Makalla: CCM nafasi zote zipo wazi isipokuwa ya Urais

peno hasegawa

JF-Expert Member
Feb 24, 2016
14,255
23,946
IMG-20240423-WA0037.jpg

Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi, Amos Makalla amesema nafasi zote za kuchaguli katika chaguzi zijazo zipo wazi isipokuwa ya Rais wa JMT.

Akizungumza leo Aprili 20 hapa Songea mkoani Ruvuma, Makalla amewataka wana CCM kuhamasisha Vijana, Wanawake na Watu wenye ulemavu kuchukua mikopo ya halmashauri kujikwamua kiuchumi, na kuachana na mambo ya kuandamana.

"Msingi wa CCM ni katika mabalozi na matawi na CCM tunaamini mkoa wa Ruvuma ni ngome imara ya CCM na hili mtaliendeleza."

"Rais Samia kila mahali katika taifa letu ameweka alama ya maendeleo ndio maana wana CCM wote kwa pamoja tumeridhia katika kuelekea uchaguzi mwakani 2025 nafasi zote zitakuwa wazi kasoro moja ya Urais ambayo CCM tumejiridhisha kwa pamoja kuwa mgombea ni Dk. Samia Suluhu Hassan"

"Hapa mkoani Ruvuma zimetumika Sh bilioni 37 kuboresha uwanja wa ndege wa hapa Ruvuma, hiyo yote ni dhamira ya Rais Samia katika kuboresha sekta ya usafiri wa anga."

"Sh bilioni 2.1 zimetengewa hapa mkoani Ruvuma kwaajili ya mikopo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu, wakati wenzetu wanahamasisha maandamano sisi tuhamasishe watu kupata mikopo ya kujikwamua kiuchumi."
 
Kwani Filimbi imeshapulizwa na Chama?

Nimeshatenga fedha kwaajili ya Wajumbe tayari 🤗
 
Majimbo yaliyo wazi:
1. Jimbo la babsti mji
2. Hai Kilimanjaro
3. Moshi vijijini Kilimanjaro
4. Mpwapwa
5. Karatu
6. Rorya
7. Chunya
8. Lupa
9. Moshi mjini
10.
 
Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi, Amos Makalla amesema nafasi zote za kuchaguli katika chaguzi zijazo zipo wazi isipokuwa ya Rais wa JMT.

Akizungumza leo Aprili 20 hapa Songea mkoani Ruvuma, Makalla amewataka wana CCM kuhamasisha Vijana, Wanawake na Watu wenye ulemavu kuchukua mikopo ya halmashauri kujikwamua kiuchumi, na kuachana na mambo ya kuandamana.

"Msingi wa CCM ni katika mabalozi na matawi na CCM tunaamini mkoa wa Ruvuma ni ngome imara ya CCM na hili mtaliendeleza."

"Rais Samia kila mahali katika taifa letu ameweka alama ya maendeleo ndio maana wana CCM wote kwa pamoja tumeridhia katika kuelekea uchaguzi mwakani 2025 nafasi zote zitakuwa wazi kasoro moja ya Urais ambayo CCM tumejiridhisha kwa pamoja kuwa mgombea ni Dk. Samia Suluhu Hassan"

"Hapa mkoani Ruvuma zimetumika Sh bilioni 37 kuboresha uwanja wa ndege wa hapa Ruvuma, hiyo yote ni dhamira ya Rais Samia katika kuboresha sekta ya usafiri wa anga."

"Sh bilioni 2.1 zimetengewa hapa mkoani Ruvuma kwaajili ya mikopo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu, wakati wenzetu wanahamasisha maandamano sisi tuhamasishe watu kupata mikopo ya kujikwamua kiuchumi."
Screenshot_20240422-223846.jpg
 
..mambo ya kupita bila kupingwa yamezuiliwa.

..Samia ashindanishwe na wanaCcm wenzake kuamua nani awe mgombea wa Ccm.
 
Back
Top Bottom