KERO Manispaa ya Morogoro rekebisheni taa, swichi na feni katika Soko Kuu la Chifu Kingalu hazifanyi kazi

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Bado Hujasema

Member
Dec 1, 2024
10
12
IMG-20241208-WA0039.jpg

Mimi ni Mfanyabiashara wa Soko Kuu la Chifu Kingalu ambalo lipo Manispaa ya Morogoro, katika soko hili kuna changamoto kubwa hasa kuharibika kwa taa, swichi za feni pamoja na masinki ya kunawia mikono.

Tangu soko lifunguliwe Mwaka 2020 halijawahi kufanyaiwa ukarabati, hivyo taa haziwaki mpaka tunahofia mali zetu kuibiwa hasa nyakati za usiku.

Kwa upande wa masinki ni mabovu mpaka yanasababisha maji hayapiti vizuri, hii ni mbaya sana ukiangalia soko hili ni kubwa na watumiaji ni wengi, pasipokarabatiwa hali itazidi kuwa mbaya sana.

IMG-20241208-WA0036.jpg
IMG-20241208-WA0038.jpg

Tumejaribu kuulizia kuwa ni gharama kiasi gani zinaweza kutumika katika kukarabati vitu vyote hivyo, ambapo tumeambiwa ni shilingi laki 8 tu za kitanzania zinaweza kuweka mazingira sawa hapa.

Lakini tunashangaa kwanini hapakarabatiwi na kibaya zaidi tumeomba kufanyiwe ukarabati.

Hapa sokoni kwa mwezi zinakusanywa Shilingi milioni 74 kwa ajili ya mapato, hivi kweli laki 8 inashindikana kutolewa ili pawe salama humu ndani?

Tunauomba Uongozi wa Manispaa ya Morogoro kuangalia hili suala maana tushaomba sana ukarabati ufanyike lakini mpaka sasa hakuna utekelezaji, hii ni mbaya sana.

Soko limeshafikisha miaka minne mpaka sasa lakini hamna maboresho hayo mapato yanayoingizwa ni ya nini mwisho wa siku lije nipoteze mvuto watu wahame humu mapato yakosekane tuwe na utaratibu wa kuvipenda vitu vinavyotuingizia fedha.

IMG-20241208-WA0032.jpg
IMG-20241208-WA0030.jpg

IMG-20241208-WA0033.jpg
IMG-20241208-WA0031.jpg
 

Attachments

  • IMG-20241208-WA0037.jpg
    IMG-20241208-WA0037.jpg
    73.9 KB · Views: 8
  • IMG-20241208-WA0034.jpg
    IMG-20241208-WA0034.jpg
    51.3 KB · Views: 5
  • IMG-20241208-WA0035.jpg
    IMG-20241208-WA0035.jpg
    56 KB · Views: 6
  • IMG-20241208-WA0029.jpg
    IMG-20241208-WA0029.jpg
    53.1 KB · Views: 6
Nchi hii miradi ikikamilika watu wanawaza kuvuna pesa tu kukarabati aaaa!

Ni sawa na mabasi ya mwendo kasi walikuwa wanafurahia kuvuna mabilioni ya nauli za wananchi tu ila kununua mabasi mapya aaah.

Yani kuna ya mambo ya hovyo

Hivi watu wanavyotafuta nyadhifa na ajira inakuwaje kuna watu wako ofisini hawazingatii weledi, wanajifanya hawajui kuna watu wanataka viti walivyokalia, hawaogopi hata kidogo wakawa watu wenye wakawajibika.
 
Back
Top Bottom