SAKATA la kuondolewa kwa wafanyabiashara ndogondogo al-maarufu kama Wamachinga katika mengi nchini, kwa sasa limezua hali ya ukosefu wa amani kwa machinga hao jijini Dar es salaam.
Uamuzi huo umejaribiwa kutekelezwa karibu kila mkoa nchini lakini kwa kiasi kikubwa umekuwa ukijaribiwa sana katika Jiji la Dar es Salaam, Arusha, Mwanza na Mbeya.
Operesheni ya kuwahamisha na kuwamata wamachinga jijini Dar es Salaam imeongeza kasi ikiwa ni muda mfupi tangu wafanyabiashara hao walipoamriwa kuondoka pembezoni mwa maeneo ya barabara mpya za mwendo kasi, hali ambayo imesababisha msongamano katika eneo moja huku wizi ukipamba moto kutokana na msongamano mkubwa wa watu katika eneo dogo.
Sasa nasikia wa Mwanza wamepelekwa mbali na mji, vipi hawa wa Kariakoo bado wapo au wametupwa mbali?
Au vipi, mbona hujatuletea update kinachoendelea? wengine tuko mbali na Tanzania ya Makonda
Muda mwingine huwa nashindwa
Hata kuelewa kabisa yaani mtu
mzima na akili zake anapanga bidhaa barabarani kweli jamani
Kwa wakazi wa mwanza kama
Mna kumbukumbu kuna kipindi
Machinga waligoma kuhamishiwa
Eneo la mlango mmoja
Kwa madai hakuna watu wa kununua bidhaa zao
lakini sasa hivi mlango mmoja ni
Eneo la kibiasha zaidi kwa hiyo na hawa waende tu
KILOLELI NYEGEZI SINAI KWA KAKOBE MKUYUNI tutawafuata huko huko