Makonda ni karata muhimu CCM kwa jimbo la Arusha mjini 2025. Anafaa kupewa jimbo.

Matongee

JF-Expert Member
Jun 17, 2023
1,044
2,645
Katika majimbo yanayoleta changamoto kubwa kwa CCM nyakati za uchaguzi ni jimbo la Arusha mjini. Kibaya zaidi changamoto kubwa huwa ni ndani ya CCM kwenyewe wakati wa kupata mgombea ubunge kupitia CCM. Kwa utafiti wangu binafsi nadhani CCM Arusha ndo imejaa mamluki wengi sana wa CHADEMA kuliko majimbo mengine. WanaCCM ambao husaidia CHADEMA kisirisiri wapo sana ndani ya CCM Arusha.

Hii hitilafu ndani ya chama husababisha mgombea wa CCM kuwa dhaifu dhidi ya mgombea wa kudumu wa CHADEMA ndugu Godbless Lema. Nimetamka mgombea wa kudumu kwa sababu ndani ya CHADEMA kuna watu ni kama wamiliki wa hizo nafasi za kugombea ubunge. Lema, Heche, Sugu, Wenje, Pumbulu, Mbowe, Msigwa na Mnyika ni wagombea wa kudumu kwenye majimbo yao.

CCM Arusha hadi sasa sijaona kada mwenye nguvu za kisiasa kumkabili mgombea wa kudumu Lema. Mbunge Gambo anamalizia muda wake kwasababu haitawezekana kwa yeye kugombea tena Arusha. Ni mfitini asiyetakiwa hata na CCM Arusha. Meya wa jiji, Max Iranqhe naona naye anapambana kujiweka sawa lakini kiukweli kisiasa bado ni mchanga. Amekaa kiutendaji zaidi. Alberto Msando yuko vizuri kisiasa ila naye anatajwa tajwa kwenye mambo yasiyo mazuri hivyo wapinzani kumbomoa ni rahisi. Mzee Monaban kashapoteza mvuto baada ya kushindwa mara kadhaa. Mwenezi Bananga bado nguvu yake ngazi ya jimbo zima ni ndogo.

Kwa sasa mwenye nguvu kisiasa kuliko mwanasiasa yeyote ndani ya Arusha ni RC Makonda. Mambo yake anayofanya yanamweka karibu sana na wapiga kura. Kama akiendelea hivi hadi 2025 basi CCM impitishe kugombea Arusha mjini.
 
Mkuu Matongee tafadhali usichanganye uongozi wa kuteuliwa na wa kuchaguliwa. Unaweza kuwa kiongozi wa kuteuliwa maarufu lakini usifue dafu kwenye uchaguzi. Mara nyingi tu, viongozi waandamizi wa kuteuliwa hupoteza uchaguzini.

Kama kuwa maarufu [kwa wema au kwa ubaya], Makonda wa Dar alikuwa maarufu kuliko huyo wa Arusha. Unakumbuka kilichotokea alipojaribu kugombea jimbo mojawapo la Dar? Huo umaarufu wa viongozi wa kuteuliwa huchagizwa na maigizo yao mbele ya kamera.

Uchaguzi ni kitu kingine kabisa. Wakuu wa mikoa, wilaya na wengineo ambao ni maarufu hupigwa mweleka kirahisi sana....usikariri!
 
Screenshot_20231102_120808_Remix.png
 
Katika majimbo yanayoleta changamoto kubwa kwa CCM nyakati za uchaguzi ni jimbo la Arusha mjini. Kibaya zaidi changamoto kubwa huwa ni ndani ya CCM kwenyewe wakati wa kupata mgombea ubunge kupitia CCM. Kwa utafiti wangu binafsi nadhani CCM Arusha ndo imejaa mamluki wengi sana wa CHADEMA kuliko majimbo mengine. WanaCCM ambao husaidia CHADEMA kisirisiri wapo sana ndani ya CCM Arusha.

Hii hitilafu ndani ya chama husababisha mgombea wa CCM kuwa dhaifu dhidi ya mgombea wa kudumu wa CHADEMA ndugu Godbless Lema. Nimetamka mgombea wa kudumu kwa sababu ndani ya CHADEMA kuna watu ni kama wamiliki wa hizo nafasi za kugombea ubunge. Lema, Heche, Sugu, Wenje, Pumbulu, Mbowe, Msigwa na Mnyika ni wagombea wa kudumu kwenye majimbo yao.

