SoC04 Maendeleo ya Kilimo nchini na uhifadhi wa mazingira kwa matumizi ya ardhi ya madampo kama mbolea

Tanzania Tuitakayo competition threads

Daniel Reverian

New Member
Oct 28, 2023
2
0
 Tanzania inazo sehemu nyingi za kutupa taka zinazo oza na zisizo oza sehemu hizi zinajulikana kwa jina maarufu kama dampo (jalala). Kuna namna ambavyo taka hizi zinaweza zikaleta mageuzi makubwa katika sekta ya kilimo na kusaidia katika uhifadhi wa mazingira nchini kama ifuatavyo.

1. Serikali ifanye utafiti kwenye udongo unapatikana kwenye majlala makubwa una rutuba kiasi gani na unaweza kuzalisha ama kufaa kwa kilimo cha mazao gani kisha, itengeneze mbolea ya asili kwa kuweka dawa kwa ajili ya kuuwa vijidudu ambavyo vinaweza kuleta athari kwa mazao kisha na kuigawa mbolea hiyo bure kwa wakulima mbalimbali nchini, teknolojia ya utengenezaji wa mbolea hii italeta maufaa kwa wakulima, utengezaji wa ajira kwa vijana kupitia kilimo lakini pia kwa wasomi wa masuala ya kilimo kama watafiti huku ikiipunguzia serikali gharama za ununuzi wa mbolea ghafi kwa bei kubwa kutoka nje ya nchi.

2. Baada ya ubunifu huo wa utengenezwaji wa mbolea hiyo kutoka katika majalala basi ardhi hiyo itasombwa na kupelekwa mashambani kwa ajili ya kilimo maanake eneo hilo ambalo ardhi itaondoshwa litabaki wazi kwajili ya matumizi mengine ya kuendelea kutumika kama jalala (dampo), hii itasaidia zaidi kutokuwa na sehemu nyingi kwa ajili ya kutupa taka badala yake kutakuwa na maeneo machache ambayo yatatumika na kusaidia kuendelea kuhifadhi mazingira nchini.

Teknolojia hii ya uzalishwaji wa mbolea hii itapimwa kwa kiasi gani imeleta matokeo chanya au hasi kwa walau baada ya mwaka mmoja tangu kuanza kutumika kwake, binafsi nimejaribu kutumia mbinu hii ya kuzalisha mbolea kutokea katika jalala na imeonekana kuwa na tija japo sikuifanya kisayansi zaidi kama ambavyo serikali inaweza kuifanyia utafiti wa kina zaidi.

Hii unaweza kuwa teknolojia ya bei nafuu yenye matokeo makubwa zaidi kwa taifa, sekta ya kilimo na sekta na uhifadhi wa mazingira....!
Mvuvi
 
Back
Top Bottom