Mamlaka ya vitambulisho vya taifa NIDA mmenyoka sana hadi raha mitano tena

kajamaa kadogo

JF-Expert Member
Nov 2, 2018
2,708
6,428
Kulikuwa na malalamiko sana kwenye mamlaka hii maana kila kijana ukimkuta kijiweni lawama kwa NIDA ila hali mnavyoenda nayo kiukweli niwape maua yenu๐Ÿ’๐Ÿ’๐Ÿ’๐Ÿ’๐Ÿ’๐Ÿ’

Jamaa wangu alipeleka maombi tarehe 01 january hii ya juzi yaani mpaka tarehe kumi tu namba na kitambulisho tayari

Hongera nida hongera masauni
 
Japo waswahili wana msemo wao kufa usifiwe mimi nataka niwape maua kabla hamjafa๐Ÿ”ฅ
20240930_085847.jpg
 
Wale ambao walichelewa kuchukua vitambulisho vya ukienda kuchukua unakuta kitambusho kimechakaa, kwa kwa nini wasiweke vitambulisho vya watu individual kuliko kuvichanganya kama noti, hawaoni kuwa vinasagana na kuchakaa pale wanapotafuta cha mtu?
 
Muda waliouweka wa kuchukua vitambulisho kwa wale wanaotumia namba ni mwezi mmoja hautoshi. Watu wako mbali sana na walikojiandikisha. Walipaswa kuweka muda mrefu ili mtu ajiandae vema kusafiri kwenda mkoa alikojiandikisha kuchukua kitambulisho chake. Ishu ni nauli kubwa kusafiri. Unakuta mtu alijiandikisha mkoani kilimanjaro akahamia mtwara kabla kitambulisho kutoka. Kutoka mtwara mpaka moshi ni shughuli pevu ndani ya mwezi mmoja
 
Kulikuwa na malalamiko sana kwenye mamlaka hii maana kila kijana ukimkuta kijiweni lawama kwa NIDA ila hali mnavyoenda nayo kiukweli niwape maua yenu๐Ÿ’๐Ÿ’๐Ÿ’๐Ÿ’๐Ÿ’๐Ÿ’

Jamaa wangu alipeleka maombi tarehe 01 january hii ya juzi yaani mpaka tarehe kumi tu namba na kitambulisho tayari

Hongera nida hongera masauni
Wewe kapuku kweli,mitano tena ๐Ÿค”๐Ÿค”๐Ÿค”๐Ÿค”๐Ÿค”
 
Wale ambao walichelewa kuchukua vitambulisho vya ukienda kuchukua unakuta kitambusho kimechakaa, kwa kwa nini wasiweke vitambulisho vya watu individual kuliko kuvichanganya kama noti, hawaoni kuwa vinasagana na kuchakaa pale wanapotafuta cha mtu?
kwahiyo unashauri vipigwe lamination๐Ÿคฃ
 
Back
Top Bottom