CCM Arusha hadi sasa sijaona kada mwenye nguvu za kisiasa kumkabili mgombea wa kudumu Lema. Mbunge Gambo anamalizia muda wake kwasababu haitawezekana kwa yeye kugombea tena Arusha. Ni mfitini asiyetakiwa hata na CCM Arusha. Meya wa jiji, Max Iranqhe naona naye anapambana kujiweka sawa lakini kiukweli kisiasa bado ni mchanga. Amekaa kiutendaji zaidi. Alberto Msando yuko vizuri kisiasa ila naye anatajwa tajwa kwenye mambo yasiyo mazuri hivyo wapinzani kumbomoa ni rahisi. Mzee Monaban kashapoteza mvuto baada ya kushindwa mara kadhaa. Mwenezi Bananga bado nguvu yake ngazi ya jimbo zima ni ndogo.

Kwa sasa mwenye nguvu kisiasa kuliko mwanasiasa yeyote ndani ya Arusha ni RC Makonda. Mambo yake anayofanya yanamweka karibu sana na wapiga kura. Kama akiendelea hivi hadi 2025 basi CCM impitishe kugombea Arusha mjini.
Wa Arusha hawacheki na nyani linapokuja suala la kuchagua.
Wana vina saba na kenya sjui kama unajua kinachoendelea kenya
 
Wa Arusha hawacheki na nyani linapokuja suala la kuchagua.
Wana vina saba na kenya sjui kama unajua kinachoendelea kenya
Enzi hizo .....ila siku hizi wanakua na mambo ya vijana wa pwani,,,,,Chuga yenye ufanano na Kenya ilishajifiaga enzi hizo za wakina xplastaz,,,.........walipoanza kujimix na watoto wa dasalama kwisha kazi
 
Mkuu Matongee tafadhali usichanganye uongozi wa kuteuliwa na wa kuchaguliwa. Unaweza kuwa kiongozi wa kuteuliwa maarufu lakini usifue dafu kwenye uchaguzi. Mara nyingi tu, viongozi waandamizi wa kuteuliwa hupoteza uchaguzini.

Kama kuwa maarufu [kwa wema au kwa ubaya], Makonda wa Dar alikuwa maarufu kuliko huyo wa Arusha. Unakumbuka kilichotokea alipojaribu kugombea jimbo mojawapo la Dar? Huo umaarufu wa viongozi wa kuteuliwa huchagizwa na maigizo yao mbele ya kamera.

Uchaguzi ni kitu kingine kabisa. Wakuu wa mikoa, wilaya na wengineo ambao ni maarufu hupigwa mweleka kirahisi sana....usikariri!
Mimi ni mzoefu sana kwenye haya mambo. 2020 Makonda alikosea sana kwenda Kigamboni kugombea kwasababu alikuwa hana misuli ya kisiasa huko na pia JPM alishamtosa. Ila kwa sasa Makonda ni wa moto mno anakubalika na wapiga kura wengi.
 
Wa Arusha hawacheki na nyani linapokuja suala la kuchagua.
Wana vina saba na kenya sjui kama unajua kinachoendelea kenya
Arusha mjini hakuna siasa kali zenye misimamo ukilinganisha na jimbo kama la Karatu. Watu wa Arusha hubadilika badilika.
 
Mkuu Matongee tafadhali usichanganye uongozi wa kuteuliwa na wa kuchaguliwa. Unaweza kuwa kiongozi wa kuteuliwa maarufu lakini usifue dafu kwenye uchaguzi. Mara nyingi tu, viongozi waandamizi wa kuteuliwa hupoteza uchaguzini.

Kama kuwa maarufu [kwa wema au kwa ubaya], Makonda wa Dar alikuwa maarufu kuliko huyo wa Arusha. Unakumbuka kilichotokea alipojaribu kugombea jimbo mojawapo la Dar? Huo umaarufu wa viongozi wa kuteuliwa huchagizwa na maigizo yao mbele ya kamera.

Uchaguzi ni kitu kingine kabisa. Wakuu wa mikoa, wilaya na wengineo ambao ni maarufu hupigwa mweleka kirahisi sana....usikariri!
Umaarufu pia hupatikana kwa kuhofiwa na watu wa chini yake. Akigombea Arusha ni aibu yake bora atulie atembelee kibao cha RC

Sent from my SM-G970U using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom