Maisha yako ni jukumu lako

Street brain

JF-Expert Member
Oct 24, 2022
575
752
Unajua kwamba ukifa, the moment watu wamemaliza tu kukufukia(kuzikwa) dakika chache sana mbele vilio vyote vitanyamaza na watu wataacha kulia, tena wengine watakuwa wanacheka na kupiga story za kawaida kuhusu maisha yao wakati wanarudi majumbani.

Usifikirie Ndugu na familia yako wote watakaa tu wakilia muda wote, la hasha watatafuta bar ya jirani watakunywa na pombe, na wengine watazinywea hapo hapo kwenye nyumba ya msiba huku wakipiga story kuhusu yanayoendelea mtandaoni!!

Wapo watu wako wa karibu saaaana hawatakuja msibani kwako wala hawatakuja kukuzika wakisingizia wamepatwa na dharura!!

Hata mwajiri wako hatasubiri wiki iishe atakuwa ameshamtafuta wa kuku-replace na office itakusahau mazima.

Ndugu jamaa na marafiki watatawanyika jioni hiyo hiyo kurudi makwao kuendelea na shughuli zao.

Baada ya wiki watoto wako watarudi shule na kuendelea na maisha yao.

Baada ya wiki mpenzi/mke/mume wako atakuwa anatazama post za vichekesho mitandaoni na kucheka!!
UTAKUWA UMESHASAHAULIKA!!

Wapo wengine watu wako wa karibu kabisa usiowadhania usiku ule ule wa msiba wako watamfariji mke/mume/mpenzi wako na kum-seduce walale naye kimapenzi.

Wanaweza kumhadaa anywe kilevi kidogo kupunguza mawazo ya msiba wako, na kilevi kikianza kushuka hawatamuingiza ndani akapumzike, watapita naye.

Mwingine ataingia kwenye mahusiano mapya mwezi mmoja tu kabla ya 40 yako kufika!!
Ukiwa unazikwa wengine wala hawatasogelea kaburi lako kumwaga mchanga, wataishia mbali kabisa kwenye parking ya magari yao, wakiwa wanapiga story zao na kucheka na kubishana kuhusu siasa na mpira na wala hata hawatasikiliza mawaidha ya sheikh au mchungaji katika safari yako ya mwisho, ni kama wamekuja tu kukamilisha ratiba!!

NAAM UTAKUWA UMESHASAHAULIKA! TENA UTASAHAULIKA NDANI YA MUDA MFUPI SANA MARA TU BAADA YA KUFUKIWA!!

Kama watu hadi ndugu zako watakusahau kirahisi na kiwepesi hivyo, sasa UNAISHI MAISHA YAKO KWA AJILI YA NANI?

Maisha yako yote unaishi kwa kuhofia watu watakufikiriaje? watakuchukuliaje? watakuonaje?

My friend They dont!!

SO ISHI MAISHA YAKO KWA AJILI YAKO MWENYEWE!!

Unajitoa, unajinyima, unapambana,unahangaika, unateseka, unamwaga machozi, jasho na damu ili uwahudumie wengine, uwasaidie ndugu, uwaokoe marafiki na uwalinde waliokuzunguka.

TENA WAKATI MWINGINE INAKUGHARIMU HADI UHAI & AFYA YAKO KWA KUJITOA KUWASAIDIA WENGINE.

Na hao hao wanakuja kukusahau dakika chache wakishakufukia ardhini!!

NB. Sisemi usisaidie watu, ndugu, jamaa na marafiki.

Rudia tena kusoma☝️Utanielewa.
 
Who cares! Once you die, it's over, you don't exist!
 
NYIE KUFENI TU MKIDHANI WATU WATALIA ,KUMBE WANASUBIRIA MIRATHI



kazi kweli kweli/jobtruetrue
 
Mada nzuri Ila wachangiaji wanachangangia utumbo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…