzisha uzi wa Yanga ungeanzisha separate. This is too low.

Kwenye uzi huu tungetaraji ijadiliwe Simba tu. Zaidi ya hapo kunakuwa hakuna maana ya kujadili uzi huu
mtu kacomment Simba kushinda ugenini sio issue wakati Tanzania ipo timu ya Yanga Africa inashinda nje ndani.
sasa hapo nimekosea nini?
 
Hiyo CBE na Vital'O ndiyo za kujigamba kushinda ugenini?
Timu hazina hata mashabiki serious halafu mnajinasibu kuwa nyie mnashinda ugenini?
Kuna watu ikipita wiki tu, vichwa vyenu huwa vinafuta memory yote ya nyuma???

Mwaka juzi Yanga imecheza FAINALI ya Hilo shirikisho na ilikuwa inashinda nje ndani.

Mwaka jana, robo FAINALI Simba imepangwa na Al Ahly wakashangilia kinoma halafu wakachabangwa nje ndani
 
Rekebisha kwanza hapo kwenye bold...!!
Michuano ipi ya club bingwa anayoshiriki 5imba?
 
Hiyo CBE na Vital'O ndiyo za kujigamba kushinda ugenini?
Timu hazina hata mashabiki serious halafu mnajinasibu kuwa nyie mnashinda ugenini?
Kutokukubali makosa kutawafanya mbaki shirikisho na kutoa droo kila kukicha..!! We timu gani kwenye mchezo wote wa dakika 90 haina shuti lililolenga lango hata moja..!! Halafu unarudi hapa kumsema aliyeko club bingwa na kumlinganisha na wa KOMBE LA WALIOFELI..!!
 
kwa bongo ni Yanga tu ndio wenye uwezo wa kushinda nje ndani.ukubwa wa Simba Africa uko wapi kama kushinda ugenini sio muhimu!
SIMBA alishinda ugenini dhidi ya AS Vita ya Congo bao moja la Penati, amewahi kushinda mechi bao 3-1 (C.D Primeiro de Agosto 1-3 Simba SC Tanzania) so bado anaweza kushinda ugenini pia inategemea na maandalizi aliyofanya pamoja na mbinu anazokwenda nazo katika mchezo husika
 
Simba nipeni timu mimi mbona mtafurahi.
wachezaji wote nitawanyoa vipara,Kibu kipara,Awesu kipara,Che malone kipara.
viatu over size kama wadudu wa Arusha.
nitakua kocha wa kwanza mwenye uthubutu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…